TANU na Sanduku la fedha la Abdul Sykes

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,917
30,259
TANU NA SANDUKU LA FEDHA LA ABDUL SYKES 1950s

Katika moja ya mijadala ya historia ya TANU na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika niliwaahidi wasomaji wangu kuwapa historia ya sanduku la fedha la Abdul Sykes.

Nikasahau kwa muda.

Leo msomaji wangu mmoja kaniandikia kunikumbusha nitimize ahadi yangu:

Proved,
Ahadi ni deni na kesho kiyama Allah atatuuliza katika yale tuliyoahidi hatukutimiza.
Mniwie radhi kwani nilisahau.

Ili tupate picha ya Abdul Sykes niruhusini hapa niweke kipande kutoka kwa binti yake Aisha ''Daisy'' Sykes,'' kutoka makala aliyoandika mwaka wa 2018 katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake.

Aisha ‘’Daisy’’ Sykes Buruku ni binti ya Abdulwahid Sykes mmoja kati ya wazalendo 17 waliounda chama cha TANU kilichopigania uhuru wa Tanganyika.

Daisy kama anavyofahamika zaidi kwa jina hili, ni msichana wa kwanza Mwafrika kusoma Shule ya Wasichana ya Aga Khan mwanzoni mwa miaka ya 1950 na msichana wa pili kuingia Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki, Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 1960.

Daisy amefahamiana na wazalendo wengi mmoja wapo akiwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na machifu mashuhuri kama Mangi Mkuu Thomas Marealle waliokuwa wakifika nyumbani kwa baba yake wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Katika kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha baba yake, Daisy aliandika makala kukumbuka siku zile zilizojenga haiba ya baba yake na ya wazalendo walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa miaka mingi Daisy amekuwa akiishi na kufanya kazi nje ya Tanzania.

Daisy anasema: ''Wageni mashuhuri waliokuwa wakija nyumbani ni pamoja na Mangi Mkuu Thomas Marealle, Machifu Abdiel Shangali, John Maruma kutoka Moshi, Adam Sapi Mkwawa kutoka Iringa, Kidaha Makwaia kutoka Usukuma, Abdallah Fundikira, Harun Lugusha kutoka Tabora, Humbi Ziota kutoka Nzega, Michael Lukumbuzya kutoka Ukerewe na Patrick Kunambi kutoka Morogoro na wengine wengi.

(Angalia picha ya machifu wa Tanganyika hapo chini 1958).

Hawa machifu kwa kawaida walikuwa wakija na wake zao, wanawake warembo ambao hawakuacha kunifanya mimi kuwashangalia.
Nakumbuka katika machifu wale, alikuwapo chifu mmoja na wa pekee mwanamke - Mwami Theresa Ntare kutoka Kasulu Kibondo.

Lakini aliyeshika nafasi ya juu kabisa katika fikra zangu nikiwa mtoto alikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na ni kupitia kwake ndipo tukapata kujua kwa mara ya kwanza kuwa kuna kabila linaitwa, ‘’Wazanaki.’’

Kila alipokuwa anakuja nyumbani kwetu kuja kwake kulikuwa jambo maalum kulikosababisha minong’ono watu wakizungumza kwa sauti za chini wakipeana taarifa kuwa, ‘’Nyerere anakuja au keshafika.”

Kwangu mimi hii ilikuwa ishara ya kutimiza kazi yangu kwani siku zote nilikuwa nikiambiwa kutengeneza kifungua kinywa cha chai na mayai kila alipokuja nyumbani akitokea Shule ya Mt. Francis, Pugu alipokuwa akisomesha.

Nakumbuka katika akili yangu ya kitoto kumuona Mwalimu Nyerere akiishi nyumbani kwetu kwa muda katika nyumba yetu ya Mtaa wa Stanley baada ya kuacha kazi wakati marafiki zake wa karibu baba na Dossa Aziz walikuwa wanamtafutia nyumba ya kuishi.

Ilikuwa katika kipindi hiki cha mimi kuanza kupata akili katika kukua kwangu ndipo nilipokutana na wanawake wazalendo waliokuwa wanaochipukia katika uongozi wa Tanganyika, wanawake kama Bi. Lucy Lameck kutoka Moshi, Mary Ibrahim na akina mama wa Kiislam kama Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Hawa bint Maftah, hawa kutoka Dar es Salaam, wote hawa kwangu mimi walikuwa bibi zangu.

Kitu cha kufurahisha ni kuwa hawa akina mama wa Kiislam wote walivutwa katika siasa na Bibi Chiku bint Kisusa, maarufu akijulikana kama Mama Sakina.

(Angalia picha hapo chini akina mama wamevaa mabaibui wako uwanja wa ndege wanamsindikiza Julius Nyerere safari ya kwanza UNO 1955 kulia wa kwanza ni Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed na wa kwanza kushoto ni Bi. Tattu bint Mzee na Julius Nyerere huyo katikati).

Alikuwa Mama Sakina ndiye aliyewapa hawa wanawake wa Kiislam niliowataja hapo juu utambulisho na wakaja kuwa watu maarufu.

Baba yeye ndiye alikuwa kiongozi wa mikakati hii yote kwa sababu bila yeye kuwatia hima kwa kutumia ushawishi wake ingekuwa vigumu kuweza kuwatia hawa wanawake katika kuwahamasisha wanawake wenzao wa Kiislam na wao watoke majumbani kuja mstari wa mbele katika mikutano wakiimba na kutoa vibwagizo vya kuunga mkono TANU na kudai uhuru.

Hili jambo lilikuwa jipya, jambo ambalo katika utamaduni wetu kwa wakati ule halikutarajiwa na ni kinyume katika utamaduni wetu kwa wanawake wa Kiislam kulifanya katika siku zile.

Prince Karim Aga Khan alipokuja kutembelea shule yetu mwaka wa 1956, wakati ule alikuwa kijana mdogo na akakagua dafatari langu.
(Angalia picha ya Prince Karim Aga Khan hapo chini katika ujana wake).

Jambo hili halijanitoka kamwe.

Lakini zaidi ya haya uhusiano wa baba yangu na jamii ya Ismailiyya ulikuja kujitokeza kwa nguvu sana kwa uamuzi wao mwaka wa 1960 kumuuzia baba Mercedes Benz 280S, DSQ 666, ambayo ilinunuliwa makhsusi kwa matumizi ya Prince Karim Aga Khan pale alipozuru Tanganyika mwaka ule wa 1956.

Kwa siku zile hili lilikuwa jambo adhim na kubwa sana, sisi tukiwa watoto wadogo tukipakiwa na baba ndani ya gari hii nzuri na ya kifahari iliyokuwa rangi ya kijivu, hili lilikuwa jambo lisilo na mfano wake.

Baba alijikita sana katika suala la elimu. Akiwa mjumbe katika bodi ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika taasisi iliyoasisiwa na babu yangu, Abdallah Kleist Sykes mwaka wa 1933, pamoja na wenzake kama Ali Jumbe Kiro, Mzee bin Sudi na wengineo ambao hawa wote walikuwa vile vile katika African Association, alijishughulisha katika kuwaelimisha watoto wa kike.

Shule hii ya Al Jamiatulul Islamiyya iliyokuwa New Street (sasa Lumumba Avenue) jengo lake lipo hadi leo kama kielelezo cha Waislam katika kujiendeleza katika elimu.

Uhusiano wa baba yangu na shule ya Al Jamiatul Islamiyya unakwenda nyuma wakati wa utoto wake yeye akiwa mwanafunzi katika shule hii iliyojengwa na baba yake.

Mwaka wa 1936 akiwa na umri wa miaka 12 na mwanafunzi hapo shuleni alichaguliwa kusoma risala mbele ya Aga Khan, Sultan Mohamed Shah, baba yake Prince Karim Aga Khan huyu kiongozi wa Ismailiya aliepo sasa, alipoitembelea shule ya Al Jamiatul Islamiyya.

Ikatokea kuwa katika jengo hili la shule hii ya Al Jamiatul Islamiyya ndipo nilipoingizwa na baba kuanza chekechea na nikaanza kusoma Qur’an hapo nyakati za asubuhi na mchana nakwenda kusoma shule Aga Khan.

(Angalia jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika hapo chini).

Uhuru ulipokuwa dhahiri sasa unapatikana na ulipopatikana ulikuja na changamoto nyingi ambazo naamini baba hakuzitegemea.
Haitakuwa sawasawa ikiwa sitaeleza upeo wa juu wa baba yangu katika wema, huruma na unyofu aliokuwanao.

Hata nilipokuwa mtoto nilipata kushuhudia na kuona chokochoko na chuki dhidi yake bila shaka kwa ajili ya hasad kwani baba kwa kiwango chochote kile alikuwa mtu aliyefanikiwa na kwenye ngazi nyingi wengi hawakuthubutu hata kuota kukanyaga, lakini sikumuona baba kukasirika wala kutaka kulipiza kisasi.

Katika unyofu wa hali ya juu aliendelea na maisha yake.''

Ndugu zanguni,

Huyo hapo chini ndiye Abdulwahid Kleist Sykes na Mama Daisy wakiwa kwenye dhifa Government House (Ikulu) katika miaka ya 1950.
Naamini mmemwelewa alikuwa kiongozi wa namna gani katika TAA hadi TANU.

Sasa tuje kwenye lile sanduku la fedha.

Kitabu kilikuwa kimetoka na siku hiyo nilikwenda nyumbani kwa Mama Daisy kumpa nakala yake ya kitabu.
Tulikuwa tumekaa kwenye varanda yake nyumba yake Barabara ya Ali Hassan Mwinyi iliyokuwa mkabala na Hellenic Club.

Alikipokea kitabu akawa anatazama picha ya mumewe kwenye jalada na akawa kimya kwa muda mrefu.
Bila shaka alikuwa anawaza maisha aliyoishi na baba yetu wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika katika miaka ya 1950.

Mama Daisy alikuwa shoga wa marehemu mama yangu Bi. Baya bint Mohamed na nyumba zao hazikuwa mbali kwani sisi tulikuwa Mtaa wa Kipata na si mbali na Mtaa wa Aggrey.

Nyumba zao zilitenganishwa na Mtaa wa Kitchwele (sasa Uhuru Street).

Naamini kuwa ile mimi mtoto wa shoga yake kuwa ndiye niliyekuja kuandika kitabu cha Abdul Sykes, mtu ambae historia ilikuwa imemfuta bila shaka fikra hii ilikuwa ikizunguka katika kichwa chake.

''Mwanangu Mohamed, baba yako alijitolea sana katika kupigania uhuru wa Tanganyika,'' Mama Daisy alianza kusema.

Alikuwa na sanduku lake akiweka fedha zake na kila TANU wakija hapa kutaka kile au hiki yeye alikuwa anaingia ndani analifungua lile sanduku anatoa fedha kuwapa alikuwa hawarudishi mikono mitupu.

Mimi nikawa namwambia, Bwana Abdul taratibu lakini hakunisikia, hakuacha kutoa fedha kwa ajili ya chama chake.
Bwana Abdul alikuwa mtu karimu sana.''

May be a black-and-white image of 3 people and people standing

May be an image of 7 people and people standing

May be an image of 1 person and standing

May be an image of outdoors and text that says 'ÎÎ 中 30 Jengo la Jamiatul Islamia linavyoonekana leo Mtaa wa Lumum'

May be an image of 3 people and people standing


 
Watu walijitolea kukikuza chama Kwa Mali Zao like ardhi, majengo, pesa.
Lkn leo hii watu wanaiba Mali za chama bila aibu wakisema ,hiki chama ni Chao, kwaio wanayo haki ya kuiba.

History ya inchi hii inabidi iandikwe upya ili isije ikapotea. Maana iliyo kuwepo imepindisha ukweli wa Mambo
 
Watu walijitolea kukikuza chama Kwa Mali Zao like ardhi, majengo, pesa.
Lkn leo hii watu wanaiba Mali za chama bila aibu wakisema ,hiki chama ni Chao, kwaio wanayo haki ya kuiba.

History ya inchi hii inabidi iandikwe upya ili isije ikapotea. Maana iliyo kuwepo imepindisha ukweli wa Mambo
Chui,
Mwalimu Nyerere alipokuwa anaeneza TANU Kilwa alikuwa anafikia nyumbani kwa Abdulkarim Hajj Mussa Jamadari.

Huyu bwana alikuwa na pikipiki na huo ndiyo uliokuwa usafiri wake wa kumpeleka Mwalimu katika vijiji vyote.

Nyumba na pikipiki ndiyo picha hizi hapo chini:

1644639862030.png
 
TANU NA SANDUKU LA FEDHA LA ABDUL SYKES 1950s

Katika moja ya mijadala ya historia ya TANU na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika niliwaahidi wasomaji wangu kuwapa historia ya sanduku la fedha la Abdul Sykes.

Nikasahau kwa muda.

Leo msomaji wangu mmoja kaniandikia kunikumbusha nitimize ahadi yangu:

Proved,
Ahadi ni deni na kesho kiyama Allah atatuuliza katika yale tuliyoahidi hatukutimiza.
Mniwie radhi kwani nilisahau.

Ili tupate picha ya Abdul Sykes niruhusini hapa niweke kipande kutoka kwa binti yake Aisha ''Daisy'' Sykes,'' kutoka makala aliyoandika mwaka wa 2018 katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake.

Aisha ‘’Daisy’’ Sykes Buruku ni binti ya Abdulwahid Sykes mmoja kati ya wazalendo 17 waliounda chama cha TANU kilichopigania uhuru wa Tanganyika.

Daisy kama anavyofahamika zaidi kwa jina hili, ni msichana wa kwanza Mwafrika kusoma Shule ya Wasichana ya Aga Khan mwanzoni mwa miaka ya 1950 na msichana wa pili kuingia Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki, Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 1960.

Daisy amefahamiana na wazalendo wengi mmoja wapo akiwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na machifu mashuhuri kama Mangi Mkuu Thomas Marealle waliokuwa wakifika nyumbani kwa baba yake wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Katika kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha baba yake, Daisy aliandika makala kukumbuka siku zile zilizojenga haiba ya baba yake na ya wazalendo walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa miaka mingi Daisy amekuwa akiishi na kufanya kazi nje ya Tanzania.

Daisy anasema: ''Wageni mashuhuri waliokuwa wakija nyumbani ni pamoja na Mangi Mkuu Thomas Marealle, Machifu Abdiel Shangali, John Maruma kutoka Moshi, Adam Sapi Mkwawa kutoka Iringa, Kidaha Makwaia kutoka Usukuma, Abdallah Fundikira, Harun Lugusha kutoka Tabora, Humbi Ziota kutoka Nzega, Michael Lukumbuzya kutoka Ukerewe na Patrick Kunambi kutoka Morogoro na wengine wengi.

(Angalia picha ya machifu wa Tanganyika hapo chini 1958).

Hawa machifu kwa kawaida walikuwa wakija na wake zao, wanawake warembo ambao hawakuacha kunifanya mimi kuwashangalia.
Nakumbuka katika machifu wale, alikuwapo chifu mmoja na wa pekee mwanamke - Mwami Theresa Ntare kutoka Kasulu Kibondo.

Lakini aliyeshika nafasi ya juu kabisa katika fikra zangu nikiwa mtoto alikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na ni kupitia kwake ndipo tukapata kujua kwa mara ya kwanza kuwa kuna kabila linaitwa, ‘’Wazanaki.’’

Kila alipokuwa anakuja nyumbani kwetu kuja kwake kulikuwa jambo maalum kulikosababisha minong’ono watu wakizungumza kwa sauti za chini wakipeana taarifa kuwa, ‘’Nyerere anakuja au keshafika.”

Kwangu mimi hii ilikuwa ishara ya kutimiza kazi yangu kwani siku zote nilikuwa nikiambiwa kutengeneza kifungua kinywa cha chai na mayai kila alipokuja nyumbani akitokea Shule ya Mt. Francis, Pugu alipokuwa akisomesha.

Nakumbuka katika akili yangu ya kitoto kumuona Mwalimu Nyerere akiishi nyumbani kwetu kwa muda katika nyumba yetu ya Mtaa wa Stanley baada ya kuacha kazi wakati marafiki zake wa karibu baba na Dossa Aziz walikuwa wanamtafutia nyumba ya kuishi.

Ilikuwa katika kipindi hiki cha mimi kuanza kupata akili katika kukua kwangu ndipo nilipokutana na wanawake wazalendo waliokuwa wanaochipukia katika uongozi wa Tanganyika, wanawake kama Bi. Lucy Lameck kutoka Moshi, Mary Ibrahim na akina mama wa Kiislam kama Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Hawa bint Maftah, hawa kutoka Dar es Salaam, wote hawa kwangu mimi walikuwa bibi zangu.

Kitu cha kufurahisha ni kuwa hawa akina mama wa Kiislam wote walivutwa katika siasa na Bibi Chiku bint Kisusa, maarufu akijulikana kama Mama Sakina.

(Angalia picha hapo chini akina mama wamevaa mabaibui wako uwanja wa ndege wanamsindikiza Julius Nyerere safari ya kwanza UNO 1955 kulia wa kwanza ni Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed na wa kwanza kushoto ni Bi. Tattu bint Mzee na Julius Nyerere huyo katikati).

Alikuwa Mama Sakina ndiye aliyewapa hawa wanawake wa Kiislam niliowataja hapo juu utambulisho na wakaja kuwa watu maarufu.

Baba yeye ndiye alikuwa kiongozi wa mikakati hii yote kwa sababu bila yeye kuwatia hima kwa kutumia ushawishi wake ingekuwa vigumu kuweza kuwatia hawa wanawake katika kuwahamasisha wanawake wenzao wa Kiislam na wao watoke majumbani kuja mstari wa mbele katika mikutano wakiimba na kutoa vibwagizo vya kuunga mkono TANU na kudai uhuru.

Hili jambo lilikuwa jipya, jambo ambalo katika utamaduni wetu kwa wakati ule halikutarajiwa na ni kinyume katika utamaduni wetu kwa wanawake wa Kiislam kulifanya katika siku zile.

Prince Karim Aga Khan alipokuja kutembelea shule yetu mwaka wa 1956, wakati ule alikuwa kijana mdogo na akakagua dafatari langu.
(Angalia picha ya Prince Karim Aga Khan hapo chini katika ujana wake).

Jambo hili halijanitoka kamwe.

Lakini zaidi ya haya uhusiano wa baba yangu na jamii ya Ismailiyya ulikuja kujitokeza kwa nguvu sana kwa uamuzi wao mwaka wa 1960 kumuuzia baba Mercedes Benz 280S, DSQ 666, ambayo ilinunuliwa makhsusi kwa matumizi ya Prince Karim Aga Khan pale alipozuru Tanganyika mwaka ule wa 1956.

Kwa siku zile hili lilikuwa jambo adhim na kubwa sana, sisi tukiwa watoto wadogo tukipakiwa na baba ndani ya gari hii nzuri na ya kifahari iliyokuwa rangi ya kijivu, hili lilikuwa jambo lisilo na mfano wake.

Baba alijikita sana katika suala la elimu. Akiwa mjumbe katika bodi ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika taasisi iliyoasisiwa na babu yangu, Abdallah Kleist Sykes mwaka wa 1933, pamoja na wenzake kama Ali Jumbe Kiro, Mzee bin Sudi na wengineo ambao hawa wote walikuwa vile vile katika African Association, alijishughulisha katika kuwaelimisha watoto wa kike.

Shule hii ya Al Jamiatulul Islamiyya iliyokuwa New Street (sasa Lumumba Avenue) jengo lake lipo hadi leo kama kielelezo cha Waislam katika kujiendeleza katika elimu.

Uhusiano wa baba yangu na shule ya Al Jamiatul Islamiyya unakwenda nyuma wakati wa utoto wake yeye akiwa mwanafunzi katika shule hii iliyojengwa na baba yake.

Mwaka wa 1936 akiwa na umri wa miaka 12 na mwanafunzi hapo shuleni alichaguliwa kusoma risala mbele ya Aga Khan, Sultan Mohamed Shah, baba yake Prince Karim Aga Khan huyu kiongozi wa Ismailiya aliepo sasa, alipoitembelea shule ya Al Jamiatul Islamiyya.

Ikatokea kuwa katika jengo hili la shule hii ya Al Jamiatul Islamiyya ndipo nilipoingizwa na baba kuanza chekechea na nikaanza kusoma Qur’an hapo nyakati za asubuhi na mchana nakwenda kusoma shule Aga Khan.

(Angalia jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika hapo chini).

Uhuru ulipokuwa dhahiri sasa unapatikana na ulipopatikana ulikuja na changamoto nyingi ambazo naamini baba hakuzitegemea.
Haitakuwa sawasawa ikiwa sitaeleza upeo wa juu wa baba yangu katika wema, huruma na unyofu aliokuwanao.

Hata nilipokuwa mtoto nilipata kushuhudia na kuona chokochoko na chuki dhidi yake bila shaka kwa ajili ya hasad kwani baba kwa kiwango chochote kile alikuwa mtu aliyefanikiwa na kwenye ngazi nyingi wengi hawakuthubutu hata kuota kukanyaga, lakini sikumuona baba kukasirika wala kutaka kulipiza kisasi.

Katika unyofu wa hali ya juu aliendelea na maisha yake.''

Ndugu zanguni,

Huyo hapo chini ndiye Abdulwahid Kleist Sykes na Mama Daisy wakiwa kwenye dhifa Government House (Ikulu) katika miaka ya 1950.
Naamini mmemwelewa alikuwa kiongozi wa namna gani katika TAA hadi TANU.

Sasa tuje kwenye lile sanduku la fedha.

Kitabu kilikuwa kimetoka na siku hiyo nilikwenda nyumbani kwa Mama Daisy kumpa nakala yake ya kitabu.
Tulikuwa tumekaa kwenye varanda yake nyumba yake Barabara ya Ali Hassan Mwinyi iliyokuwa mkabala na Hellenic Club.

Alikipokea kitabu akawa anatazama picha ya mumewe kwenye jalada na akawa kimya kwa muda mrefu.
Bila shaka alikuwa anawaza maisha aliyoishi na baba yetu wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika katika miaka ya 1950.

Mama Daisy alikuwa shoga wa marehemu mama yangu Bi. Baya bint Mohamed na nyumba zao hazikuwa mbali kwani sisi tulikuwa Mtaa wa Kipata na si mbali na Mtaa wa Aggrey.

Nyumba zao zilitenganishwa na Mtaa wa Kitchwele (sasa Uhuru Street).

Naamini kuwa ile mimi mtoto wa shoga yake kuwa ndiye niliyekuja kuandika kitabu cha Abdul Sykes, mtu ambae historia ilikuwa imemfuta bila shaka fikra hii ilikuwa ikizunguka katika kichwa chake.

''Mwanangu Mohamed, baba yako alijitolea sana katika kupigania uhuru wa Tanganyika,'' Mama Daisy alianza kusema.

Alikuwa na sanduku lake akiweka fedha zake na kila TANU wakija hapa kutaka kile au hiki yeye alikuwa anaingia ndani analifungua lile sanduku anatoa fedha kuwapa alikuwa hawarudishi mikono mitupu.

Mimi nikawa namwambia, Bwana Abdul taratibu lakini hakunisikia, hakuacha kutoa fedha kwa ajili ya chama chake.
Bwana Abdul alikuwa mtu karimu sana.''

May be a black-and-white image of 3 people and people standing

May be an image of 7 people and people standing

May be an image of 1 person and standing

May be an image of outdoors and text that says 'ÎÎ 中 30 Jengo la Jamiatul Islamia linavyoonekana leo Mtaa wa Lumum''ÎÎ 中 30 Jengo la Jamiatul Islamia linavyoonekana leo Mtaa wa Lumum'

May be an image of 3 people and people standing


Mzee mwenzangu, unakumbuka mama wa kimanyema aliyetoa jengo lake ili liwe afisi ya TANU pale Lumumba? Na sasa ndipo Afisi Ndogo ya ccm
 
Chui,
Mwalimu Nyerere alipokuwa anaeneza TANU Kilwa alikuwa anafikia nyumbani kwa Abdulkarim Hajj Mussa Jamadari.

Huyu bwana alikuwa na pikipiki na huo ndiyo uliokuwa usafiri wake wa kumpeleka Mwalimu katika vijiji vyote.

Nyumba na pikipiki ndiyo picha hizi hapo chini:

View attachment 2116805
Wapigania Uhuru wamebaki kuwa masikini kabisa, history Yao inafichwa fichwa Tu😭😭
 
Mzee mwenzangu, unakumbuka mama wa kimanyema aliyetoa jengo lake ili liwe afisi ya TANU pale Lumumba? Na sasa ndipo Afisi Ndogo ya ccm
Kolola,
Hapana haikuwa hivyo.

African Association imeundwa na wazalendo hawa wafuatao: Cecil Matola (President), Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ali Said Mpima, Rawson Watts, Raikes Kusi, Zibe Kidasi na Suleiman Majisu mwaka wa 1929.

Kuazia 1929 - 1933 walijenga ofisi hapo New Street kona na Kariakoo.

Jengo hili lilifunguliwa na Gavana Donald Cameron.

Angalia picha hapo chini:

1644692041484.png
 
Abdul kleist sykes

What was he doing for living that time?
The...
Abdul Sykes alikuwa Market Master, Kariakoo Market.
Nafasi hii ilikuwa imeshikwa na Mwingereza anaitwa Brian Hodges.

Alipotoka Abdul Sykes akachukua nafasi hiyo.
Alikuwa pia na family business.

1644692509693.jpeg

Soko la Kariakoo katika 1950s hiyo nyumba ndogo kulia ndiyo ilikuwa ofisi ya Market Master
 
Kolola,
Hapana haikuwa hivyo.

African Association imeundwa na wazalendo hawa wafuatao: Cecil Matola (President), Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ali Said Mpima, Rawson Watts, Raikes Kusi, Zibe Kidasi na Suleiman Majisu mwaka wa 1929.

Kuazia 1929 - 1933 walijenga ofisi hapo New Street kona na Kariakoo.

Jengo hili lilifunguliwa na Gavana Donald Cameron.

Angalia picha hapo chini:

View attachment 2117664
Mzee mwenzangu, hiyo si sawa! Mama wa kimanyema ndiye aliyetoa jengo lililoandikwa ‘katika jengo hili ndipo TANU ilizaliwa’ hilo jengo lilikuja kukarabatiwa na JK alipokuwa Rais juzi juzi. Unalosema ni jengo sasa hivi la umoja wa wazazi pale karibu na Soko la Kariakoo- ambalo sina uhakika na historia yake
 
Mzee mwenzangu, hiyo si sawa! Mama wa kimanyema ndiye aliyetoa jengo lililoandikwa ‘katika jengo hili ndipo TANU ilizaliwa’ hilo jengo lilikuja kukarabatiwa na JK alipokuwa Rais juzi juzi. Unalosema ni jengo sasa hivi la umoja wa wazazi pale karibu na Soko la Kariakoo- ambalo sina uhakika na historia yake
Kolola,
Kabla hajafariki Kleist Sykes aliandika maisha yake na huu kama mswada wa kitabu alimwachia mwanae Abdul Sykes.

Mwaka wa 1968 bint yake Aisha ''Daisy'' Sykes akiwa mwanafunzi wa Education and History, University of East Africa, Dar es Salaam chini ya John Iliffe alitumia mswada huu kuandika seminar paper kuhusu maisha ya babu yake, Kleist Sykes.

(Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95-114).

Hii seminar paper kama ulivyosoma hapo juu ni moja ya sura katika kitabu alichohariri Iliffe, ''Modern Tanzanians,'' (1973).

Kleist Sykes katika ameeleza jinsi walivyojenga nyumba hiyo kwa kujitolea kila Jumapili na picha ya sherehe ya ufunguzi ndiyo hiyo nimeweka kutoka Nyaraka za Sykes.

Nyuma ya nyumba hii ni nyumba ya Sheikh Haidar Mwinyimvua (1905 - 1907) aliyekuwa mmoja wa wazee waliokuwa mstari wa mbele katika TANU.

Nyumba hii akiishi mama yake Bi. Mwamtoro bint Chuma mmoja wa akina mama waiounga mkono TANU.

Ilikuwa TANU wakiwa na mkutano wa ndani walikuwa wanaondoa ua makuti katika ya nyumba hizi hizi mbili na kuwa na nafasi ya kutosha kuenea wanawake na wanaume.

Wanawake wakikaa nyuma na wanaume mbele.

Naijua vizuri sana historia ya TANU kwa kuwa ni historia ya wazee wangu na nimeipokea vizuri kutoka kwao.

1644726442770.png

Nyumba ya Bi. Mwamtoro bint Chuma ambayo TANU ikifanya mikutano yake ya ndani

1644726567290.png

Bi. Mwamtoro bint Chuma akipiga kura Uchaguzi wa 1970
 
Kolola,
Kabla hajafariki Kleist Sykes aliandika maisha yake na huu kama mswada wa kitabu alimwachia mwanae Abdul Sykes.

Mwaka wa 1968 bint yake Aisha ''Daisy'' Sykes akiwa mwanafunzi wa Education and History, University of East Africa, Dar es Salaam chini ya John Iliffe alitumia mswada huu kuandika seminar paper kuhusu maisha ya babu yake, Kleist Sykes.

(Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95-114).

Hii seminar paper kama ulivyosoma hapo juu ni moja ya sura katika kitabu alichohariri Iliffe, ''Modern Tanzanians,'' (1973).

Kleist Sykes katika ameeleza jinsi walivyojenga nyumba hiyo kwa kujitolea kila Jumapili na picha ya sherehe ya ufunguzi ndiyo hiyo nimeweka kutoka Nyaraka za Sykes.

Nyuma ya nyumba hii ni nyumba ya Sheikh Haidar Mwinyimvua (1905 - 1907) aliyekuwa mmoja wa wazee waliokuwa mstari wa mbele katika TANU.

Nyumba hii akiishi mama yake Bi. Mwamtoro bint Chuma mmoja wa akina mama waiounga mkono TANU.

Ilikuwa TANU wakiwa na mkutano wa ndani walikuwa wanaondoa ua makuti katika ya nyumba hizi hizi mbili na kuwa na nafasi ya kutosha kuenea wanawake na wanaume.

Wanawake wakikaa nyuma na wanaume mbele.

Naijua vizuri sana historia ya TANU kwa kuwa ni historia ya wazee wangu na nimeipokea vizuri kutoka kwao.

View attachment 2117935
Nyumba ya Bi. Mwamtoro bint Chuma ambayo TANU ikifanya mikutano yake ya ndani

View attachment 2117942
Bi. Mwamtoro bint Chuma akipiga kura Uchaguzi wa 1970
Unachanganya madesa hii kitu ninachokueleza kuna maandishi yake naweza kukuonesha pale Lumumba. Si hiyo unayoonesha bwana. Nyumba yenyewe ipo kwenye kona ambayo upande wa pili ni magazeti ya Uhuru!!!!!!!!!!!!
 
Unachanganya madesa hii kitu ninachokueleza kuna maandishi yake naweza kukuonesha pale Lumumba. Si hiyo unayoonesha bwana. Nyumba yenyewe ipo kwenye kona ambayo upande wa pili ni magazeti ya Uhuru!!!!!!!!!!!!
Kolola,
Kitu cha kwanza ninachokuomba ukiwa katika mjadala na mimi naomba lugha tutumie lugha za kistaarabu na tujadili kwa utulivu.

Lugha za ''kuchanganya madesa,'' hapa si mahali pake ndani ya mjadala na kwa mtu unaejadiliananae.

Mimi chanzo changu ni Nyaraka za Sykes na Kleist Sykes katibu muasisi wa African Association kaeleza ujenzi wa ofisi ya African Association na picha ya siku ya ufunguzi nimeweka na Kleist mwenyewe yupo katika hiyo picha pamoja na ndugu yake Ramadhani Mashado Plantan.

Katika kitabu hicho cha Iliffe (1973) Abdul Sykes anaeleza kuwa yeye alipokuwa mtoto mdogo baba yake alikuwa anamchukua kwenda na yeye kwenye ujenzi huu na kaona ofisi ikijengwa kwa macho yake.

Sikulazimishi kuniamini.

1644753386509.png

Ofisi ya African Association ni hiyo hapo kwenye kona ya iliyokuwa New Street (Lumumba Avenue) na Kariakoo na hapo ndipo ilipozaliwa TANU 1954.

1644753646731.png

Katika waaasisi 17 hakuna aliyekuwa anaijua historia ya TANU kushinda Abdul Sykes.

Yeye kaona jengo hilo likijengwa na pia baba yake kamuachia mswada wa kitabu wa historia ya maisha yake na historia ya African Association.
 
History ya Sykes ni fake maana ni biased! Kesho nitapiga picha document kutoka ccm. Kuchanganya madesa ni polite way ya kusema umefuanganya! Usipende kulazimisha Hoja zako katika mjadala
 
History ya Sykes ni fake maana ni biased! Kesho nitapiga picha document kutoka ccm. Kuchanganya madesa ni polite way ya kusema umefuanganya! Usipende kulazimisha Hoja zako katika mjadala
Kolola,
Silazimishi chochote huwa naeleza kile ninachokijua.
Wala sihamaki na kumtolea mtu jeuri au kutumia maneno yasiyopendeza.

Unaweza kupitia makala zangu na hayo utayaona.
Kuwa historia ya Abdul Sykes ni ''fake'' nitakueleza kuwa si kweli.

Ikiwa Sykes si kweli nani atakuwa kweli katika historia ya uhuru wa Tanganyika?

Katika wazalendo walioasisi African Association 1929 ni Kleist peke yake aliyeandika historia ya chama hicho.

Ushahidi utaupata Maktaba ya Chuo Kikuu, East Africana seminar paper ya A.D. Sykes ''The Life of Kleist Sykes,'' University of Dar es Salaam Ref. No. JAN/HIST/143/15).

Unaweze pia ukaangalia pia machapisho ya John Iliffe, ''The Role of the African Association in the formation and Realisation of Territorial Consciousness in Tanzania,'' University of East Africa Social Science Conference, 1968.

Halikadhalika unaweza kuangalia pia nyaraka za kikachero za Special Branch Tanganyika Political Intelligence Summary.

Nakuwekea hapo chini:

Mohamed Said: TANGANYIKA POLITICAL INTELLIGENCE SUMMARY, MARCH 1952

"Tanganyika Political Intelligence
Summary, March 1952":

"...it is reported that the Secretary of the Association, Abdul Wahid Sykes has
dispatched letters to all branches asking members for suggestions under
the following heads for a memorandum to be prepared for the Royal
Commission..."

“...Abdul Wahid Kleist Sykes, Secretary of the African Association who, as
reported in last month's summary (paragraph 20) was going on safari up
country, visited Mwanza, where he met Paul Bomani, President of the
Bukoba African Association, and accompanied him to Bukoba. Sykes then
visited Kampala alone.....on 8th March, a secret meeting was held, attended
by leading members of the Mwanza Branch...”

(Hizi ni taarifa kutoka Rhodes House Library, Oxford kutoka majalada ya
kikachero ya Waingereza baada ya miaka 50 yanawekwa wazi kwa mtafiti
yeyote kuyasoma na kufanya nakala akipenda).

Ukipenda unaweza pia kuwatazama akina Sykes katika Dictionary of African Biography, Oxford University Press, New York 2011.

1644781923764.png


1644780846373.png





 

Similar Discussions

Back
Top Bottom