Sophist
Platinum Member
- Mar 26, 2009
- 4,484
- 3,400
Tafadhali jisomee mwenyewe msimamo wa TPN kuhusiana na mgomo wa madaktari hapa nchini. Viongozi wa TPN wamesukumwa na uzalendo au ukada?
Tanzania ProfessionalsNetwork (TPN) P.O. Box 21605 Dar EsSalaam -0784-618320/0713-334078/0716898685/0658-482597/0755067-594
February 2,2012
Pressrelease:Kwamuda mrefu sasa jamii yetu imekumbwa na migogoro na migomo ya mara kwa marakatika sekta mbalimbali ikiwemo Afya, Elimu n.k.
Nainaonekana kwamba hali hii inataka kuzoeleka na kuonekana ni hali ya kawaida,na kama haitathibitiwa kwa kupatiwa ufumbuzi wa kudumu basi inawezaikalifikisha Taifa letu mahali pabaya na kupunguza kasi ya ukuaji wa uchumi nahivyo kuathiri mikakati ya kupunguza umasikini.
Kwasasa dunia nzima iko katika hali tete kutokana na kudorora kwa uchumi na baadhiya nchi ukuaji wa uchumi umesimama au umeshuka sana hivyo kwa namna moja aunyingine nchi zetu pia zinaathirika na hali hii kwa njia moja au nyingine.
Kwakuzingatia hali hiyo sisi wanataaluma tunaona kwamba kwa sasa rasilimalitulizonazo ikiwemo watu, ardhi, maliasili n.k tuzitumie vizuri ili zitusaidiekupambana na janga hilo.
Kwahali hiyo ni dhahiri uwezo wa serikali kugharamia baadhi ya huduma utapunguahivyo basi tunaomba kwa sasa wananchi waelewe hali hivyo na ni jukumu letu sotesasa kushirikiana kupambana na changamoto hizo.
Chanzokimojawapo cha migomo na migogoro hiyo ni kupungua kwa mawasiliano miongoni mwawadau husika hivyo kusababisha upande mmoja kutojua au kutohusishwa katikakututua tatizo husika.
Hivyobasi tunashauri wadau wote yaani serikali, viongozi, watendaji wa wizara nataasisi mbalimbali wakae na washirikishane katika sehemu zao za kazi nakupashana habari kwa muda muafaka.
Kuhusutatizo linaloendelea kwa sasa katika sekta ya afya tunawapa pole nyingi sanawatanzania wote waliopoteza maisha na waliaothirika kwa namna moja au nyinginekutokana na athari za mgomo huu.
Baadhiwa waliaothirika yaani wagonjwa na baadhi ya madaktari ni wanachama wetu.
Sisikama wanataaluma tunaipongeza serikali kwa hatua zilizochokuliwa hadi sasa zakupunguza athari za tatizo hili japokuwa bado sehemu nyingine hali badohaijatengemaa lakini ni matumani yetu kila mtu atatimiza wajibu wake kwa mujibuwa taaluma zao.
TunaiombaSerikali iharakishe mazungumzo na madaktari na itoe ahadi ya kutekeleza madaiya madaktari kadri uwezo utakavyoruhusu Tunaiomba Serikali ifikire upya uamuziwake wa awali wa kuwafukuza kazi wale madaktari ambao walikuwa badohawajaripoti kazini kama agizo la Mh. Waziri Mkuu lilivyoelekeza badala yaketunashauri hatua nyingine za kinidhamu zichukuliwe badala ya kuwafukuza kazi,kwa sasa bado nchi ina upungufu mkubwa wa wataalamu katika sekta hii.
Tunawashaurimadaktari wote nchini wakati madai yao yakishughulikiwa warejee katika maeneoyao ya kazi na wafanye kazi kwa bidii na maarifa yao yote, waonyeshe uzalendokwa nchi yao.
Walewote walitajwa katika taarifa mbalimbali kwa tuhuma mbalimbali ikiwa ni pamojana kushindwa kuwajibika kwa kutoa kauli zilizochochea au kukuza mgogoro huubasi waombe radhi mara moja na kama wakishindwa basi hatua za kinidhamuzichukuliwe haraka dhidi yao.
Tunaombawatanzania wote, viongozi, watendaji wa Taasisi za umma na binafsi tuwewaadilifu tuzingatie dhana ya utawala na uongozi bora, tuwe wazalendo wa kwelina tuweke mbele Utaifa na maslahi ya walio wengi.
Phares Magesa
Rais- TPN