Ajira kwa Wahitimu Elimu ya Juu
Mwaka 2014
Katika mwaka wa fedha 2014/2015 Jeshi la Polisi
Tanzania linatarajia kuajiri wahitimu wa vyuo vya
Elimu ya Juu wa mwaka 2013/2014. Ili kutekeleza
azma hii waombaji watajaza kikamilifu na
wataambatanisha vivuli vya vyeti vyao na kutuma
Makao Makuu ya Polisi kwa njia ya Posta kabla ya
tarehe 31.08.2014 kwa anuani ifuatayo:
Inspekta Jenerali wa Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
S. L. P. 9141,
DAR ES SALAAM
Waombaji wawe na taaluma zifuatazo:
Shahada: Menejimenti ya Rasilimali Watu, Utawala
katika Utumishi wa Umma, Uchumi, Saikolojia na
Ushauri Nasihi, Usimamizi wa Sheria na Utekelezaji
[BaLE], Sheria, Ualimu, Maendeleo ya Jamii,
Uandishi wa Habari, Uandishi wa Habari za
Michezo, Mawasiliano ya Umma, TV & Redio
Production, Michezo, Ugavi[BA in Procurement &
Supplies], Mawasiliano ya Redio[Bsc in Radio
Communication], Mazingira[BA in Environmental
Disaster Mgt], Uhandisi Mitambo, Uhandisi Madini
[Mining Engineering], Uchoraji[BA in Fine Arts],
Fedha na Benki[Finance & Banking], Daktari[Medical
Doctor] na Daktari wa Meno[Dental Surgeon],
Mkemia, Bailojia[Molecular Biology].
Stashahada: Utunzaji Kumbukumbu, Katibu
Muhutasi[Personal Secretaries], Mawasiliano ya
Redio, Matengenezo ya Kompyuta, Fax na
Photocopy Machines, Mafundi Mitambo wa Meli,
Mafundi Umeme wa Magari, Ugavi[Procurement &
Supplies], TV na Video Production, Manahodha,
Tabibu[Clinical Officer], Tabibu wa Meno[Dental
Therapist], Mzoeza Viungo[Psysiotherapist/
Occupational Therapist], Fundi Sanifu Mionzi
[Radiographer] na Fundi Sanifu Macho[Optometrist].
Astashahada: Uzamiaji, Mpishi, Fundi Pikipiki,
Fundi Ushonaji na Muuguzi Msaidizi[Enrolled
Nurse].
MASHARTI KWA MWOMBAJI
1. Mwombaji atajaza fomu ya maombi kikamilifu na
atabandika
picha yake Ppt Size kwenye fomu.
2. Mwombaji aambatanishe katika fomu vivuli vya
vyeti vyote
yaani cheti cha kuzaliwa, kuhitimu elimu ya
sekondari[Leaving
& Academic], cheti/vyeti vya taaluma[Academic
Transcript].
3. Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
SIFA ZA MWOMBAJI
1. Awe Mtanzania kwa kuzaliwa.
2. Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi
miaka 25.
3. Awe amehitimu chuo mwaka wa masomo
2013/2014 tu.
4. Awe na tabia njema.
5. Asiwe na kumbukumbu za kutenda uhalifu.
6. Awe na afya njema[kimwili na kiakili]
7. Awe hajaoa/hajaolewa au kuwa na mtoto.
8. Asiwe na alama za kuchora mwilini[tatuu].
9. Awe na urefu usiopungua sentimita 155.
10. Asiwe mtumiaji wa madawa ya kulevya.
11. Awe hajaajiriwa na idara nyingine Serikalini.
12. Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya awali ya
Polisi.
13. Awe tayari kufanya kazi popote ndani na nje ya
Tanzania.
Pakua Fomu:- Fomu ya Ajira Elimu ya Juu
2013/2014