TANESCO mbona mnatupa TOKENI tatu tatu?

TANESCO mbona mnatupa TOKENI tatu tatu?

rom99

New Member
Joined
Jul 2, 2024
Posts
1
Reaction score
1
TANESCO nashangaa na sielewi mbona mnatupa TOKENI tatu tatu?. Aisee kuandika hayo manamba ni kazi sana rudini kwenye utaratibu wa tokeni moja.

Screenshot_20240702-202226~2.png
 
Mi mwenyewe juzi kati nimemaind ivo ivo mkuu
Au waliona kuna wahuni wanajua kuzibuni token zao hahaha!?
 
TANESCO nashangaa na sielewi mbona mnatupa TOKENI tatu tatu?. Aisee kuandika hayo manamba ni kazi sana rudini kwenye utaratibu wa tokeni moja.

View attachment 3031867
Hizo zingine ni security codes ambazo mtumiaji huingiza mara moja tu, kisha baadaye unaendelea kama kawaida baada ya hizo.

Uwekaji wake ni speed bila kuacha nafasi ya mita kuanza upya. Zoezi hili linaenda mikoa kwa mikoa. Na lengo ni security tu.

Ova.
 
Mkuu em acha kulalamika hovyo, ilipaswa kuuliza na sio kutoa lawama.
Hapo umeambiwa mita yako inafanyiwa marekebisho na unatakiwa kuingiza hizo namba kwa mpangilio ili kufanya hayo marekebisho, sasa cjui unacholalamika kama mtoto wa kike n nn

Anyway, umeficha hizo namba kwa kujiona una akili kumbe kichwa maji.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mbona umeficha hiyo afu 5 . Tunataka tuone umepata unit ngapi
 
Hizo zingine ni security codes ambazo mtumiaji huingiza mara moja tu, kisha baadaye unaendelea kama kawaida baada ya hizo.

Uwekaji wake ni speed bila kuacha nafasi ya mita kuanza upya. Zoezi hili linaenda mikoa kwa mikoa. Na lengo ni security tu.

Ova.
Wanalinda kitu gan, mita zisidukuliwe au ?
 
Ila wabongo mnapenda kulalamika asee

Yaani Tanesco kupiga kote kelele juu ya hili swala na taarifa yote waliyotuma unalalamika kweli?

Acha uzembe! Ishi na dunia acha kulaumu watu kwa uzembe wako
 
Mkuu em acha kulalamika hovyo, ilipaswa kuuliza na sio kutoa lawama.
Hapo umeambiwa mita yako inafanyiwa marekebisho na unatakiwa kuingiza hizo namba kwa mpangilio ili kufanya hayo marekebisho, sasa cjui unacholalamika kama mtoto wa kike n nn

Anyway, umeficha hizo namba kwa kujiona una akili kumbe kichwa maji.
Zinaitwa funguo za kufungua luku. Ukifungiwa luku mpya, umeme wao ukiisha, kuna namba unazopewa zinaitwa funguo ili uendelee kuingiza umeme.
 
Zinaitwa funguo za kufungua luku. Ukifungiwa luku mpya, umeme wao ukiisha, kuna namba unazopewa zinaitwa funguo ili uendelee kuingiza umeme.
Sasa mtoa mada analalamika tuu utadhani amekatwa kichwa kufikiria kuomba msaada kujua
 
Wanalinda kitu gan, mita zisidukuliwe au ?
Kwa kawaida taasisi kubwa zinazotoa huduma kwa jamii zinazohusu malipo ya fedha, huwa na utaratibu wa kuwa huduma za security za Microsoft.

Kama vile mabenki, visimbuzi na hata kampuni za simu. Tanesco kwa mwaka wanalipa kama zaidi shilingi bilioni tatu hizo security.

Kwenye visimbuzi hizo code huwa tu zinaingia automatic, utaona kisimbuzi kinareboot kisha kama ina download na baadaye inarudi kuonesha vipindi.

Kwenye mabenki huwa ni suala la ndani. Kwa hiyo mifumo ya security ni moja ya biashara kubwa za Microsoft.

Ova
 
Sijaelewa kwanini umeficha baadhi ya namba😃
 
Sasa wewe unanunua umeme kwa hela ya supu (5000) utapewa ata token mia
 
Back
Top Bottom