Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 575
- 2,559
Picha za Ajali
Ndugu waandishi wa Habari na Ndugu wananchi wa Mkoa Wa Tanga na Tanzania kwa ujumla Nimepokea kwa masikitiko makubwa tukio la Ajali Mbaya iliyotokea usiku wa leo. Ajali hiyo imehusisha Magari mawili na kusababisha Vifo vya watu 17 na Majeruhi 12 Pamoja na Uharibifu mkubwa wa Magari hayo..
Ajali ilitokea Tarehe 03/02/2023 Majira ya Saa 4.30 Usiku Eneo la Magila Gereza Kata ya Magila Gereza Tarafa ya Mombo Wilayani Korogwe, Barabara Kuu ya Segera - Buiko.
Magari yaliyohusika na Ajali hiyo ni Gari Na T.673 CUC aina Mitsubish Fuso Ikiendeshwa na Dereva ambaye Jina Lake Halijafamika iligonga na Gari T.863 DXN aina ya Coaster Coaster Iliyokuwa imebeba Mwili wa Marehemu n Abiria 26 iliyokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa mazishi.
Ajali hii inasababisha Vifo 17 na Majeruhi 12. Ambao Majina yao wote Hayajafahamika. Miili ya Marehemu imehifadhiwa katika Hospitali yetu ya Wilaya Ya Korogwe na Majeruhi 10 Wamehamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo na Majeruhi 2 wamebaki Hospital ya Korogwe Kwa Matibabu.
Chanzo cha Ajali ni Mwendo Kasi na Uzembe wa Dereva wa Gari Na :T.673 CUC M/Fuso Kulipita gari la mbele Bila Ya kuchukua Tahadhari na kugongana Uso kwa uso Gari Na :T.863 DXN T/Coaster
Tukio la Ajali Baada ya kukaguliwa , Magali yote yameshaondolewa barabarani na Sasa Barabara inapitika.
Mgumba T. Omary
Mkuu wa Mkoa Wa Tanga.