TANESCO watoa ufafanuzi matatizo ya LUKU!

Kibo10

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,277
8,840
MWENDELEZO WA TAARIFA KUHUSU KUKOSEKANA KWA MTANDAO WA LUKU

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa mwendelezo wa taarifa ya tatizo la kukosekana kwa huduma ya kununua umeme wa LUKU kwa njia ya Mtandao lililoanza usiku wa kuamkia Februari 28, 2015.

Kama tulivyoeleza awali, Tatizo kubwa lilikuwa ni hitilafu ya kiufundi iliyotokea kwenye mfumo wa kununua umeme wa LUKU.

Baada ya kugundua tatizo, mafundi wa Tanesco na Kampuni ya Itron kutoka Afrika Kusini ambao ndio watengenezaji wa mfumo huo, wamefanikiwa kurejesha huduma ya kununua umeme wa LUKU kwa njia ya Benki.

Benki za CRDB na NMB kwa kutumia simbanking na ATM kwa sasa wanaweza kuuza umeme. Pia Maxmalipo nao wameanza kuuza kwa baadhi ya vituo.Mitandao ya simu (M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money) bado hawajaanza kuuza.

Jana tuliwashauri wateja wetu kwenda kununua umeme kwa Mawakala wetu na baadhi walifanya hivyo lakini baadae tuligundua kuwa units (tokens) walizokuwa wametumiwa zilikuwa haziingii kwenye mita zao, hivyo tukasimamisha kununua kwa kutumia mawakala mpaka tutakapo rekebisha tatizo.

Tunawaomba Wateja wote ambao wana tokens ambazo hazikuingia kwenye mita zao wawe na subira kwani tutoa maelekezo baada tu ya mfumo kurudi kwenye hali ya kawaida.

Aidha tunawapa matumaini wateja wetu kuwa tatizo tutalipatia ufumbuzi muda si mrefu na wale wote ambao walishatuma pesa zao kwa njia ya simu na hawajapa tokens, mfumo ukitengamaa watatumiwa tokens zao.

Hakuna pesa ya mteja itakayopotea. Uongozi wa Shirika unaendelea kuomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makuu.
 
MWENDELEZO WA TAARIFA KUHUSU KUKOSEKANA KWA MTANDAO WA LUKU

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa mwendelezo wa taarifa ya tatizo la kukosekana kwa huduma ya kununua umeme wa LUKU kwa njia ya Mtandao lililoanza usiku wa kuamkia Februari 28, 2015.

Kama tulivyoeleza awali, Tatizo kubwa lilikuwa ni hitilafu ya kiufundi iliyotokea kwenye mfumo wa kununua umeme wa LUKU.

Baada ya kugundua tatizo, mafundi wa Tanesco na Kampuni ya Itron kutoka Afrika Kusini ambao ndio watengenezaji wa mfumo huo, wamefanikiwa kurejesha huduma ya kununua umeme wa LUKU kwa njia ya Benki.

Benki za CRDB na NMB kwa kutumia simbanking na ATM kwa sasa wanaweza kuuza umeme. Pia Maxmalipo nao wameanza kuuza kwa baadhi ya vituo.Mitandao ya simu (M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money) bado hawajaanza kuuza.

Jana tuliwashauri wateja wetu kwenda kununua umeme kwa Mawakala wetu na baadhi walifanya hivyo lakini baadae tuligundua kuwa units (tokens) walizokuwa wametumiwa zilikuwa haziingii kwenye mita zao, hivyo tukasimamisha kununua kwa kutumia mawakala mpaka tutakapo rekebisha tatizo.

Tunawaomba Wateja wote ambao wana tokens ambazo hazikuingia kwenye mita zao wawe na subira kwani tutoa maelekezo baada tu ya mfumo kurudi kwenye hali ya kawaida.

Aidha tunawapa matumaini wateja wetu kuwa tatizo tutalipatia ufumbuzi muda si mrefu na wale wote ambao walishatuma pesa zao kwa njia ya simu na hawajapa tokens, mfumo ukitengamaa watatumiwa tokens zao.

Hakuna pesa ya mteja itakayopotea. Uongozi wa Shirika unaendelea kunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.

TUMESHAJUA NJAMA ZENU MMEWARAHISISHIA MAFISADI WENYE VIAAKAUNT CRDB NA NMB afu mmetuacha makabwela tuendelee kumbwelambwela... ku........nina zenyu... wangese sana nyie tanescrooooo
 
TUMESHAJUA NJAMA ZENU MMEWARAHISISHIA MAFISADI WENYE VIAAKAUNT CRDB NA NMB afu mmetuacha makabwela tuendelee kumbwelambwela... ku........nina zenyu... wangese sana nyie tanescrooooo

Pole mkuu, ila wana kera saaana. Walitakiwa watoe taarifa mapema na sio kushitukiza kama walivyo fanya
 
Mbona mimi jana asubuhi kabla ya saa tatu asubuhi niliwezanunua umeme kwa Airtel Money ama hii memo ni ya tarehe ngapi wajameni
 
Ahsante tanesco kwa taarifa. Je shirika limepata hasara ya kiasi gani hadi sasa? Je wateja walioathirika kwa kukosa umeme mtawafidia??
 
Lawama hazisaidii lakini ingewagharimu kiasi gani kuutahadharisha umma/kutoa taarifa mapema ili wateja waepuke usumbufu na hasara tuliopata? Wateja ndo wanafanya shirika li-sustain. Mjifunze kutoa taarifa mapema au kwa wakati.tanesco badilikeni ki-utendaji.
 
Daaaaaaaaaaaa! Jana tuu nimetoka kununua mazagazaga nikayahifadhi kwenye frigi. Leo nimeenda tanesco mtandao hausomi crd sim banking inagoma, mpesa inagoma, tigo pesa inagoma. Nasikitika sana kwavili ka 200,000 kangu ambako ni sehemu ya 400,000 ya kamshahara kangu ka mwezi imeshapotea. Maskini Mungu nisaidie.
 
Dah aise siku ya pili tena hii nalala giza...nilizoea kurudi home saa 11 jioni ila kuanzia jana nashinda bar kurudi saa 4 naoga nalala...manake hm hamna flavor kabisa bila umeme
 
Nimepanga folen kuanzia saa 12 jion nakuja kupata umeme saa 5 usiku...pambf zenu tangiza @/<>¡ì:#0„6@
 
Back
Top Bottom