MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,978
Katika kupambana na kile kinachoonekana kwa uongozi wa juu wa TANESCO kuwa ni taswira hasi(negative image), Uongozi wa TANESCO umewalipa pesa wanaoitwa “washawishi wa kwenye mitandao ya kijamii(social networks influencer)” ili waisaidie katika kubadilisha taswira na kuwa taswira chanya kwenye jamii.
Kwa sasa ukiingia kwenye mitandao ya kijamii kama twitter, facebook na clubhouse utakuta jumbe mbalimbali za kuisifia TANESCO katika utendaji kazi kutoka kwa washawishi “wakubwa” katika mitandao nchini.
Kwa sasa, wale wale ambao walikuwa wanalalamika sana kuhusu huduma mbovu za TANESCO na “kumzodoa” Waziri wa Nishati, January Makamba kwa sasa wanaimba tena “mapambio” ya kuipongeza TANESCO na Waziri Makamba.
Kuna msemo usemao, “Penye udhia penyeza rupia". January Makamba amepenyeza rupia ili kuondoa udhia!
Inashangaza kuona TANESCO wanatumia pesa nyingi za serikali/wananchi kuwalipa washawishi wa kwenye mitandao ili wawasafishe kwa propaganda wakati wananchi wengi wanachohitaji ni umeme wa uhakika na pia kuunganishiwa umeme kwa haraka.
Waziri wa Nishati, January Makamba na bodi yake ya TANESCO wanadhani propaganda zitaondoa tatizo la msingi la TANESCO.
Baada ya kuteuliwa na kuapishwa, Waziri Makamba alitoa matamko mbali mbali kuhusu tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara lakini imeanza kugundulika kuwa baadhi ya matamko hayo hayakuwa na ukweli.
Baadhi ya wabunge ambao wanaunda kamati ya kudumu ya bunge ya Nishati na Madini wameanza kuhoji kuhusu kauli zake huku kamati ikimtaka awasilishe bungeni maintanence schudule kuonyesha jinsi ambavyo mitambo haikufanyiwa service kwa miaka 5 mfululizo kama alivyodai.
Kwa yanayoendelea kwa sasa, kuna uwezekano mkubwa kwa TANESCO kupenyeza pia rupia kwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini kama ilivyofanya kwa “washawishi wa kwenye mitandao ya kijamii(social networks influencer)” ili iwanyamazishe!
Kwa sasa ukiingia kwenye mitandao ya kijamii kama twitter, facebook na clubhouse utakuta jumbe mbalimbali za kuisifia TANESCO katika utendaji kazi kutoka kwa washawishi “wakubwa” katika mitandao nchini.
Kwa sasa, wale wale ambao walikuwa wanalalamika sana kuhusu huduma mbovu za TANESCO na “kumzodoa” Waziri wa Nishati, January Makamba kwa sasa wanaimba tena “mapambio” ya kuipongeza TANESCO na Waziri Makamba.
Kuna msemo usemao, “Penye udhia penyeza rupia". January Makamba amepenyeza rupia ili kuondoa udhia!
Inashangaza kuona TANESCO wanatumia pesa nyingi za serikali/wananchi kuwalipa washawishi wa kwenye mitandao ili wawasafishe kwa propaganda wakati wananchi wengi wanachohitaji ni umeme wa uhakika na pia kuunganishiwa umeme kwa haraka.
Waziri wa Nishati, January Makamba na bodi yake ya TANESCO wanadhani propaganda zitaondoa tatizo la msingi la TANESCO.
Baada ya kuteuliwa na kuapishwa, Waziri Makamba alitoa matamko mbali mbali kuhusu tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara lakini imeanza kugundulika kuwa baadhi ya matamko hayo hayakuwa na ukweli.
Baadhi ya wabunge ambao wanaunda kamati ya kudumu ya bunge ya Nishati na Madini wameanza kuhoji kuhusu kauli zake huku kamati ikimtaka awasilishe bungeni maintanence schudule kuonyesha jinsi ambavyo mitambo haikufanyiwa service kwa miaka 5 mfululizo kama alivyodai.
Kwa yanayoendelea kwa sasa, kuna uwezekano mkubwa kwa TANESCO kupenyeza pia rupia kwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini kama ilivyofanya kwa “washawishi wa kwenye mitandao ya kijamii(social networks influencer)” ili iwanyamazishe!