GE2025 TAKUKURU yakamata wajumbe wa UWT kwa madai ya rushwa

GE2025 TAKUKURU yakamata wajumbe wa UWT kwa madai ya rushwa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
2,439
Reaction score
6,692
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Geita, imewakamata wajumbe wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Nyankumbu Jimbo la Geita mjini walionekana katika picha mjongeo wakigawana rushwa katika mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM huku taasisi hiyo ikiendelea na uchunguzi kwa watia nia ngazi ya ubunge na udiwani wanaodaiwa kusambaza rushwa ya fedha kwa wajumbe ili wapate nafasi ya kuchaguliwa ili kugombea nafasi za ubunge na udiwani katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Tukio hili lilitokea tarehe 2 Agosti 2025 baada ya picha za video kuonyesha wajumbe wakigawana fedha kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya TAKUKURU, baada ya tukio hilo kusambaa, ofisi ya mkoa ilichukua hatua ya haraka kwa kuwatambua na kuwakamata wajumbe waliokuwa wakionekana kwenye picha hizo na kwamba Inadaiwa kuwa vitendo hivyo vilifanyika mara baada ya zoezi la kuwanadi wagombea ubunge kukamilika.

Katika tukio jingine, tarehe 4 Agosti 2025, TAKUKURU ilipokea taarifa kuwa chakula na vinywaji vilitolewa kwa wajumbe siku ya upigaji kura za maoni katika jimbo la Chato Kaskazini, picha za tukio hilo zilisambazwa pia kwenye mitandao ya kijamii na kusababisha TAKUKURU kuanza msako na kuwakamata washukiwa kwa ajili ya mahojiano.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Geita James Ruge, amesema kuwa kutokana na matukio haya na mengine, ofisi imeanzisha uchunguzi unaoelekea kukamilika, ikiwa ni hatua ya kukusanya ushahidi ili kuthibitisha tuhuma za rushwa dhidi ya wahusika.

 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Geita, imewakamata wajumbe wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Nyankumbu Jimbo la Geita mjini walionekana katika picha mjongeo wakigawana rushwa katika mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM huku taasisi hiyo ikiendelea na uchunguzi kwa watia nia ngazi ya ubunge na udiwani wanaodaiwa kusambaza rushwa ya fedha kwa wajumbe ili wapate nafasi ya kuchaguliwa ili kugombea nafasi za ubunge na udiwani katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Tukio hili lilitokea tarehe 2 Agosti 2025 baada ya picha za video kuonyesha wajumbe wakigawana fedha kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya TAKUKURU, baada ya tukio hilo kusambaa, ofisi ya mkoa ilichukua hatua ya haraka kwa kuwatambua na kuwakamata wajumbe waliokuwa wakionekana kwenye picha hizo na kwamba Inadaiwa kuwa vitendo hivyo vilifanyika mara baada ya zoezi la kuwanadi wagombea ubunge kukamilika.

Katika tukio jingine, tarehe 4 Agosti 2025, TAKUKURU ilipokea taarifa kuwa chakula na vinywaji vilitolewa kwa wajumbe siku ya upigaji kura za maoni katika jimbo la Chato Kaskazini, picha za tukio hilo zilisambazwa pia kwenye mitandao ya kijamii na kusababisha TAKUKURU kuanza msako na kuwakamata washukiwa kwa ajili ya mahojiano.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Geita James Ruge, amesema kuwa kutokana na matukio haya na mengine, ofisi imeanzisha uchunguzi unaoelekea kukamilika, ikiwa ni hatua ya kukusanya ushahidi ili kuthibitisha tuhuma za rushwa dhidi ya wahusika.

 
Aise! Nimecheka sana,mgawaji kala chake mapema sana! Haaaaa
 
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Geita James Ruge, amesema kuwa kutokana na matukio haya na mengine, ofisi imeanzisha uchunguzi unaoelekea kukamilika
Utahitimishwa na Mwenyekeiti
 
Naikumbuka ile tamthilia ya days of our lives,enzi hizo CTN TELEVISION TV ndy zinaanzaanzaa

Ova
 
Hakuna intellegensia yeyote mpaka waone trending clip kama hizo ndo wakamate wakati harufu za rushwa ni nyingi.

mbaya zaidi wanakamata madagaa tu
 
Back
Top Bottom