..jamaa wa ewura ni kama refarii.
..anatetea watumiaji na wazalishaji.
..pia anaamua baada ya shauri kupelekwa mbele ya baraza la wadau.
..sasa Tanesco walipeleka ombi umeme upande kwa 18% lakini ewura wamewapa 8%. Kwa hiyo utaona kwamba mdhibiti ameangalia pande zote--watumiaji na wazalishaji huduma.
..sasa kwa uelewa wangu sheria ya udhibiti wa hizi huduma inamzuia waziri kuingilia maamuzi yanayotolewa na mamlaka za udhibiti.
..huko tunakoelekea, bahati mbaya ua nzuri watawala huwa hawatuambii ukweli, sekta ya Nishati na Umeme itashirikisha makampuni binafsi.
..Msije mkashangaa sekta ya nishati na umeme ikawa kama sekta ya mawasiliano ambapo kuna makampuni mengi binafsi ya simu.
Ndiko tunakoelekea huko.
..sasa kukiwa na ushindani Waziri hawezi kuingilia na kupangia bei watoa huduma.
..Kwa maoni yangu huu uamuzi ni wa muda tu kulingana na upepo wa kisiasa. Kinachosababisha Tanesco wapandishe bei ya umeme siyo Wakurugenzi wabovu bali ni mikataba ya kifisadi baina yake na independent power producers kama IPTL na wengine.
..hili suala la Tanesco na kujikanganya baina ya Magufuli na Muhongo kuhusu Tanesco lilishaletwa hapa JF na mwanachama anaitwa
HNIC lakini wachangiaji wakawa wanambeza.