Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 4,058
- 16,927
Dalili ya wenye upungufu wa nguvu za kiume inazidi kuongezeka.
Mwanaume mwenye akili timamu,
Mwenye nguvu ya mwili na mwenye hofu ya Mungu lazima aoe , halafu ampende mke wake,ikiwa ni pamoja na kumpa huduma zote.
Chakula kizuri,
Mavazi mazuri,
Malazi mazuri,
Pamoja na kumridhisha kwenye kila angle.
Tatizo wanaume wa sasa mnataka mpendwe na wake (mademu)zenu hili ni kosa.
Mwanamke kazi yake ni kukuheshimu na kukuweka kwenye kifua chake yaani ukimfanyia mazuri atajitoa mzima mzima na kujaa kwako anakuwa hajiwezi.
Hana atachokufanyia zaidi ya kukuzalia tena asilimia nyingi watoto lazima wafanane na wewe.
Wakuu key ya hapa ni kufanya kazi Kwa bidii mno, mwanamke anapenda kuwa na mwanaume atakaye tatua matatizo yake.
Kwenye biblia katika kitabu cha mwanzo,Yakobo alifanya kazi miaka saba ili ampate Raheli,licha ya kutimiza miaka hiyo hakupewa aliyemtarajia badala yake akaongeza miaka saba mingine ili tu kumpata aliyemkusudia hebu fikiria miaka 14 mtu anakubali kuwa mtumwa ili tu kumpata mwanamke.
Wazee, Ndoa siyo ya mwanaume aliyelegea, ndoa siyo Kwa mwanaume mchoyo na mbinafsi , ndoa siyo Kwa mtu mwenye kupenda mteremko,ndoa ni kwaajili ya wenye AKILI TIMAMU.
Mwanaume mwenye akili timamu,
Mwenye nguvu ya mwili na mwenye hofu ya Mungu lazima aoe , halafu ampende mke wake,ikiwa ni pamoja na kumpa huduma zote.
Chakula kizuri,
Mavazi mazuri,
Malazi mazuri,
Pamoja na kumridhisha kwenye kila angle.
Tatizo wanaume wa sasa mnataka mpendwe na wake (mademu)zenu hili ni kosa.
Mwanamke kazi yake ni kukuheshimu na kukuweka kwenye kifua chake yaani ukimfanyia mazuri atajitoa mzima mzima na kujaa kwako anakuwa hajiwezi.
Hana atachokufanyia zaidi ya kukuzalia tena asilimia nyingi watoto lazima wafanane na wewe.
Wakuu key ya hapa ni kufanya kazi Kwa bidii mno, mwanamke anapenda kuwa na mwanaume atakaye tatua matatizo yake.
Kwenye biblia katika kitabu cha mwanzo,Yakobo alifanya kazi miaka saba ili ampate Raheli,licha ya kutimiza miaka hiyo hakupewa aliyemtarajia badala yake akaongeza miaka saba mingine ili tu kumpata aliyemkusudia hebu fikiria miaka 14 mtu anakubali kuwa mtumwa ili tu kumpata mwanamke.
Wazee, Ndoa siyo ya mwanaume aliyelegea, ndoa siyo Kwa mwanaume mchoyo na mbinafsi , ndoa siyo Kwa mtu mwenye kupenda mteremko,ndoa ni kwaajili ya wenye AKILI TIMAMU.