Tangu 2012 napambana ila bado bado

Sina Mtaji Tyu Nawaza Nifuge Kuku
Hilo eneo anza hata kupanda mbogamboga uza utapata mtaji! Kaza mtoto wa kiume! Ukipewa hiyo elfu 50 hutokuwa na machungu nayo, utarudi tena kuomba hapa kwasababu unaona ni rahisi!

Piga hata vibarua viwili vitatu huwezi kosa! Kuna mwenzako naye jana kaanzisha uzi ila ukimpa kazi hataki yeye anataka ela..

Kila la kheri..
 
Sina Mtaji Tyu Nawaza Nifuge Kuku
Mi kipindi naenda kufanya kibarua cha ujenzi sikua na mtaji kaka, mule hauombwi mtaji, ni wewe na ujuzi wako au nguvu, teknolojia imerahissha siku hizi ujenzi kazi sio ngumu mashine ndio zina koroga zege we hubebi zege kichwani unatumiwa kitoroli nk hamna kazi ngumu kule labda uwe mvivu tu
 
Hongera huo mziki hakikisha na kuucheza unajua.
 
Kwa heshima, kwa kuanzia nahitaji TSh 50,000 tu. Ni kiasi nitakachotumia kuanzisha ufugaji wa kuku na kuanza kujenga hatua kwa hatua. Kama utaweza kunisaidia kwa kiasi hicho au sehemu yake, nitashukuru sana. Mungu awabariki. 🤲🏽
Mkuu hebu kua serious Toka hapo kwenye comfort zone hivi elfu 50k ni Hela ya kushindwa kupata kweli kwa kijana wa miaka 30

Eneo ulilopo hamna hata vibarua vya 5k kwa siku tukifanya siku kumi ushajipatia mtaji

Nikajua unahitaji kiasi flan reasonable Sasa 50k real??
 
Kila kitu unacho, rudisha mindset yako maana naona ndio changamoto kubwa uliyonayo.
 
Kila la heri mkuu
 
Nikajua unataka kuokoa jahazi wengine tumemshauri ujinga😁
 
Hahah mkuu niliona dogo kakomaa kuomba mtaji nikasema ngoja nimtengenezee mazingira wadau wam_push

Anaishia kusema 50k. Bado hajachapika vizuri
Mkuu nimekupata. Hii 50K kwangu ni mwanzo wa kujitengenezea, si ombi la starehe. Kwa heshima na unyenyekevu, kama kuna nafasi ya kunisukuma hata kwa kiasi chochote, nitashukuru sana. Nikipata mwanzo huu, niko tayari kupambana kwa juhudi zangu. Mungu akubariki sana. 🤲🏽
 
Embu tuwe wapole. Kila mtu anapitia mapambano yake ambayo huenda hatuyaoni. Tusihukumu haraka wala kudharau juhudi za mwingine. Tujengeane moyo, tushauriane kwa heshima na pale tunapoweza, tusaidiane. 🤝

Mwisho wa kutafakari: Maisha hubadilika kwa wakati usiotarajiwa. Leo unaweza kuwa na nguvu, kesho ukahitaji msaada wa yule uliyemdharau. Tuwe wema, tuwe na huruma, na tuache alama nzuri katika maisha ya wengine. Maana mwisho wa yote, tunachobaki nacho si ukubwa wa tulichokuwa nacho, bali namna tulivyowatendea wengine. ❤️
 
Angalia Fundi ujenzi wa Mataani Kwako Apo, Ongea nae awe anakuchukua Kwenda kibaruani hawana Noma.

Au Tembelea site Za Ujenzi Ajira Zipo Kibao Sema Mchawi HASIRA na nguvu mbona Utatoboa mzee
Ushauri wako nimeupokea mkuu, na ni wa maana sana. 🙏 Sitaki kuchagua kazi; niko tayari kuanza popote penye nafasi na kujifunza. Changamoto kubwa ni kupata mtu wa kunipa nafasi ya kuanzia. Lakini nitaanza kufuatilia mafundi na site za ujenzi huku nikiendelea na mipango yangu. Mungu akijalia, nitapambana mpaka nitoboe. 💪
 
ngoja nile kusapoti upambanaji wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…