Jpinduzi
Senior Member
- Feb 26, 2011
- 136
- 68
Hati ya talaka ni kweli ilikuweko katika jamii ya kiisraeli mwanamume aliweza kutoa hati ya talaka lakini sio kwa kila jambo hasa ni katika uzinzi ambao tutauongelea zaidi katika agano jipya Yesu anaposema Musa aliwaruhusu kutoa haki ya talaka kwa sababa ya ugumu wa mioyo yenu lakini mambo hayakuwa hivyo tangu mwanzo, Injili ya Mtakatifu Mt. 19:3-12.
Wangapi leo wanakwenda kwa padree au mchungaji na kusema padre\mchungaji mimi leo nimetereza, nimeshindwa mji au ndoa imevunjika. Ni kweli Padre anaweza kushuhudia ndoa na kuitakatifunza lakini hana madaraka ya kusema sakramenti iliyokuwa halali imeisha nadhani watalaamu washeria za kanisa watatusaidia sana hapa. Je hata tunapoamua kuachana kwa nguvu ni kiasi gani cha madhara tunayashuhudia katika familia na jamii nzima?
Kwa ujumla katika Agano la Kale watoto ni wenye thamani kubwa (Zab 127:4-5). Ndiyo maana katika utasa ruksa ya kuoa mwingine ilitolewa kwa ridhaa ya wana ndoa wote na ndiyo maana iliruhusiwa kumridhi ndugu yako endapo amekufa na kumzalia ndugu yako watoto Kumb 25:5-10, na kijana aliyeoa karibuni hakuruhusiwa kwenda vitani kabla hajazaa watoto kumb 20;7 watototo ilikuwa ni dawa ya kifo kwamba hata wazazi wakifa wanaishi kwa njia ya watoto.
Dhamani ya watoto sio katika agano la kale tu ila ni katika kila jamii ulimwenguni, ni bahati mbaya kwamba baadhi ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea zimekuwa na utamaduni wa kukataa uzazi kwa hofu ya hali mbaya ya uchumi lakini dawa ya hali mbaya ya uchumi haina maana tupunguze watu kwani chakula kinapopungua mezani dawa sio kupunguza watu ila kuongeza chakula tujenge mazingira ya kuzisaidia familia kubeba majukumu yake.
Huyo uliyenaye ndie huyo wa kufa na kuzikana acha tamaa na anasa za maisha!!!!!!
Wangapi leo wanakwenda kwa padree au mchungaji na kusema padre\mchungaji mimi leo nimetereza, nimeshindwa mji au ndoa imevunjika. Ni kweli Padre anaweza kushuhudia ndoa na kuitakatifunza lakini hana madaraka ya kusema sakramenti iliyokuwa halali imeisha nadhani watalaamu washeria za kanisa watatusaidia sana hapa. Je hata tunapoamua kuachana kwa nguvu ni kiasi gani cha madhara tunayashuhudia katika familia na jamii nzima?
Kwa ujumla katika Agano la Kale watoto ni wenye thamani kubwa (Zab 127:4-5). Ndiyo maana katika utasa ruksa ya kuoa mwingine ilitolewa kwa ridhaa ya wana ndoa wote na ndiyo maana iliruhusiwa kumridhi ndugu yako endapo amekufa na kumzalia ndugu yako watoto Kumb 25:5-10, na kijana aliyeoa karibuni hakuruhusiwa kwenda vitani kabla hajazaa watoto kumb 20;7 watototo ilikuwa ni dawa ya kifo kwamba hata wazazi wakifa wanaishi kwa njia ya watoto.
Dhamani ya watoto sio katika agano la kale tu ila ni katika kila jamii ulimwenguni, ni bahati mbaya kwamba baadhi ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea zimekuwa na utamaduni wa kukataa uzazi kwa hofu ya hali mbaya ya uchumi lakini dawa ya hali mbaya ya uchumi haina maana tupunguze watu kwani chakula kinapopungua mezani dawa sio kupunguza watu ila kuongeza chakula tujenge mazingira ya kuzisaidia familia kubeba majukumu yake.
Huyo uliyenaye ndie huyo wa kufa na kuzikana acha tamaa na anasa za maisha!!!!!!