fikirini
Senior Member
- May 24, 2011
- 114
- 22
Wana Jf asalamaleykum. Hawa TANESCO kila siku mabadiliko tu yasiyo na tija bali ni ya umahiri wa kubooresha makali ya umeme, hakuna kipya....hata kinyonga japo hubadilika rangi ila ni kwa malengo na tija pia ni kwa manufaa ya maisha yake hasa pale hatari inapokuwa mbele yake. Kwa TANESCO Hakuna ubunifu, kweli hiki ni kichefuchefu. Hii inatokana na habari za kusikitisha kuwa shirika hilo limetangaza mgawo mkubwa wa umeme usio na kikomo, utakaokuwa kwa saa 10, siku saba kwa wiki nzima.Maafisa wa shirika hilo na Wizara ya Nishati na Madini wamesema mgawo huo umetokana na upungufu wa maji katika bwawa la Mtera na transfoma zake kuzalisha umeme mdogo kuliko mahitaji.Kwa mujibu wa tangazo la ratiba ya mgao huo lililotolewa na Tanesco jana, mgao huo utakuwa wa kati ya saa sita hadi 10 kwa siku ambapo maeneo yatabadilishana muda wa mgao. Hata hivyo, tangazo hilo la Tanesco limekuja wakati maeneo mengi nchini yakiwa na mgawo wa muda mrefu wakinyemela na ambao unachukua muda wa saa zaidi ya zilizotangazwa jana na shirika hilo hali inayosababisha malalamiko kwa wananchi na kupoteza imani na serikali iliyopo madarakani.
Sasa hii serikali na shirika lake, wanaona fahari gani kila siku kuwa wataalam tu wa kutoa ratiba za mgao, hivi utoaji wa huduma za umeme hatuwezi tukafanya kama makampuni ya simu.? Turuhusu ushindani katika sekta hii wadau.....alafu ndo tunaambiwa tudumishe amani. Ni amani gani hii ya kuumizana? Kutojaliana? Huu ni unafiki wa viongozi wetu....nini hatima ya kilio hiki wana JF?
Sasa hii serikali na shirika lake, wanaona fahari gani kila siku kuwa wataalam tu wa kutoa ratiba za mgao, hivi utoaji wa huduma za umeme hatuwezi tukafanya kama makampuni ya simu.? Turuhusu ushindani katika sekta hii wadau.....alafu ndo tunaambiwa tudumishe amani. Ni amani gani hii ya kuumizana? Kutojaliana? Huu ni unafiki wa viongozi wetu....nini hatima ya kilio hiki wana JF?