Hao jamaa wa TANESCO ni wapuuzi sana tena sana.Tanesco pumbavu sana, lakini yote yana mwisho na mwisho wenu hauna masaa.
Pole mkuu, ila wana kera saaana. Walitakiwa watoe taarifa mapema na sio kushitukiza kama walivyo fanya
unauliza hasara ya nini.... Unakuwa kama mbwiga na wewe... Hasara yao inakuhusu nini... Tunataka umeme hatutaki longolongo..ahsante tanesco kwa taarifa. Je shirika limepata hasara ya kiasi gani hadi sasa? Je wateja walioathirika kwa kukosa umeme mtawafidia??
Wanatengeneza mianya ya kulipana over time, hawana lolote.
Mkuu nadhani kuna kitu watanzania tunatakiwa kukifanya kwa ajili ya kuinusuru nchi yetu, inawezekana vipi mtu una pesa zako mkononi halafu unalazimishwa kukaa gizani, vitu ndani ya friji vinaoza kisa eti mtandao unasumbua.Hao jamaa wa TANESCO ni wapuuzi sana tena sana.
Nimemshuhudia Mkurugenzi wao mkuu, Engineer Mramba, kwenye taarifa ya habari ya ITV ya saa 2 usiku, akituassure waTz kuwa tatizo limekuwa solved.
Akatuhakikishia kuwa kila kitu kitarudi katika hali ya kawaida usiku huu, kumuhakikishia Mkurugenzi huyo wa TANESCO kuwa aliongea uongo wa kupitiliza ni kwamba, usiku wote huu ninapopost hii mada, ninaendelea kukaa gizani, kwa kuwa nimejaribu mara kadhaa kununua umeme huo kwa M-Pesa na Tigo Pesa, lakini nara zote zinazozidi mara 10, nimekuwa nikirejeshewa meseji ya kuwa muamala wangu wa pesa umerejeshwa, kutokana na matatizo ya kiufundi kwenye mfumo wa LUKU.
Kwa kulidanganya waziwazi Taifa zima, kupitia kwenye chombo cha habari hicho kinachoangaliwa na watu wengi sana, na kwa TANESCO kuendelea.kutupa usumbufu mkubwa, nadhani ingekuwa vyema Mkurugenzi huyo wa TANESCO aamue tu kuwajibika kwa kuachia ngazi.
Nimezuia tusi kubwa sana kunitoka, inatia hasira mno mkuu.Hawa jamaa ni washenzi sana taarifa hawakutoa alafu wanajidai kuomba samahani, pumbavu sana hawa
Kupeana ajira kwa vimemo na kujuana ndiko kunapelekea majanga kama haya. Ni mtaaalamu gani huyo aliyesomea kazi yake na kuhitimu kwa mafanikio anashindwa kurekebisha kasoro ya kimfumo siku zote hizi na yupo analipwa mshahara kwa kusinzia tu kwenye kiti!!!Hivi kumbe hapa Tanzania hatuna wataalamu,umefika wakati TANESCO ianzishe utaratibu wa kuwatrain watu.
Hivi yule mdada sijui meneja mahusiano yupo?
Hata leo umeme umekatika tanesco ...
hata jina lake moja ? ungeliweka hapa.
Hata leo umeme umekatika tanesco kwa hiyo wateja wameshimdwa kuhudumiwa! Sasa inakuaje shirika.kubwa kama.hili kukosa umeme?hta jenereta hamna?ni shida tanesco