Tanganyika imerudi

Tanganyika imerudi

kp24032014.jpg
 
Tanganyika irudi,muungano uvunjike,ccm ife.over

Sasa Tanganyika ni koloni la Zanzibar ili Ipate Uhuru lazima Mkoloni Zanzibar ajitenge Muungano Ufariki . Pia Hili jina Tanzania ni jina Mali ya Tanganyika kwali Nyerere Ndie alikwenda nalo kwenye kuasisi Muungano,hivyo muungano Ukifariki Tanganyika inaweza kuitwa Tanzania tu ili pale UN wasihangaike kubadili jina . Wale wakoloni watabaki na jina Zanzibar sisi Bara pataitwa Tanzania a.k.a Tanganyika hilo jina Tanzania ni Mali halali ya Tanganyika .
 
Ndiyo irudi haraka sana. Hiyo bendera ya nchi yetu itengenezwe kwa wingi tuanze kuipeperusha kama wenzetu zanzibar wanavyopeperusha bendera yao
 
Muungano upo Mahututi unapumulia Mashine Miaka 47 Zanzibar hawajahudumia Muungano kwa Miaka 47, huku Tanganyika ikiwaogopa kuwakumbusha eti ikiwauliza wangevunja Muungano. ! Huku kujipendekeza kwa Tanganyika juu ya huduma za Zanzibar Ndio kumepelekea Zanzibar kuonekana ni Mkoloni . Maana anawanyonya Watanganyika Live , kisha anavurumusha Vuvuzela ili kuwapumbaza wasijitambue wananyonywa.
 
Tutauhitaji tu muungano hasa watakapopata mafuta na sisi wakati huo tuwe tumeachiwa mashimo tu kwenye migodi halafu mbaya zaidi tuwe tumeuza kila kitu. Oops labda tuje kuanza kubinafsisha taasisi!
 
.Wanabodi!!!


  1. Unawachukua wabunge 80 toka Visiwani (kwa miaka50!) wanakaa Dodoma wanajadili Barabara za Geita na Katavi. Unawalipa msharahakila mwezi na posho kwa kodi toka Tanganyika!
  2. Unammchukua Makamu wa Raisi, Mawaziri, Mabalozi na 20% ya wafanyakzi wa Wizara za Muungano toka visiwani.. kisha unawalipa mishahara na posho (kwa miaka 50!) kwa kodi za Watanganyika!
  3. Tunajuinga na Afrika Mashariki. Bara wanalipia pesa ya kodi gharama za Afrika Mashariki.. Wabunge ni 9 kama walivyo wabunge toka Rwanda (9), Kenya (9). Then!!!!! Tanyanyika inatoa Wabunge (6) Na Visiwan iwabunge (3). Then Bara kwa kodi zao unawalipia wabunge wa Visiwani katika Bungela Afrika Mashariki!!!
  4. Unawateua wabunge toka Visiwani kamati za Bunge Muungano kukagua barabara kule Ngara na Tandahimba unawalipa pesa ya kodi ya Tanganyika kwa miaka 50!
  5. Halafu unakaa unajivuna Muungano huu ni waKuigwa Bara la Afrika na Dunia yote na unajipiga2 kifua kuwa na fikra sahii za waasisi wa Taifa hili!
  6. Miaka 50! Wewe unakuwa rafiki au mshirika wangu!Siku zote tukionana mimi nakununulia tu soda au bia wewe.. wewe hata siku mojahaununui… na unaona ni poa tu! Kwa mika 50!
  7. Halafu watoto wetu wa shule kule Handeni naKondoa wanakaa Chini hawana madawati na tunalalamika na kuona ni sawa!

SAA INGINE NAONA KAMA TANGANYIKA AU TANZANIA BARA TUMEROGWA AND WE ACTUALLY DO NOT KNOW OUR PRIORITIES!
WATOTO NA WAJUKUU ZETU WATAULIZA SIKU MOJA NA HATUTAKUWA NAMAJIBU!

WATANGAYIKA TUAMKE TUACHE UNAFIKI HUU!
 
Back
Top Bottom