Kuna Mwalafyale alileta mchele wa biashara, katika kutafuta wateja na soko akutana na mambo hayo hapo juu, licha ya hivyo akitoka kwenye mihangaiko anakuta mahanjumati kwenye sahani vimefunikwa kwa kawa. Baba wa watu ameuza umchele akaanza kumega faida, mwisho mtaji, mwisho pesa imekwisha akatafuta kibarua. Imepita miaka mitatu nduguzake wanakuja kumtafuta, wanamkuta na balghashia anatoka na tasbii.