Huyu mheshimiwa aliwahi kusema kuwa "hatokosa usingizi na hatojali kama taifa letu tukufu likiingia kwenye giza kwa kukosa umeme"
Nadhani its about time na yeye aje atoe tamko lake kwa nini yeye anaona ni sawa kwa waTanzania na baadhi yao wapiga kuwa wake kuendelea kukosa umeme na huduma zingine muhimu.
Mashabiki wake ambao wanajiita wapiganaji waliopo USA,ULAYA na CANADA najua watakuja kumtetea lakini nadhani itakuwa si vibaya kwa huyu bwana Mwakyembe akaja kutoa tamko ili tujue maoni yake kuhusu hii adha, je imebadilika au la?
Ni kweli kabisa mkuu.Badala ya kufanya kazi kuondoa adha ya umeme iliyodumu kwa muda mrefu sasa, tunakaza kulazimisha kwamba mitambo ya Dowans is the only solution. What about IPTL ambayo imekaa bila kuzalisha umeme kwa zaidi ya mwaka sasa? Na yote haya yanatusumbua sasa kwasababu ya rushwa na tamaa za watu wachache wakishirikiana na wana siasa. Imefika mahala sasa siasa zikae pembeni, tuanze kufanya kazi kama watu wenye vichwa vyenye kufikiri.Hizi danadana za kutafuta justification ya kitu ambacho siyo sahihi hazinisaidii mimi binafsi na naamini na wengine wengi.Tutende haki jamani,kazi ya kuzalisha umeme na kuweka mikakati ya umeme endelevu ni ya TANESCO kwani tunalipa kodi zetu na umeme pia tunaulipia. Mwakyembe alitekeleza majukumu yake.
Kila mtu akitekeleza majukumu yake haya mambo yatabaki kuwa historia.Pia, Biashara na siasa haviendi pamoja,kila mtu anaingia kwenye siasa kwa maslahi ya kibiashara. Inapotokea mtu anatakiwa kuchukua maamuzi magumu anashindwa kwani ataharibu maslahi yake ya kibiashara.
Kila mtu atekeleze wajibu wake,kama mwanasiasa fanya kazi yako,watumishi wa TANESCO fanyeni kazi yenu, wanasheria wafanye kazi zao,kila kitu kitaenda sawa. Kama kuna watu wanafanya kazi zao na wengine wanafanya kuturudisha nyuma hatutafika popote.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.