TANROADS pale Mbezi mwisho jengeni bypass kama hii

TANROADS pale Mbezi mwisho jengeni bypass kama hii

Uwa najiuliza unashindwaje kujenga daraja wakati wataalam, materials kama cement, nondo nk zipo ndani ya nchi? Nashauri eneo lote la hifadhi ya barabara toka KIMARA-MBEZI TANROADS wawape wawakezaji wajenge Hotels, supermarket, Petro station zenye mvuto nk, ili kuleta muonekano unaendana na miji ya kisasa.
Sawa kabisa ule muonekano wa Mwenge, Makumbusho uhamie kimara kibamba, Uje mpaka makaburi ya Ilala kuja buguruni uende zake Mabibo hapo tutakuwa na jiji poa sana sijui kwanini matajiri hawajengi maeneo niliyotaja wote wanajazana Kinondoni
 
Tanroad huwa hawasikii la kuambiwa
Tanroads tunaomba sana wakati mnajenga barabara ya Kimara - Kibaha hakikisheni mnajenga kwa kiwango cha kimataifa, dar es salaam tunahitaji bypass roads, na sio mtuwekee taa za kuongozea magari.

Jifunzeni kenya , wameawezaje ?

Tunahitaji barabara ambayo mtu akitoka Kibaha, iwe ni none stop hadi bandarini.

Jengeni Highway ya kueleweka, mmebomoa na mna nafasi ya kutosha, hamna sababu ya kujenga vibarabara vya ajabu ajabu.


Bypass ya kwanza ni pale MBEZI MWISHO .
 
Haya njoo twambie viwango vya kusasa ni vipi.. zebra kama uwanja wa netball[emoji28][emoji28]
kwa awamu hii ya tano chini ya JPM sina shaka barabara hiyo ya Kibaha hadi kimara itajengwa kwa viwango vya kisasa,.
haswa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo ndio lango kuu la kuingia katikati ya jiji, huo ndio muonekano wa jiji, barabara hiyo ndio imeshikilia uchumi wa nchi yetu, sidhani kama kutakuwa na ubabaishaji.
Barabara hiyo inapaswa ianze kujengwa haraka!!
 
Back
Top Bottom