Tamko la TPN: Ni uzalendo au ukada?

Sophist

Platinum Member
Mar 26, 2009
4,484
3,400
Tafadhali jisomee mwenyewe msimamo wa TPN kuhusiana na mgomo wa madaktari hapa nchini. Viongozi wa TPN wamesukumwa na uzalendo au ukada?
Tanzania ProfessionalsNetwork (TPN) P.O. Box 21605 Dar EsSalaam -0784-618320/0713-334078/0716898685/0658-482597/0755067-594

February 2,2012

Pressrelease:
Kwamuda mrefu sasa jamii yetu imekumbwa na migogoro na migomo ya mara kwa marakatika sekta mbalimbali ikiwemo Afya, Elimu n.k.
Nainaonekana kwamba hali hii inataka kuzoeleka na kuonekana ni hali ya kawaida,na kama haitathibitiwa kwa kupatiwa ufumbuzi wa kudumu basi inawezaikalifikisha Taifa letu mahali pabaya na kupunguza kasi ya ukuaji wa uchumi nahivyo kuathiri mikakati ya kupunguza umasikini.

Kwasasa dunia nzima iko katika hali tete kutokana na kudorora kwa uchumi na baadhiya nchi ukuaji wa uchumi umesimama au umeshuka sana hivyo kwa namna moja aunyingine nchi zetu pia zinaathirika na hali hii kwa njia moja au nyingine.
Kwakuzingatia hali hiyo sisi wanataaluma tunaona kwamba kwa sasa rasilimalitulizonazo ikiwemo watu, ardhi, maliasili n.k tuzitumie vizuri ili zitusaidiekupambana na janga hilo.

Kwahali hiyo ni dhahiri uwezo wa serikali kugharamia baadhi ya huduma utapunguahivyo basi tunaomba kwa sasa wananchi waelewe hali hivyo na ni jukumu letu sotesasa kushirikiana kupambana na changamoto hizo.

Chanzokimojawapo cha migomo na migogoro hiyo ni kupungua kwa mawasiliano miongoni mwawadau husika hivyo kusababisha upande mmoja kutojua au kutohusishwa katikakututua tatizo husika.

Hivyobasi tunashauri wadau wote yaani serikali, viongozi, watendaji wa wizara nataasisi mbalimbali wakae na washirikishane katika sehemu zao za kazi nakupashana habari kwa muda muafaka.

Kuhusutatizo linaloendelea kwa sasa katika sekta ya afya tunawapa pole nyingi sanawatanzania wote waliopoteza maisha na waliaothirika kwa namna moja au nyinginekutokana na athari za mgomo huu.

Baadhiwa waliaothirika yaani wagonjwa na baadhi ya madaktari ni wanachama wetu.
Sisikama wanataaluma tunaipongeza serikali kwa hatua zilizochokuliwa hadi sasa zakupunguza athari za tatizo hili japokuwa bado sehemu nyingine hali badohaijatengemaa lakini ni matumani yetu kila mtu atatimiza wajibu wake kwa mujibuwa taaluma zao.

TunaiombaSerikali iharakishe mazungumzo na madaktari na itoe ahadi ya kutekeleza madaiya madaktari kadri uwezo utakavyoruhusu Tunaiomba Serikali ifikire upya uamuziwake wa awali wa kuwafukuza kazi wale madaktari ambao walikuwa badohawajaripoti kazini kama agizo la Mh. Waziri Mkuu lilivyoelekeza badala yaketunashauri hatua nyingine za kinidhamu zichukuliwe badala ya kuwafukuza kazi,kwa sasa bado nchi ina upungufu mkubwa wa wataalamu katika sekta hii.

Tunawashaurimadaktari wote nchini wakati madai yao yakishughulikiwa warejee katika maeneoyao ya kazi na wafanye kazi kwa bidii na maarifa yao yote, waonyeshe uzalendokwa nchi yao.

Walewote walitajwa katika taarifa mbalimbali kwa tuhuma mbalimbali ikiwa ni pamojana kushindwa kuwajibika kwa kutoa kauli zilizochochea au kukuza mgogoro huubasi waombe radhi mara moja na kama wakishindwa basi hatua za kinidhamuzichukuliwe haraka dhidi yao.

Tunaombawatanzania wote, viongozi, watendaji wa Taasisi za umma na binafsi tuwewaadilifu tuzingatie dhana ya utawala na uongozi bora, tuwe wazalendo wa kwelina tuweke mbele Utaifa na maslahi ya walio wengi.

Phares Magesa
Rais- TPN
 
Hili si tamko...Hamna kitu hapo, halina uzito wowote. An Empy Basin
 
kama haya ndiyo maoni ya wanachama wao basi bado tunayo safari ndefu sana kutoka hapa tulipokwama! mbaya zaidi eti haya ni maoni ya wasomi. kama siyo kutafuta ubunge wa viti maalumu CCM ni nini hii? aibu!
 
Jukumu la kutoa huduma za afya (kwa watanzania wote) liko kwa serikali. Hilo tuelewe. Madaktari wanafanya kazi kwa makubaliano (contract) na serikali lakini hili halimanishi hata kidogo kuwa madaktari ndio wenye jukumu hilo. Na makubaliano hayo kila mmoja ana wajibu wake: Madaktari watoe ujuzi wao (huduma) na serikali igharamie huduma hapa ikimaanisha vitendea kazi, pamoja na mishahara.

Je, kila upande umetekeleza wajibu wake kama walivyokubaliana? Hivi ukingia mkataba na mkandarasi akujengee nyumba na ukaahidi kuwa utaleja saruji, matofali, mabati, na ikatokea hukuleta utamlaumu huyo mkandarasi kama hakujenga nyumba? Hospitali hazina dawa, hazina vifaa, wanategemea nini? Yeyote anayebisha kuwa hospitali zetu hazina vifaa aseme ni kwanini wakubwa wanaenda India? Tanzania inaongoza Afrika nzima kwa kupelea wagonjwa India. Kwa utajiri gani tulio nao?

Hii hadithi kuwa hali mbaya ya uchumi wa dunia inaathiri Tanzania kwangu mimi ni sawa na 'chekundu cheusu'. Ugumu Tanzania? Kwa vipi? posho? mashangingi? ugumu gani wakati matanuzi yako pale pale?

Tanzania kama kweli tulikuwa na watu makini hatutakiwi kabisa kulia na mambo ya uchumi wa dunia. Tuna madini, na kipindi chote cha mdororo wa uchumi wa dunia bei ya dhahabu imezidi kupanda maana watu wanaona ndio asset isiyopungua thamani. Hivyo sisi kama tulikuwa makini huu ungekuwa msimu wetu wa kuvuna. Australia wanapeta kutokana na mchango wa madini na hawana hata nusu ya rasilimali ya madini tuliyonayo.
 
Ni ujikombi wa mwisho sijawahi kuona, kwanza halijajadiliwa na mtu yoyote ni huyo Phares kaliandikia chumbani anatafuta lcous kwa kuliita la TPN, mimi nilikua active member wa TPN tangu enzi za Mtsimbe lakini sikuwahi kuona uchafu kama huu, tangu leo nimejitoa. Hivi kuna mtu anaweza kujiita professional katika nchi yoyote ikiwemo ndogo kama Gambia akaandika ushuzi kama huo? Phares Magesa ajiuzulu mara moja toka TPN ama sivyo abaki na TPN yake peke yake, hatuwezi kutumiwa na wagombea ubunge wa magamba kusukuma agenda zake, pu pu pu huu ni udhalilishaji wa hali ya juu sikutegemea kuuona katika maisha yangu yote. Sasa hivi tunataka TPN iitishe uchaguzi mara moja kujadili haya huku ni kuwazalilisha madaktari kwa maslahi binafsi, mnafiki mkubwa. Naomba binafsi kutoa pole kwa madaktari waliozalilishwa na kuomba member wote wa JF ambao ni member wa TPN wasiokubaliana na msimamo huu waunge mkono hapa kuonyesha kwamba sisi kwetu uzalendo ndio uko mbele kuliko matumbo yetu.
 
Mimi sikubaliani na statement kuwa uchumi wa dunia umedorora kwa hiyo hata sisi hali mbaya tuliyonayo ni katika mwingiliano uliopo! Ni tegemeo langu kungekuwa na management nzuri ya resource tulizonazo tungekuwa tunaandika nne! Tatizo ni mismanagement iliyopo kutoka juu mpaka chini-corruption. Hata mwananchi ukishiriki kwa kujituma kwa nafasi yako uliyonayo katika jamii na unachozalisha kinakuwa-mismanaged tutafika? Kama madaktari wanajituma kwa uwezo wao wote wakiishi maisha magumu wakaona hao waheshimiwa wanajiongezea posho mara 5 kwanini nao wasidai nao waongezewe waweze kujikimu na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi?
 
Jukumu la kutoa huduma za afya (kwa watanzania wote) liko kwa serikali. Hilo tuelewe. Madaktari wanafanya kazi kwa makubaliano (contract) na serikali lakini hili halimanishi hata kidogo kuwa madaktari ndio wenye jukumu hilo. Na makubaliano hayo kila mmoja ana wajibu wake: Madaktari watoe ujuzi wao (huduma) na serikali igharamie huduma hapa ikimaanisha vitendea kazi, pamoja na mishahara.

Je, kila upande umetekeleza wajibu wake kama walivyokubaliana? Hivi ukingia mkataba na mkandarasi akujengee nyumba na ukaahidi kuwa utaleja saruji, matofali, mabati, na ikatokea hukuleta utamlaumu huyo mkandarasi kama hakujenga nyumba? Hospitali hazina dawa, hazina vifaa, wanategemea nini? Yeyote anayebisha kuwa hospitali zetu hazina vifaa aseme ni kwanini wakubwa wanaenda India? Tanzania inaongoza Afrika nzima kwa kupelea wagonjwa India. Kwa utajiri gani tulio nao?

Hii hadithi kuwa hali mbaya ya uchumi wa dunia inaathiri Tanzania kwangu mimi ni sawa na 'chekundu cheusu'. Ugumu Tanzania? Kwa vipi? posho? mashangingi? ugumu gani wakati matanuzi yako pale pale?

Tanzania kama kweli tulikuwa na watu makini hatutakiwi kabisa kulia na mambo ya uchumi wa dunia. Tuna madini, na kipindi chote cha mdororo wa uchumi wa dunia bei ya dhahabu imezidi kupanda maana watu wanaona ndio asset isiyopungua thamani. Hivyo sisi kama tulikuwa makini huu ungekuwa msimu wetu wa kuvuna. Australia wanapeta kutokana na mchango wa madini na hawana hata nusu ya rasilimali ya madini tuliyonayo.

Well said!
 
In God's economy...
- There is NO recession
- There is NO financial crisis
- There is NO shortage of jobs.

Kwa nchi kama hii yenye rasilimali nyingi, tungeweza hata kuwapa allowance wazee. Nani kasema kama kuna shida ya pesa sote lazima tuwe nayo. Kuna watu bongo hii hii hawaibi sio mafisadi wala nini lakini shida hawana kwasababu hawaishi kwa kushindana. Ukitaka kujua nchi hii inafuja pesa angalia mashangingi ya mawaziri, manaibu, wakuu wa idara, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, Government agencies. Angalia per diem zao not less than $300 per day. Misafara ya wakuu nje ya nchi. Yaani basi tu. Mkulo anadiriki kusema kuwa serikali inatumia billioni 360 kwa posho kati ya hizo 14 billioni ni kwa wabunge peke yake. Na anaongea bila kumun'gunya. Jamani hawa watu wanalipwa mishahara. Huwa nashindwa kuelewa the so called 'posho' sijui zilianza lini na kwa nini?

Leo unaombwa pesa kidogo tu tena kwa ajili ya kuwahudumia wapiga kura wako unajibu siasa. Hilo tamko la TPN lilitakiwa liende shule kabisa.
 
he is just another opportunist like kibonde! kwa matamko kama haya unaweza pata picha kwa nini nchi yetu haiendelei hivi huyu anaweza akajibu swali kwa nini nchi hii ina kila kitu ambacho a country would wish to have ili i develop lakini ni sisi tu ndio hatuendelei!
 
Ndo maana hivi vyama vingine huwa hatuna papara ya kujiunga navyo. Afadhali niwe mwanachama au shabiki wa Akudo au Twangapepeta nijue moja.Havina agenda ya kweli hata kidogo. Ni kula tu na ujanja ujanja wa watu wachache. Ukiona hivyo jua tayari kuna pandikizi....
 
Moja kati ya madai ya madaktari ni kumtaka KM kujiuzuru, je mdororo wa uchumi unaingia vipi katika hili? Hata kupatiwa audience na viongozi mnasingizia hali ya uchumi??? Jamani wachumi tunaomba kuelimishwa kidogo hapo.
 
Si muda tutasikia Bwa Phares Magesa anatangazwa kuwa Katibu Mkuu, ama barozi, ama anateuliwa kuwa mbunge
 
Back
Top Bottom