TANESCO LUKU TOKEN

TANESCO LUKU TOKEN

Chief

Platinum Member
Joined
Jun 5, 2006
Posts
4,027
Reaction score
3,818
Tangu jana nimeshindwa kununua umeme kupitia Airtel na Halotel. Airtel nimekatwa hela na sijapata token. TANESCO shughulikieni tatizo hili tunalala gizani hela ya kununua umeme tunayo.
 
Nasikia zaidi ya umeme unaozalishwa unapotea kwa ajiri ya miundo mbinu ya hovyo 👎
 
Kuangalia salio kwa CIU yako inakubali?

Mie iligoma pote hadi kwa mawakala,nikapiga huduma kwa wateja wakaomba namba ya mita,nikaambiwa CIU yangu ya kubadilisha.
 
TANESCO

Tunaomba ufafanuzi kuhusiana na hii changamoto.
Mrejesho: Nimepiga simu customer service hatimaye nimempata mhudumu ambaye kanieleza kuna deni la jengo ambalo sijalipa zaidi ya mwaka (sijui waliniruhusu kununua vipi umeme siku zote hizo) hivyo wamelifufua na nisinunue umeme chini ya kiwango fulani ili kulipa deni hilo. Baada ya kufanya hivyo nikafanikiwa kupata token.
 
Mrejesho: Nimepiga simu customer service hatimaye nimempata mhudumu ambaye kanieleza kuna deni la jengo ambalo sijalipa zaidi ya mwaka (sijui waliniruhusu kununua vipi umeme siku zote hizo) hivyo wamelifufua na nisinunue umeme chini ya kiwango fulani ili kulipa deni hilo. Baada ya kufanya hivyo nikafanikiwa kupata token.
Hapo sawa umesomeka mkuu.
 
Tangu jana nimeshindwa kununua umeme kupitia Airtel na Halotel. Airtel nimekatwa hela na sijapata token. TANESCO shughulikieni tatizo hili tunalala gizani hela ya kununua umeme tunayo.

Hapo sawa umesomeka mkuu.
Habari Chief.

Tunafurahi kufahamu kuwa umefanikiwa kupata huduma kuhusu suala lako. Endapo utahitaji msaada zaidi au utapata changamoto nyingine yoyote, tafadhali usisite kuwasiliana nasi.

Asante na karibu sana! ^FL
 
Tanesco na NMB mnatutesa sana hatuwezi nunua umeme na unit zimeisha

Walionunua hawajapa Token Hadi leo
 
Tanesco na NMB mnatutesa sana hatuwezi nunua umeme na unit zimeisha

Walionunua hawajapa Token Hadi leo
Habari, ndugu mteja.

Pole sana kwa changamoto unayopitia. Tafadhali tutumie namba ya mita yako ili tuweze kufanya ufuatiliaji na kukupatia msaada zaidi.

Asante! ^GK
 
Back
Top Bottom