Tambwe Hizza: Nitagombea Urais

Tambwe Hizza: Nitagombea Urais

Mbona mda tu, huoni matendo na kauli zake

Hahahaha. Umeua mkuu mbavu sina na kuna mmoja nadhani ni Kibajaji au Mwigulu Arumeru aliahidi Nassari akishinda atatembea uchi Arusha hadi Dar hizi ni akili za misukule.
 
alishawahi kusema kuwa akihamia CCM toka upinzani basi lazima awe kalala na mama yake!

KASHAMLALA?

Umenikumbusha story iliyo-hit wakati huu mwana siasa huyu alivyokuwa machachari (by then alikuwa anajoin CUF akitokea CCM), maneno hayo kimsingi hayakuwapendeza wana CCM achilia mbali watu wenye akili zao timamu. Siku alipo achana na siasa za mageuzi (wengi huziita siasa za upinzani) akikiacha chama cha CUF na kurudi nyumbani CCM (nyumba aliyoirushia vijembe kwa lugha isiyofaa) magazeti yali report kwa headings tofauti zikimkejeli kwa reflection ya swali ulilouliza hapo juu. Tunachoweza kujifunza kutokana na kauli zake, ni muhimu kwa wana siasa kupima kauli na maneno kabla hawajayatamka because ni maneno yakishatamkwa hayarudi kinywani tena, na mbaya zaidi yataendelea kuwa hukumu juu yako.

Pili, ukiachilia kuwa kwa siku za karibuni, Urais kama Taasisi, imefanywa rahisi, kiasi kwamba kila mtu anadhani anaweza kuwa mkuu wa Kaya, ni muhimu kuwapa watu nafasi ya ku-excercise demokrasia, sasa kama wana sifa stahiki ni jambo la vikao vya chama husika/au wananchi kuamua kupitia sanduku la kura. TUSIWABEZE, tusiwatukane, tusiwakejeli bali tuwasikilize kupitia mijadala ya wazi, tuwaulize maswali magumu, tupime majibu yao kama yana kidhi haja, tuwajadili kisha tufanye maamuzi sahihi, hapo naamini tutapata kiongozi tumtakaye.

Tatu, kuongoza nchi maskini ni mzigo kwa kiongozi mtendaji lakini siku za hivi karibuni imekuwa tofauti, hata media zina report, bwana so and so 'KAULA', bibi so and so 'KAULA' wakimaanisha kachaguliwa au kuteuliwa kuwatumikia Watanzania katika wadhifa fulani. Kiongozi unaula? kweli? hapo kuna kiongozi au mtawala? tena mtawala asiyejali maslahi ya watu achilia mbali nchi yake.
 
alishawahi kusema kuwa akihamia CCM toka upinzani basi lazima awe kalala na mama yake!

KASHAMLALA?
ndiyo hivyo tena,anatumia demokrasia yake.cdm asingekubaliwa hana maadili, ni afadhali ngamia ana maadili kuliko huyu hiza,vipi tumbo halimsumbui tena?
 
Kugombea sio ishu, ila ni mtu asie na msimamo. Huyu jamaa ni zile kelele za chura. Nchi yoyote wanapo elekea uchaguzi vituko kama hivi havikosekani. Kwahivyo, mutasikia mengi na bado yakuhama vyama akina Shibuda na wengine wengi. Kila mmoja hutafuta riziki wakati wa uchaguzi. Tulieni tu, mutaona na kusikia mengi.
 
daah kwa namna hii hata MSALANI nae si ajabu akatangaza kugombea urais.

We vipi ... mbona ita'sound' vizuri tu ... imagine President Msalani, kwa kiswahili kingine President Choo, au ukitaka kwa kiingereza President Toilet, au President Lavatory wa Tanzania
 
nini tambwe hiza watu tumeona hamisi tambwe aende zake huko labda awe rais wa kona bar
 
Si wanamwona Jk wa pili kila siku yuko hewani, travelling is an adventure kila mtu anapenda kusafiri kwenda ulaya na marekani kwa mwezi mara mbili. Hata mimi muda ukifika nitagombea
 
Haki ya mama Tambwe amewaacha hoi mamia ya watanzania!
 
Acha dharau za kijinga!

Hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha magamba kila mtu anataka kugombea urais..kweli kikwete kashusha hadhi ya urais
 
Kweli kumekucha ccm, hata vibwengo navyo vinajiona vinafaa kuwa Rais! Why? Urais umekuwa rahisi mno! Kama nchi inaweza kujiendesha yenyewe tena bila remote controlling (Rais muda wote u nje ya nchi) tuna haja gani kuwa na serious Raisi? Hata Tambwe anaweza kukaa pale Ikulu, ili mradi tu ana manguo yale ya kijani!!! Ccm hebu kuweni serious na nchi yetu badala ya kuifanya kama kichwa cha mwendawazimu, vinginevyo tuachieni nchi yetu kama mmelewa hivyo madaraka
Duu umeua mkuu...
 
Kuna mvuvi mmoja wa samaki ktk bwawa la Mindu nae ni kada mzuri sana wa CCM nae kaita waandishi wa habari kaweka nia ya kugombea URAISI 2015!
 
Back
Top Bottom