Takwimu: Zijue nchi masikini Duniani

ritz kweli we kiza kama ilivyo ccm ,wasomi ndio wanaotuibia karume hakuwa msomi ila alileta maendeleo znz.sasa mwangalie yule mpare profesa maghembe amesaidia nini nchi hii?wewe mwenyewe usomi wako badala ufanye kazi unashinda jf unaandika upuuzi tu

Hapo kwenye jina la Prof. MAGHEMBE yaani huyo ndiyo moja ya wasomi tuliyowaamini kumbe wanayao ya moyoni. Wizi wa maliasili na fedha za umma umehalalishwa na CCM halafu leo Kinana/NAPE hawalioni hilo.

#MABADILIKO NI LAZIMA...
 
Inauma sana, nchi masikini yenye rasilimali nyingi na viongozi MATAJIRI wanaoongoza wananchi MASIKINI
 
Leo katika Gazeti la Majira nimekutana na Repoti hii.
UMOJA wa Mataifa (UN), umeziweka nchi 48 katika kundi la nchi maskini duniani (LDCs), zikiwemo nchi 33 za Afrika, Asia (9), Pacific (5) na Caribbean (1).

Ripoti ya nchi maskini sana duniani ya mwaka 2012 iliyotolewa na Shirika la Biashara na Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNCTAD) kutoka Geneva, nchini Uswisi, ilisema idadi ya watu waliohamia Ulaya kutoka nchi maskini sana (LDCs) iliongezeka.

Ongezeko hilo ni kutoka watu milioni 19 mwaka 2000 hadi milioni 27 mwaka 2010, sawa na asilimia 3.3 ya wakazi wote wa nchi hizo.

Kwa mujibu wa ripoti ya nchi maskini sana duniani ya mwaka 2012, iliyotolewa na UNCTAD, ilisema nchi maskini sana duniani zinatoa asilimia moja ya wahamiaji duniani kote.

Imesema wahamiaji wanne kati ya watano kutoka LDCs, wanaishi katika nchi zinazoendelea (Kusini) na mmoja kati wa watano ndiye anaishi kwenye nchi zilizoendelea (Kaskazini).

“Kiwango cha fedha zinazotumwa na raia waliohamia ng’ambo kwenda katika nchi zao, kiliongezeka mara nane kati ya mwaka 1990 na 2011, kutoka dola bilioni 3.5 hadi bilioni 27.

“Mwaka 2011, kiasi cha fedha zilizotumwa kwenda nchini Tanzania kutoka Uingereza zilikuwa dola milioni 4.5, kutoka Canada milioni 3.2 na kutoka Kenya milioni 2.5,” ilisema taarifa hiyo.

Fedha zilizotumwa kwenda LDCs, zilikuwa mara mbili ya thamani ya uwekezaji wa moja kwa moja (FDI).

Nchi maskini zilizotajwa ni Angola, Benin, Burkina Faso, Burundi, Central African Republic, Chad, Comoros, Congo (DRC), Djibouti, Equatorial Guinea, Eritrea, Ethiopia, Gambia, Guinea, Guinea-Bissau, Lesotho, Liberia, Madagascar na Malawi.

Nyingine ni Mali, Mauritania, Msumbiji, Niger, Rwanda, Sao Tome na Principe, Senegal, Sierra Leone, Somalia, Sudan, Togo, Uganda, Tanzania, Zambia, Afghanistan, Bangladesh, Bhutan, Cambodia, Lao, Myanmar, Nepal, Timor-Leste, Yemen, Caribbean, Haiti,
Kiribati, Samoa, Solomon Islands, Tuvalu na Vanuatu

My Take!
Hivi nchi hii tujiringanishe na Kenya tu ambao hawapo miongoni mwa nchi masikini walichotushinda ni nini kwa upande wa Rasilimali, Hapa naona viongozi waliopo madarakani wanacho cha kujibu kwa nini Tanzania kwa wingi wa Rasilimali tulizonazo bado ni Masikini, Hii ni aibu kubwa sana jamani.

#Du hata zimbabwe inatupita?! Pamoja na kuwasaidia kupata uhuru, hata cameroon wanatupita!
 
iacheni sisiem ipumuwe,iko kwenye mpango mkakati na upepuzi yakinifu wa kuiondoa nchi kwenye hiyo orodha tuendelee kuiamini na kuichagua kila chaguzi
bora "kijani" washa kula wana jipanga kupunguza kula, wakiingia wengine itakua balaa mpaka waje kutosheka ni miaka 50 tena ijayo. tuwavumilie tu wana "jivua gamba" taratiiib wakimaliza mambo yatakuwa shwari.
 
Mbombo Ngafu, Ni ya ngapi? manake wakati tunakuwa tulikuwa tunasoma Tz ya pili kutoka chini kwa umaskini sasa katika 48 ni ya ngapi??
 
yani hii post bora usingeiweka inaniumiza roho yangu ni aibu sana waache kenya watudharau dah sasa kwa hali hii lini tutachange na sisi jamnai mbona hawa viongozi hawana huruma hivi hawaoni aibu wanavyokwenda Nchi za wenzao
 
yani hii post bora usingeiweka inaniumiza roho yangu ni aibu sana waache kenya watudharau dah sasa kwa hali hii lini tutachange na sisi jamnai mbona hawa viongozi hawana huruma hivi hawaoni aibu wanavyokwenda Nchi za wenzao

Wenzio wanaona ujiko wewe unazungumzia haya! Hivi hukumbuki haya maneno ya Nyerere "Mimi napata heshima sana nnapokuwa nchi za nje kwa ajili ya kanchi haka haka"
 
Hiyo EQUATORIAL GUINEA mbona kama sio sawa. Nilisoma report moja inadai hao jamaa ni miongoni mwa mTaifa lililoko ktk cnhi 5 bora kwa utajiri barani Africa.
 
fresh hi itatusaidia kujitangaza kimataifa zaidi hivyo kuvutia wawekezaji..bravo ccm
 
Nasikitika kuona hata Rwanda haipo humu wakati wamepigana wao kwa wao wakaharibu mali, watu, miundombinu juzi tu hapo. Leo hii wao siyo masikini zaidi duniani!! Poor Tanzania Leaders!! Poor CCM, Poor JK
 
Nasikitika kuona hata Rwanda haipo humu wakati wamepigana wao kwa wao wakaharibu mali, watu, miundombinu juzi tu hapo. Leo hii wao siyo masikini zaidi duniani!! Poor Tanzania Leaders!! Poor CCM, Poor JK

Rwanda wamo Mkuu, pitia vizuri hii orodha. Viongozi wa Serikali yetu hawana kesi ya kujibu kwa vile walishasema 'hawajui kwa nini Watanzania ni maskini', waliosema wanafahamika, hata wao wanashangaa ni kwa nini wanaendelea kuwa madarakani.
 
Mwajiliwa aliyelifilisi kampuni la mwajili wake afanyiwe nini? Kuachishwa kazi peke yake hakutoshi, afanyiwe nini niambieni wana jf.
 
Wazungu ni watu wa ajabu sana,ok fine sisi ni maskini kwanini wao kila kukicha wanamiminika kuja afrika kutafuta fursa za uwekezaji? Kwanini wanatumia kila aina ya mbinu kutufanya sisi kushindwa kufanya mambo yetu wenyewe mpaka wao wawepo?.Wao wenyewe ndio wanatupiganisha sisi kwa sisi,wanatufanya tushabikie mambo yao ilihali tukiacha kufanya kazi kwa bidii.Ebu tujiulize nini mantiki ya hoja hii? Hivi inaingia kabisa akilini kwamba sisi ni maskini wale ni matajiri alafu wale ambao ni matajiri wanatutumia sisi ambao ni maskini ili wao waendelee kuwa matajiri alafu wanakuja kutuambia ninyi ni maskini sana kwa hiyo tufanyeje sasa?.Ndio maana tunaanza kulaumiana sisi kwa sisi alafu wao wanafurahi kwelix2 na kutuona sisi ni mazuzu na ujinga uliokithiri,maana kama tungelikuwa welevu tungeliwakataa ili tutumie fursa wanazitumia wao hapa Afrika/Tanzania ili nasi siku moja tuwekwe kwenye rekodi zao.Kwa mtizamo wangu si kweli kwamba sisi ni maskini bali wao ni maskini ndio maana kila kukicha wanakuja kuchukua mali zetu ili wao wawe matajiri.
 
Wanaotazama kutoka nje wanaona uchumi wetu unafanya vizuri. Hii nimeikuta The Independent


Economic growth stirs hope in Africa
Over the next five years, the continent will expand faster than any other

While ministers in Europe try to hold together crumbling economies, a success story has been quietly emerging to the south. Africa is experiencing its longest income boom for 30 years, with gross domestic product growth rates averaging about 5 per cent annually over the past decade. Even this year, as markets elsewhere collapse, the continent's income is projected to increase by around 4.5 per cent.


Africa will have the world's fastest-growing economy during the next five years of any continent, according to the International Monetary Fund.
Its forecasts also show that seven of the world's 10 fastest-growing economies will be African, with Ethiopia, Mozambique, Tanzania, Congo, Ghana, Zambia and Nigeria expected to expand by more than 6 per cent a year until 2015.

The world is starting to take notice: trade between Africa and the rest of the globe increased by 200 per cent between 2000 and 2011. As well as the usual exports of oil, natural gas and minerals, the sale of African-manufactured goods is also increasing. Over the past ten years, African manufactured output has doubled.


Zambia is one of the continent's most promising economies, growing at 7.6 per cent in 2010 and 6.6 per cent in 2011. Thanks to the technology boom, its supply of copper, which now accounts for almost half its exports, is highly sought after. Though it is still among the poorest in the world – it is ranked 164 out of the 187 countries on the UN Human Development Index – there are signs that its economic success is starting to translate into better lives for its citizens. By 2009, the country had full primary school enrolment, up from 80 per cent in 1990, and the latest figures show a decline in the infant mortality rate to 86 per 1,000 live births in 2009 from 88 in 2008.


Marcelo Giugale, the director of the World Bank's poverty reduction programme for Africa, has been watching how the continent's economic successes impact on its poorest people and is cautiously optimistic. "Sustained growth is necessary but not sufficient on its own to have an impact on poverty", he said. "You can have growth for a long time and it will help only a few people. We have been lucky that growth has been accompanied by poverty reduction. Not as much as you'd hope, but still. We don't have continental numbers, but we do have individual countries that show a reduction in poverty, especially extreme poverty.

Endelea kusoma HAPA
 
Mungu aliipenda sana Tanzania akaipa utajiri wa kila aina ambao kama ungetumika vilivyo, wananchi wake wasingehangaika hata na utafutaji kwani raslimali tulizonazo zingetosha kabisa kila mmoja wetu kula na kulala wala asishughulike na kazi nyingine yoyote, kwa kuwa ardhi yote imejaa utajiri wa madini, mbuga, maziwa makubwa,mito,nk. Mimi naamini kama kuna siku ya kusimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mwenyezi Mungu, basi wote ambao walipewa mamlaka ya kuwagawia watu wa Mungu kile alichotoa kwa nchi hii, wana kesi ya kujibu. Nawaomba wahusika wafanye hima kurekebisha mambo kabla ya siku hiyo ya kutisha haijafika. Amina.
 
Back
Top Bottom