Tangazo hili la "Hakielimu" sidhani kama litadumu

Tangazo hili la "Hakielimu" sidhani kama litadumu

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,646
Reaction score
164,798
Kuna tangazo,binafsi nimeliona leo ITV, linaonyesha tatizo kubwa la vyoo katika shule zetu za msingi.

Tangazo hilo linasikitisha ukiliangalia. Tangazo linaonyesha jengo bovu na chakavu sana la choo huku wanafunzi wakipanga foleni ndefu na hapo hapo wakigombania kuingia chooni na kibaya zaidi mwalimu wa kike anaonekana awali akitoka katika choo hicho kabla ya wanafunzi kuingia kitu kinachomanisha kuwa walimu wanachangia choo hicho na wanafunzi wao.

Kwa waliona tangazo hilo bila shaka watakubaliana na mimi na huenda wakawa na mengi ya kuongeza kuhusu tangazo hilo.Mimi ndio leo nimeliona kwa mara ya kwanza sijui nyinyi wenzangu maana huenda lina muda.

Kwa ujumbe unaobebwa katika tangazo hilo,sidhani kama litavumiliwa.

Tusubiri muda utaongea.
 
tangazo lina wik nzima mkuu sema we umeliona ITV Ni Mara Yao Ya Kwanza Kuonyesha
 
Mi nimeliona limebeba ujumbe yenye uhalisia kwenye shule nyingi hasa zilizopo vijijini sasa ni wajibu wetu na serikali kuchukua hatua na sio kuliondoa tangazo
 
Huo ndio ukweli serekali inatakiwa iboreshe mazingira ya shule.
 
Mwenyewe sijaliona ila kwa ulivyoelezea tu haitavumiliwa hata kidogo, wangevumilia kidogo ingekuwa labda mwaka 2014, 13,12, 11 au hata 2016, 17 lakini siyo 2015
 
Mwenyewe sijaliona ila kwa ulivyoelezea tu haitavumiliwa hata kidogo, wangevumilia kidogo ingekuwa labda mwaka 2014, 13,12, 11 au hata 2016, 17 lakini siyo 2015
Hiyo ndio hofu yangu hata mimi.
 
Kiukweli vyoo vya shule ni sheeda,, HV Jana nilikuwa na mwalimu furani kutoka shule ya msingi kaja kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa kitongoji kuwa wanafunga shule kwa lazima kutokana na uhaba wa vyoo,, kwani shule yaweza kupata magonjwa ya mlipuko any time,,,,,,
 
Kuna tangazo,binafsi nimeliona leo ITV, linaonyesha tatizo kubwa la vyoo katika shule zetu za msingi.

Tangazo hilo linasikitisha ukiliangalia. Tangazo linaonyesha jengo bovu na chakavu sana la choo huku wanafunzi wakipanga foleni ndefu na hapo hapo wakigombania kuingia chooni na kibaya zaidi mwalimu wa kike anaonekana awali akitoka katika choo hicho kabla ya wanafunzi kuingia kitu kinachomanisha kuwa walimu wanachangia choo hicho na wanafunzi wao.

Kwa waliona tangazo hilo bila shaka watakubaliana na mimi na huenda wakawa na mengi ya kuongeza kuhusu tangazo hilo.Mimi ndio leo nimeliona kwa mara ya kwanza sijui nyinyi wenzangu maana huenda lina muda.

Kwa ujumbe unaobebwa katika tangazo hilo,sidhani kama litavumiliwa.

Tusubiri muda utaongea.
Hata Mimi nimeliona kwa mara ya kwanza Leo na tulijaribu kuongelea na famila hapa kuwa watalitoa maana limegusa uhalisia na siku zote hawapendi uhalisia hawa CCM
UNADHANI hawa Haki ya elimu kwenye uongozi wa Mkapa waliwahi kufungiwa.
 
Mmh hata mimi ndio nimeliona kupitia ITV leo. Sidhani kama serikali wataweza kuvumilia ukizingatia hata sheria ya uhalifu mitandaoni ilivyosainiwa chap chap, unaweza ukajua kabisa lengo ni kuwaziba watu midomo.

Yote kwa yote, tangazo limebeba ujumbe sahihi, kwa mfano
1/Linaonyesha kuna mwamko wa watu kupenda kutumia vyoo na sio kwenda kujisaidia vichakani.

2/Vyoo vingi vya taasisi za umma na serikali hususani mashuleni ni vibovu, vichafu na vichache.

3/Uko ustaarafu wa kuwa na vyoo vya wanaume na wanawake katika shule lakini hakuna choo cha walimu(staff)

4/Kuna tatizo la kuwa na vyoo vya kutosha na vyenye ubora katika shule zetu.

5/Utu wa mtu unaweza ukapotea kwa kukosa mazingira bora ya kujisaidia na kujisitiri.
 
shule+zetu.jpg


Pit%20Latrines%20Image%20%28thewaterproject.org%29_1.jpg


shule.jpg


Hivi ni moja ya vyoo vingi ambavyo vinatumika katika shule zetu za Msingi na Sekondari hapa Tanzania.​
 
Kwa kweli hili tangazo la HAKI ELIMU nimeliona leo kwa mara ya tatu na nafikiri kuwa linaonyesha kuwa kuna uhaba wa vyoo bora mashuleni. Hata hivyo kwa maoni yangu nafikiri chumvi imeongezwa sana na hii itasababisha lisitishwe muda si mrefu, isipokuwa kama serikali ilishirikishwa katika kuliandaa.
 
Huo ndio ukweli serekali inatakiwa iboreshe mazingira ya shule.

Nadhani pia jamii ya watanzania haina budi kubadili fikra katika mambo kama haya, sidhani kama ni vema majukumu yote tukaitupia serikali ni wakati sasa uwajibikaji uhimizwe kw jamii nzima katika upana wake.

Mambo kama haya ya kujenga na kuboresha huduma kama za vyoo yanawezwa kabisa kufanywa na alumni, mashirika kupitia CSR na mobilization ya makundi mengine katika jamii.

Kama individually tunaweza kufanya mobilization ya michango ya harusi, mazishi, kukodi mabasi ili kusafiri na timu na hata kuandaa bonanza kwa nini kwa moyo na ari hiyohiyo tusifikie mahala pa kuona kuwa huduma za msingi za jamii zilizo bora ni wajibu unaopaswa kuanzia kwa wanajamii husika? Tafakari na chukua hatua.
 
Kwa kweli hili tangazo la HAKI ELIMU nimeliona leo kwa mara ya tatu na nafikiri kuwa linaonyesha kuwa kuna uhaba wa vyoo bora mashuleni. Hata hivyo kwa maoni yangu nafikiri chumvi imeongezwa sana na hii itasababisha lisitishwe muda si mrefu, isipokuwa kama serikali ilishirikishwa katika kuliandaa.

Una uhakika chumvi imeongezwa?
 
Nadhani pia jamii ya watanzania haina budi kubadili fikra katika mambo kama haya, sidhani kama ni vema majukumu yote tukaitupia serikali ni wakati sasa uwajibikaji uhimizwe kw jamii nzima katika upana wake.

Mambo kama haya ya kujenga na kuboresha huduma kama za vyoo yanawezwa kabisa kufanywa na alumni, mashirika kupitia CSR na mobilization ya makundi mengine katika jamii.

Kama individually tunaweza kufanya mobilization ya michango ya harusi, mazishi, kukodi mabasi ili kusafiri na timu na hata kuandaa bonanza kwa nini kwa moyo na ari hiyohiyo tusifikie mahala pa kuona kuwa huduma za msingi za jamii zilizo bora ni wajibu unaopaswa kuanzia kwa wanajamii husika? Tafakari na chukua hatua.

Mkuu nimekuelewa kabisa! Ila ndugu yangu nani awajibike kwa hili? Hao wezi wa mabiliono wanafanya nini? Hakuna cha kuwajibika mpaka majizi yamerudisha hele za walala hoi.
 
Hilo Tangazo nimeliona, kiukweli linatia hasira, hasa ukioanisha na ufisadi unaondelea Nchini.
 
Back
Top Bottom