Tall building a threat to Ikulu

Nchi yetu ni ya kusadikika kweli kwani tunangoja mpaka mambo yameharibika ndio tunaanza kupiga mayowe!!! Acha hilo sakata la hilo ghorofa karibu na Ikulu; hivi sasa kuna ufisadi wa hali ya juu unafanywa kuhusiana na viwanja vya TANGANYIKA PACKERS, ambavyo inasemekana serikali imemrudishia fedha zake yule muwekezaji kutoka arabuni na sasa wameamua kuhujumu wenye nchi viwanja pale mahala. Ukipita kule chini karibu na hotel ya Mediterranian utakuta jamaa amekatiwa kiwanja kikubwa na anaharakisha kuzungusha ukuta na kuendeleza ile sehemu ingawa inasemekana kuna mpango kabambe wa NHC kujenga sehemu ile!!! Sasa ni wakati muafaka wa kumzuaia yule anayejenga ukuta sehemu ile kwani ujenzi wake utaathiri ramani iliyotayarishwa na NHCya kuendeleza sehemu ile!!! Meya wa Kinondoni Mwenda should be held accountable kwa ufisadi huu.
 
suala la Ikulu kuzungukwa na majengo makubwa si geni. Angalia white house ya USA ilivyo

images
 
Hivi kwani mpaka jengo hili linajengwa floor 1,2,3,4,5....mpaka linaisha,hawa wanausalama walikuwa wapi?au ndo hawa wanawapa ajira watoto wa shangazi na mjomba?Maana kwa matamko yanayotokewa na kurugenzi ya Ikulu,haiitaji degree kujua kuwa nafasi hizo zinatolewa kimjomba na kishangazi!
 
Tanzania nchi ya ajabu sana, kuna mlolongo wa vitu ambavyo vina uhusiano na rushwa kubwa kubwa; sababu haingii akilini jengo hadi linaisha na watu wanahamia then eti tunakurupuka kwamba jengo ni refu ambapo mtu aliyeko juu anaweza kuichungulia ikulu.

Chochote kitakachofanyika, hata kama kuvunjwa au kulikondisha kwa usalama wa taifa - lakini kweli utabaki pale pale kwamba uongozi wa nchi hii una dhaifu - kuanzia ngazi ya chini hadi juu.

Na kama mkiamua kulivunja - jiandaeni kulipa Mabillion kama yale ya Dowans!! sababu mmiliki ana hati halisi, ana ana kibali cha uwekezaji.

kwanini kuzunguka? kama kuna watu wanakula kodi yetu pasipokufanya kazi yao ni idara ya usalama wa taifa!!!! this is a DEAD BODY we r carrying! better be reformed!!!!!! we have lost in every front..kwenye uwekezaji, mipakani, mikataba, ushauri kwa viongozi, bandarini, sehemu ni nyingi, hakuna pahala uwepo wao umesaidia!
 
Lakini kutokana na mabadiliko ya tekinolojia hapa dunia waweza hit ikulu ukiwa popote pale.
Hapo sasa kama wanajari usalama wa Rais wetu inabidi serikali ichukue ghorofa kazaa ziwe ofisi zake kwa walinzi wake.

Kwani Laurent Kabila aliuawa na nani? Kikulacho....
 
Cku sniper ikimparaza hakika cku hiyo hiyo litabomolewa, hii nchi maamuzi ya busara hayafanyiki mpaka kuwe na tukio hatarishi..
 
Na wewe ni mmoja wao hao mazuzu? mbona unamshambulia mtu kutoa maoni yake! Kila mmoja ana uhuru wa kuandika anavyoelewa na kujisikia

si kila mtu anachoongea kinakuwa sahihi. wengine wanaandika pumba tu. hawajui kitu lakini wanajifanya wanajua
 
Cku sniper ikimparaza hakika cku hiyo hiyo litabomolewa, hii nchi maamuzi ya busara hayafanyiki mpaka kuwe na tukio hatarishi..

Sheria ya ardhi inampa raisi kufuta hati. twaweza futa hati na kuchukua jengo, au kumlipa.
 
Lakini kutokana na mabadiliko ya tekinolojia hapa dunia waweza hit ikulu ukiwa popote pale.
Hapo sasa kama wanajari usalama wa Rais wetu inabidi serikali ichukue ghorofa kazaa ziwe ofisi zake kwa walinzi wake.

hakika hapo penye red umenikuna sana. maana wengine wanakurupuka tu na kutoa ushauri ambao sina hakika kama wanashirikisha vizuri ubongo wao
 
Mimi sielewi kabisa watu,huyo jamaa kujenga hilo jumba hakua na niambaya,tena hata ikulu hawakua na wasiwasi wowote,sasa hawa waamerika kwasababu za kuwindwa ndio kuzusha hizo kesi,au ndio kuogopa wasi muhit.


Tunakaribia... Angalia jinsi tunavyojua kutumia TINDIKALI... hakuna iliyofail; ZOOTE zinahit TARGET... Sasa Wakihamia kwenye BUNDUKI hauoni itakuwa ni MOTO?

Angalia wanavyowafyatua hao MATAJIRI wa MERERANI... Watanzania wameneemeka haswa...
Wanajua jinsi ya kutumia silaha hatari...
 
Tangu jengo hilo linaanza kujengwa watu tulijua kiwanja hicho ni mchongo wa ulaji kwani kwa watu wazima miaka yote tangu tumeijua hiyo sehemu ilikua ni uwanja wazi. Kuwashtaki maofisa fulani ni usanii umezoeleka sasa. Kama kweli serikali inamaanisha kupambana na ufisadi wapige hilo jengo chini iwe fundisho pia kwa vigogo wa kiasia wenye kushirikiana na maofisa serikalini kuvunja maadili ya utumishi.
 
Back
Top Bottom