Jamani hapo labda niweke wazi kidogo kuhusu ishu ya umri katika jeshi la polisi..1.vijana wanaotakiwa ni kuanzia miaka 18-25 kama tangazo linavyoonesha kwa kuwa kwa umri wa level iyo bado hawajachangamana sana na mtaani katika kuadapt new behaviours..kwaiyo ndio mana sasa hivi jeshi la polisi limebadilisha mfumo wa kuajiri kwa kufuata watu katika education institutions ili kuweza kuwa na historia nzuri ya waajiriwa wote.2.mtu anapoajiriwa na umri wa level iyo ni kuwa anakuwa hazina ya jeshi kwa muda mrefu mpaka umri wa kustaafu pasipo kuja kukaa muda mfupi kazini.lakini pia mtu wa umri huu bado anafundishika mambo mbalimbali na pia anaweza kusoma fani nyingine ndani ya ajira na kuweza kuwa na muda mrefu wa kulitumikia jeshi ndani ya fani nyingine..Napenda kutoa rai yangu kuwa wale wanaodhani jeshi la polisi sio zuri sio kweli waangie kikubwa ukumbuke kujiendeleza kielimu,nidhamu,na kuzingatia maadili mema ya kazi.kuhusu maslahi sitaki sana maswali mana kazi ya jeshi kwanza inaanzia moyoni na maana kuwa na moyo wa kutumika katika national service..nawatakia kila la heri wale wote watakaochaguliwa kujiunga na jeshi la polisi.kumbuka kuna vitengo vingi sio lazima uende lindo tena kwa wale wenye fani zao mambo sio mabaya.acha kusikiliza maoni na maneno ya mtaani.utafute ukweli.