Dully Sykes

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,925
30,273
DULLY SYKES

Hukaa nikarudi nyuma sana katika fikra.

Ilikuwa mwaka wa 1968 mimi na Ebby Sykes tumekaa kwenye kibaraza cha nyumba moja Mtaa wa Mchikichi na Livingstone.

Ebby alikuwa ndiyo kafiwa karibuni na baba yake.

Hapo si mbali sana na kwao nyumbani kwa bibi yake Bi. Mruguru bint Mussa.

Ebby kwa siku hizo namkumbuka kila akitoka amepiga suruali ambayo kiuno ni kikubwa anaikazia na mkanda kisha juu wakati mwingine amevaa koti zuri na shati la kuvutia.

Hizi zilikuwa nguo alizoacha marehemu baba yake Abdulwahid Sykes.

Siku ile Ebby alikuja pale barazani na guitar zuri la umeme akawa anafanya mazoezi kupiga nyimbo moja ya Sam and Dave, "Hold On I am Coming."

Guitar hili katoka nalo nyumbani kwao na lina historia ndefu...
Ni miaka mingi imepita.

Rafiki yangu Ebby katangulia mbele ya haki.

Nataka leo niandike kitu kuhusu mwanae Abdulwahid maarufu kwa jina la Dully.

Nilipanda basi la Tahmeed na Dully sote tunakwenda Mombasa.
Ilikuwa mwaka wa 2014.

Nikamuona Dully na team yake nzima wamefika lakini wamesimama nje ya ofisi ya Tahmeed.

Wanakwenda kutumbuiza Mombasa.
Hili ni basi la kwanza Alfajir saa 11.

Dully hanifahumu.

Mimi nikashuka kwenye basi nikamwendea pale aliposimama nikamtolea salaam.

Akaniitikia kwa adabu sana.

Hapo nikajitambulisha na kumtaja baba yake, Ebbie nikamwambia, "Mimi na baba yako Ebbie tumepishana kuzaliwa kwa siku moja yeye kanitangulia, siku ya pili nikazaliwa mimi na siku zote tumekuwa marafiki ndugu.

Mpe salamu zangu mwambie tumekutana."

Siku narudi kufika Likoni Ferry nikaona hiyo flyer ya jina la Dully Sykes inatangaza show yake.

Haraka nikapiga picha huku basi linakwenda na nashindwa kupata jina la Dully kwa ajili ya upepo uliokuwa ukipindua hiyo flyer.

Picha hii nilikuwa sijaiweka popote.
Nikakutana na Dully kwenye maziko ya baba yake.

Hatukukutana tena hadi kwenye Khitma nyumbani kwa Mama Ali aliyekuwa mke wa Aziz Ali.

Kumbe Dully alipozungumza na baba yake akamwambia Mohamed anatujua sisi sote kwani watu wa Gerezani wakijuana na kuishi kama ndugu miaka na miaka kabla hata sisi hatujazaliwa.

Dully akanifuata akaniambia, "Uncle Mohamed wewe umeandika kitabu cha babu yangu, hebu niambie babu yangu alikuwaje."

"Dully babu yako alikuwa akikata mitaa ya Dar es Salaam anaendesha Mercedes Benz yake na vijana wa Kariakoo waliokuwa na Mercedes alikuwa babu yako Abdulwahid Sykes na kijana mmoja wa Kiarabu Abbas Abdulwahab."

Dully aliruka akapiga kelele kashika kichwa akawageukia wenzake, "Mmesikia? Babu yangu akiendesha Mercedes."

Dully akanigeukia akasema, "Uncle mimi nilikuwa na Mercedes nikapatanayo ajali Sea View."

Dully akawa kafurahi sana.

Sikutaka kumwambia kuwa baba yake mkubwa Kleist na yeye akiendesha Mercedes mji huu huu wa Dar es Salaam katika miaka ya 1980s.

Picha ya tatu ni Mwandishi na Ebby Sykes picha hii tulipiga mwaka wa 2010.

1701226304544.png

1701226415592.png

1701226450974.png

1701226538529.png
 
Uliposema unataka kuandika kitu juu yake nikajiandaa kusoma historia yake tokea wakati anazaliwa ukiwa unamuona kwa jinsi mlivyoshibana na baba yake…

Makuzi yake na utotoni alikuwa mtoto wa aina gani?
Mzee wangu leo umeniangusha, hii sio story iliyoshiba kama story zako nyingine.

Hii ingependeza zaidi maana ni msanii mkubwa ambaye wengi tumekua tukiwa tunapenda muziki wake, kiu ya kumfahamu kutoka kwa mtu wa karibu na baba yake ni kubwa!
 
Uliposema unataka kuandika kitu juu yake nikajiandaa kusoma historia yake tokea wakati anazaliwa ukiwa unamuona kwa jinsi mlivyoshibana na baba yake…

Makuzi yake na utotoni alikuwa mtoto wa aina gani?
Mzee wangu leo umeniangusha, hii sio story iliyoshiba kama story zako nyingine.

Hii ingependeza zaidi maana ni msanii mkubwa ambaye wengi tumekua tukiwa tunapenda muziki wake, kiu ya kumfahamu kutoka kwa mtu wa karibu na baba yake ni kubwa!
Nifah,
Bahati mbaya simfahamu Dully Sykes kiasi cha kuandika hayo uliyotegemea ingawa nikimfahamu marehemu mama yake.
 
DULLY SYKES

Hukaa nikarudi nyuma sana katika fikra.

Ilikuwa mwaka wa 1968 mimi na Ebby Sykes tumekaa kwenye kibaraza cha nyumba moja Mtaa wa Mchikichi na Livingstone.

Ebby alikuwa ndiyo kafiwa karibuni na baba yake.

Hapo si mbali sana na kwao nyumbani kwa bibi yake Bi. Mruguru bint Mussa.

Ebby kwa siku hizo namkumbuka kila akitoka amepiga suruali ambayo kiuno ni kikubwa anaikazia na mkanda kisha juu wakati mwingine amevaa koti zuri na shati la kuvutia.

Hizi zilikuwa nguo alizoacha marehemu baba yake Abdulwahid Sykes.

Siku ile Ebby alikuja pale barazani na guitar zuri la umeme akawa anafanya mazoezi kupiga nyimbo moja ya Sam and Dave, "Hold On I am Coming."

Guitar hili katoka nalo nyumbani kwao na lina historia ndefu...
Ni miaka mingi imepita.

Rafiki yangu Ebby katangulia mbele ya haki.

Nataka leo niandike kitu kuhusu mwanae Abdulwahid maarufu kwa jina la Dully.

Nilipanda basi la Tahmeed na Dully sote tunakwenda Mombasa.
Ilikuwa mwaka wa 2014.

Nikamuona Dully na team yake nzima wamefika lakini wamesimama nje ya ofisi ya Tahmeed.

Wanakwenda kutumbuiza Mombasa.
Hili ni basi la kwanza Alfajir saa 11.

Dully hanifahumu.

Mimi nikashuka kwenye basi nikamwendea pale aliposimama nikamtolea salaam.

Akaniitikia kwa adabu sana.

Hapo nikajitambulisha na kumtaja baba yake, Ebbie nikamwambia, "Mimi na baba yako Ebbie tumepishana kuzaliwa kwa siku moja yeye kanitangulia, siku ya pili nikazaliwa mimi na siku zote tumekuwa marafiki ndugu.

Mpe salamu zangu mwambie tumekutana."

Siku narudi kufika Likoni Ferry nikaona hiyo flyer ya jina la Dully Sykes inatangaza show yake.

Haraka nikapiga picha huku basi linakwenda na nashindwa kupata jina la Dully kwa ajili ya upepo uliokuwa ukipindua hiyo flyer.

Picha hii nilikuwa sijaiweka popote.
Nikakutana na Dully kwenye maziko ya baba yake.

Hatukukutana tena hadi kwenye Khitma nyumbani kwa Mama Ali aliyekuwa mke wa Aziz Ali.

Kumbe Dully alipozungumza na baba yake akamwambia Mohamed anatujua sisi sote kwani watu wa Gerezani wakijuana na kuishi kama ndugu miaka na miaka kabla hata sisi hatujazaliwa.

Dully akanifuata akaniambia, "Uncle Mohamed wewe umeandika kitabu cha babu yangu, hebu niambie babu yangu alikuwaje."

"Dully babu yako alikuwa akikata mitaa ya Dar es Salaam anaendesha Mercedes Benz yake na vijana wa Kariakoo waliokuwa na Mercedes alikuwa babu yako Abdulwahid Sykes na kijana mmoja wa Kiarabu Abbas Abdulwahab."

Dully aliruka akapiga kelele kashika kichwa akawageukia wenzake, "Mmesikia? Babu yangu akiendesha Mercedes."

Dully akanigeukia akasema, "Uncle mimi nilikuwa na Mercedes nikapatanayo ajali Sea View."

Dully akawa kafurahi sana.

Sikutaka kumwambia kuwa baba yake mkubwa Kleist na yeye akiendesha Mercedes mji huu huu wa Dar es Salaam katika miaka ya 1980s.

Picha ya tatu ni Mwandishi na Ebby Sykes picha hii tulipiga mwaka wa 2010.

View attachment 2828162
View attachment 2828164
View attachment 2828165
View attachment 2828167
Hakika Tanzania hatujui kuvitumia vipaji vya uandishi kama vya huyu mzee mohamed.

Watu wengi maarufu wangekuwa wanakulipa pesa na kuwaandikia historia zao kwenye maandishi una muundo mzuri sana na wakuvutia wa uandishi wa kipekee sana..
 
Nifah,
Bahati mbaya simfahamu Dully Sykes kiasi cha kuandika hayo uliyotegemea ingawa nikimfahamu marehemu mama yake.
Aisee; Kwahio heading; Ujumbe na mjadala mzima ni kuhusu mtu usiyemfahamu bali mama yake ? Sasa hii tukisema ni Click Bait tutakuwa tumekuonea ?

Ninamiss sana enzi ambapo heading tu inakuwa imekuelewesha nini kilichomo na sio heading (kichwa) na kiwiliwili (content) ni Mafuta na Maji
 
DULLY SYKES

Hukaa nikarudi nyuma sana katika fikra.

Ilikuwa mwaka wa 1968 mimi na Ebby Sykes tumekaa kwenye kibaraza cha nyumba moja Mtaa wa Mchikichi na Livingstone.

Ebby alikuwa ndiyo kafiwa karibuni na baba yake.

Hapo si mbali sana na kwao nyumbani kwa bibi yake Bi. Mruguru bint Mussa.

Ebby kwa siku hizo namkumbuka kila akitoka amepiga suruali ambayo kiuno ni kikubwa anaikazia na mkanda kisha juu wakati mwingine amevaa koti zuri na shati la kuvutia.

Hizi zilikuwa nguo alizoacha marehemu baba yake Abdulwahid Sykes.

Siku ile Ebby alikuja pale barazani na guitar zuri la umeme akawa anafanya mazoezi kupiga nyimbo moja ya Sam and Dave, "Hold On I am Coming."

Guitar hili katoka nalo nyumbani kwao na lina historia ndefu...
Ni miaka mingi imepita.

Rafiki yangu Ebby katangulia mbele ya haki.

Nataka leo niandike kitu kuhusu mwanae Abdulwahid maarufu kwa jina la Dully.

Nilipanda basi la Tahmeed na Dully sote tunakwenda Mombasa.
Ilikuwa mwaka wa 2014.

Nikamuona Dully na team yake nzima wamefika lakini wamesimama nje ya ofisi ya Tahmeed.

Wanakwenda kutumbuiza Mombasa.
Hili ni basi la kwanza Alfajir saa 11.

Dully hanifahumu.

Mimi nikashuka kwenye basi nikamwendea pale aliposimama nikamtolea salaam.

Akaniitikia kwa adabu sana.

Hapo nikajitambulisha na kumtaja baba yake, Ebbie nikamwambia, "Mimi na baba yako Ebbie tumepishana kuzaliwa kwa siku moja yeye kanitangulia, siku ya pili nikazaliwa mimi na siku zote tumekuwa marafiki ndugu.

Mpe salamu zangu mwambie tumekutana."

Siku narudi kufika Likoni Ferry nikaona hiyo flyer ya jina la Dully Sykes inatangaza show yake.

Haraka nikapiga picha huku basi linakwenda na nashindwa kupata jina la Dully kwa ajili ya upepo uliokuwa ukipindua hiyo flyer.

Picha hii nilikuwa sijaiweka popote.
Nikakutana na Dully kwenye maziko ya baba yake.

Hatukukutana tena hadi kwenye Khitma nyumbani kwa Mama Ali aliyekuwa mke wa Aziz Ali.

Kumbe Dully alipozungumza na baba yake akamwambia Mohamed anatujua sisi sote kwani watu wa Gerezani wakijuana na kuishi kama ndugu miaka na miaka kabla hata sisi hatujazaliwa.

Dully akanifuata akaniambia, "Uncle Mohamed wewe umeandika kitabu cha babu yangu, hebu niambie babu yangu alikuwaje."

"Dully babu yako alikuwa akikata mitaa ya Dar es Salaam anaendesha Mercedes Benz yake na vijana wa Kariakoo waliokuwa na Mercedes alikuwa babu yako Abdulwahid Sykes na kijana mmoja wa Kiarabu Abbas Abdulwahab."

Dully aliruka akapiga kelele kashika kichwa akawageukia wenzake, "Mmesikia? Babu yangu akiendesha Mercedes."

Dully akanigeukia akasema, "Uncle mimi nilikuwa na Mercedes nikapatanayo ajali Sea View."

Dully akawa kafurahi sana.

Sikutaka kumwambia kuwa baba yake mkubwa Kleist na yeye akiendesha Mercedes mji huu huu wa Dar es Salaam katika miaka ya 1980s.

Picha ya tatu ni Mwandishi na Ebby Sykes picha hii tulipiga mwaka wa 2010.

View attachment 2828162
View attachment 2828164
View attachment 2828165
View attachment 2828167
Mimi nikifahamu sykes bottlers hii kiswahili ya moud saidi unaipata mwarongo na tambarani kule pwani za tangatu inaleta raha sana akisimulia jambo!
 
Uliposema unataka kuandika kitu juu yake nikajiandaa kusoma historia yake tokea wakati anazaliwa ukiwa unamuona kwa jinsi mlivyoshibana na baba yake…

Makuzi yake na utotoni alikuwa mtoto wa aina gani?
Mzee wangu leo umeniangusha, hii sio story iliyoshiba kama story zako nyingine.

Hii ingependeza zaidi maana ni msanii mkubwa ambaye wengi tumekua tukiwa tunapenda muziki wake, kiu ya kumfahamu kutoka kwa mtu wa karibu na baba yake ni kubwa!

Amesema anamjua mzee wa Dully sykes "Ebe" Lakini hajamzungumzia kwa lolote, labda kwa sababu hana kitu chochote kinachoendana na yale anayoyapigania "Historia ya waislamu Tanganyika".

Mzee wake Dully ukimuangalia tu alikuwa na usasa mwingi hivyo, sidhani hata hiyo consciousness ya kisiasa au kidini alikuwa nayo. Japo hiyo inaweza kuifanya story yake kuwa ya kipekee zaidi yaani iliwezekanaje mtoto wa mtu aliyekuwa na ushawishi mkubwa kuchagua njia aliyoichagua na pengine ingetupa picha zaidi ya Dully tunaemuona leo kupitia influence ya historia ya mzee wake

Ila sidhani kama Mzee Mohammed kama ana interest hiyo. Angekuwa labda anahusika na TANU ama kupigania harakati za waislamu uongozini. Labda hapo ndio angemchambua zaidi

Lakini huwezi jua, labda story ya Ebe inaweza kuonesha the other side ya Sykes family ambayo mzee Mohammed uitumia kama centre ya historia yake "The Perfect Royal Family".
 
Amesema anamjua mzee wa Dully sykes "Ebe" Lakini hajamzungumzia kwa lolote, labda kwa sababu hana kitu chochote kinachoendana na yale anayoyapigania "Historia ya waislamu Tanganyika".

Mzee wake Dully ukimuangalia tu alikuwa na usasa mwingi hivyo, sidhani hata hiyo consciousness ya kisiasa au kidini alikuwa nayo. Japo hiyo inaweza kuifanya story yake kuwa ya kipekee zaidi yaani iliwezekanaje mtoto wa mtu aliyekuwa na ushawishi mkubwa kuchagua njia aliyoichagua na pengine ingetupa picha zaidi ya Dully tunaemuona leo kupitia influence ya historia ya mzee wake

Ila sidhani kama Mzee Mohammed kama ana interest hiyo. Angekuwa labda anahusika na TANU ama kupigania harakati za waislamu uongozini. Labda hapo ndio angemchambua zaidi

Lakini huwezi jua, labda story ya Ebe inaweza kuonesha the other side ya Sykes family ambayo mzee Mohammed uitumia kama centre ya historia yake "The Perfect Royal Family".
Eyce,
Ebby na mimi ni rika moja na nina mengi naweza kukuekeza kuhusu yeye kwani ni ndugu yangu.

Sote tumekuwa pamoja toka utoto wetu hadi alipofariki.

Lakini unaeleza mambo ambayo jamii watapenda kufahamu huwezi kueleza mambo ya kawaida.

Hakuna atakae kujua yale ya kawaida.

Dully nimemwandika kwa kuwa ni kijana aliyefanya mambo yanayoonekana katika jamii.

Ingua You Tube utamkuta.
Si kila mtu yuko You Tube.
 
Eyce,
Ebby na mimi ni rika moja na nina mengi naweza kukuekeza kuhusu yeye kwani ni ndugu yangu.

Sote tumekuwa pamoja toka utoto wetu hadi alipofariki.

Lakini unaeleza mambo ambayo jamii watapenda kufahamu huwezi kueleza mambo ya kawaida.

Hakuna atakae kujua yale ya kawaida.

Dully nimemwandika kwa kuwa ni kijana aliyefanya mambo yanayoonekana katika jamii.

Ingua You Tube utamkuta.
Si kila mtu yuko You Tube.
Mambo ya kawaida au yasiyo ya kawaida kwa mtazamo upi,

Haya watu wanaokuulizia ili wapate majibu zaidi kwa kuona habari haijakamilika au yale ambayo yapo nje ya interest zako???....

Mfano, Lifestyle yake "Ebe" ukiilinganisha na background yake, inampa kila mtu shauku ya kutaka kumjua zaidi na kwa sababu ni mtu unayemjua zaidi, ni rahisi wewe kumuelezea kuliko kijana wake ambaye umekiri haumjui kwa ile personal level na hata story uliyoitoa inathibitisha hilo

Kumbuka huwezi muongelea Michael Jackson, Janeth Jackson au Jackson 5 bila kumtaja baba yao Joe Jackson

Au whitney Houston bila mama yake Cissy Houston

Itakuwa kwa dully ambaye baba yake alikuwa na interest na muziki directly, honi pengine ukimuongelea itatupa picha halisi ya asili ya kimuziki ya Dully sykes ??..
 
  • Thanks
Reactions: Oxx

Similar Discussions

Back
Top Bottom