TAMISEMI inahitaji kufumuliwa

TAMISEMI inahitaji kufumuliwa

A

Anonymous

Guest
Kuna uozo Mkubwa sana unaendelea Tamisemi kupitia halmashauri zetu Kuna pesa za idara OC Zinaliwa juu Kwa juu haziwafikii wahusika.

Kuna ukiritimba mwingi sana Imagine HR wa Halmashaurj anasema amekuajiri yeye anaweza kukufukuza kazi.

Mfumo wa kuthibitisha watu kazini ni mbovu unaweza jikuta umekaa miaka miwili bila ya kuthibithishwa na huna tatizo lolote lile na barua ikitoka unatoka tarehe za nyumba. Inakuwaje Baraza la madiwa Lina mandate ya kuthibitisha watumishi wa Umma?

Walimu/wafawidhi ndio wanaosimamia na kuratibu Shughuli za miradi katika vituo vyao vya kazi badala ya kujikita katika professional yako. Nadhani Tanzania ndio tunafanya huu utaratibu wa hovyo tutakuja kuwaua walimu na wafawidhi kwa pressure Kwa kuwaptia kazi ambazo siyo zao.

Civil Engineer hawatakiwi kuwepo kwenye baadhi ya Halmashauri Kwa sababu ni matumizi mabaya ya taaluma zao imagine mtu anasoma degree kuanzia miaka minne anakuja kusimamia matundu ya vyoo na vyumba vya madarasa inatafakarisha sana Kwan tunadumaza taaluma zao.

Miundombinu mingi ya shule, Vituo vya afya na zahanati ni chakavu halmashauri hazina plan yoyote mpaka mwanasiasi apite ndio wakurupuke, Kuna haja na Idara ya miundombinu kuwa Tasisi inayojitegemea tunaweza kuona matokea chanya.

Fedha za usimamizi wa miradi hasa iliyopo halmashauri haziwafikii walengwa hasa Engineer(miradi yote inakuwa na %10 ya usimamizi) lakini local government haifiki halmashauri na kama ikifika wanakula watu wakubwa wadogo hawalambi hata kitu

TAMISEMI wana Wakala wa Barabara TARURA Kwa Nini miradi yote ya Barabara za mijini ya Barabara isiende TARURA? Unakuta halmashauri Ina miradi yake ya Barabara. Kuna miradi mingine inasimamiwa na Wizara kama wizara, kwa Nini ishu zote za Ujenzi wa Barabara isiende TARURA??

Hela za kujikimu kutolipwa Kwa wakati au hazilipwi kabisa kwenye halmashauri nyingi sana, wengi wanalipwa pesa ambayo sio kiwango kinachotakiwa Kuna wanaopaswa kulipwa Kwa rate ya 150,000/= Au 130,000/= hulipwa flat rate ya 80,000/= hivyo wakurugenzi wa mtu wa fedha hushirikia kuipa pesa ya watu wengine. Reform inahitajika.

Mfumo uwepo hela zote zilipiwe Hazina hasa hasa watumishi wa Halmashauri maana watu wanaweza wakaandika dokezo wakandika jina lako then hela zikachuliwa juu Kwa juu

Mh waziri mkuu fanyeni mabadiliko ofisi yako Ina jukumu kubwa sana, shida mkiwa mmekaa wizarani hamuangalii watu wa chini yenu mnajilimbikizia nyie tu, mkitaka kujua Khali halisi njoo muongee na wafanyakazi wenu wa kawaida ambao hawana vyeo maana wenye vyeo wanalindana

Kama haya yanatushinda tutaweza kubadiliasha katiba mpya?
 
Shida umeandika kwa mhemiko sana,,ungetulia ungekuja na hoja,,nikusaidie vitu vichache
1.OC zinakuja kwa kila idara,hivyo matumizi yake hayapangiwi na mtu yeyote
2.Bodi ya ajira ndiyo inayothibitisha watumishi na siyo madiwani,,,mara nyingi inategemea na bajeti ya kuitisha hiyo bodi ya ajira,,mara nyingi wanavizia kipindi ambacho labda kuna usaili,,
 
hovyo sana eneo hilo wao hela za miradi zikisoma kwenye akaunt huita dili limeingia
 
Back
Top Bottom