Taifa teule na mataifa

Mkuu asante sana "" Umepita vyema kabisa..."" Sina mashaka na ma bandiko yako "".... acha niendelee kujifunza zaidi ""..
 
Hapa kuna mkanganyiko mkubwa isije kuwa tunadhulumiwa ukweli bila kujua
sio isije kuwa " tuna dhulumiwa kweli mkuu" "tafiti nyingi za kihistoria zinaonyesha kuwa "" watu weusi ndio watu wakale zaidi na ndio watu ambao walipaswa kuwa na dini kubwa zenye ushawishi kwenye huu ulimwengu""... historia inasema nimrod alikuwa mtu mweusi " lakini mbona haushangai ulimwengu wa sasa jinsi unavyo mzungumzia kuwa alikuwa ni mtu mweupe ""....
 
Na kama kuna watu wanamkataa yesu kwa nguvu zote Duniani basi ni waisrael wale Jewish. Sijui kwanini bado wanaqualify kuwa taifa teule then watu wa pale Mbeya waliokoka mkoa mzima wanakuwa watu wa mataifa? Inanivuruga kichwa hii!

Its injustice!
Ha hahaa hahaa
 
Sijakuelewa kabisa..afu ni vyema ukafafanua kuliko kuniqotia mlolongo wa maandishi haya mkuu.

Fafanua sasa nikuelewe!
hahahaa ..analeta mahubiri " mpaka kwenye mambo yanayotaka kufikirisha bongo kwaajili ya kufanya uchambuzi uwe na mantiki
 
inawezekana waisrael wangemkubali Kristo dunia au watu wa mataifa wasingemjua kwa nafasi aliyo nayo.
dini kwa ujumla wake kwa kadri ya mapokeo ina mambo mengi kwa kadri ya anayetupokelesha kwa kuwa huwa pia inaweza kubeba maslahi binafsi kwa wapokeaji.
lakini ninachojifunza kwa watu hawa ni mambo makubwa mawili.
  1. utuzaji wao wa taarifa- inawezekana hakuna taifa litunzalo taarifa kwa umakini kama hawa jamaa kwa kadri ya vizazi vyao toka ibrahimu mpaka sasa na wamefanikiwa kuyaweka kwenye maandishi yakisomwa dunia nzima. pamoja maandishi yalizinduliwa misri ambako hawa jamaa walikuwa watumwa, lakini walitumia fursa vizuri kuzidi wa misri wenyewe.
  2. kiingine shida na kutumikishwa kwa muda mrefu na wamisri (kama tunavyoona baadhi ya kazi zao za ujenzi) zimewafanya kuwa na uwezo mkubwa wa kupambana na mazingira wakitumia resource chache kuleta mafanikio makubwa. iko mifano mingi lakini wengi tunajua taifa hili lilivyo na mvua chache lakini linaongoza kwa kilimo cha matunda na mbogamboga wakitumia zaidi kwa uangalifu mvua chache zinazonyesha ka kukinga maji na sehemu zingine za milima zinatumika kama matenki ya kuhifadhia maji na kushuka bondeni(kwa kadri ya simulizi).
naogopa sana kuwachambua kwa kuwa wanahusika na imani nilionayo na muda si mrefu nimetoka kwenye jumuiya na somo la leo limetoka 2timotheo 4:1-8 nikitutaka tuwaubirie watu wa mataifa injili.
hivyo kwangu mimi cha kujifunza ni kwamba:-
  1. katika shida zetu na masumbufu yetu tujitahidi kutafuta njia ya kuyatatua kwa urahisi na kwa akili zote. ( mfano mzuri VICOBA ilianzia niger baada ya shida za kinamama kutelekezwa na waume zao kwa ulevi na pengine na umalaya kulisababisha wao kuanzisha vikundi hivi, lakini leo wazungu walishavichukua vikawa vyao na jina la kibantu la vikundi hivi likapotezwa na sasa ni wao na hawakumbuki hata kuwalipa haki miliki kwa waanzishaji.)
  2. tujifunze kutunza kumbukumbu zetu vizuri ili siku zijazo tuweze kuzielezea vizuri haiingii akilini eti ziwa victoria pamoja na mlima wake wa bismarock eti ulivumbuliwa na mzungu waswahili walikuwa hawauoni?
  3. tutumie muda na maarifa kutambulisha kile tulichonacho na tulichofanya badala ya muda mwingi kuzungumzia udhaifu mfano hakuna ubishi mpaka sasa binadamu wa kwanza aliishi tanzania hvyo tungeweza kusema taifa la tanania ni taifa teule na wale wengine ni watu wa mataifa.
yapo mengi na inawezekana nimetoka nje ya mada lakini nimeona mchango huu waweza faa kwa kadri nilivyoona leo yafaa kuchangia.
 
weka hicho kifungu cha methali ilipotajwa china
 
weka hicho kifungu cha methali ilipotajwa china
Jifunze kufuatilia mjadala wote hatua kwa hatua kabla hujaamua kuchangia... Ungekuwa umefanya hivyo usingekuja na swali lako hili
 
Mimi na zungumzia imani yangu unless tukubaliane kuwa iko Taurati, injili, Zaburi, Methali nk ambazo ni za Kikristo tu na nyingine za Kiislam tu. Lakini kama Abraham, Musa, Daudi, Bwana Yesu akiwa hapa duniani, kuwa hizi ni nafsi mojamoja, basi wale wa imani ya Kikristo watakuwa wanafanya makosa wakisema Yesu Kristo ndiye Issa SA. Sio Kweli kwa mujibu wa Biblia.

Yesu Kristo hakuacha kusema kwa uwazi kabisa ni amri/utaratibu gani wanadamu wanapaswa wafanye ili kumfuata yeye. Lazima kama Mkristo ujue kuwa Bwana Yesu alikuwa Mungu kweli na pia Binadamu Kweli. Hivyo alipokuwa anaelekeza ni taratibu gani zitumike ili kuwa mfuasi wake alikuwa akitimiza majukumu mawili kwa wakati mmoja, yaani lile la Kiungu na lile la kinabii mwanadamu.

Hawa manabii wengine wote tunao wajua walikuwa wanatimiza majukumu waliotumwa na Mungu/ Bwana Yesu kwa wanadamu ili hatimaye wanadamu waweze kufika kwa Mungu wao mbinguni na wasiishie jehanamu/motoni.

Kwa mkristo anaye ijua Biblia vizuri kumuambia Mtume Muhamad SA ni mtume/ nabii wa Mungu kamwe hawezi kukubali. Maana atakuuliza, je alibatizwa kwa maji na Roho? Jibu ni hapana. Na kama ni hapa wala huyo hamjui Bwana Yesu/Mungu si mmoja kati ya wale wa Yesu. Kusema unamjua Bwana Yesu wakati hufuati yale maagizo aliyokupa ili uwe mfuasi wake ni kujidanganya kwa ajili ya kujifariji kibinadamu. Kweli Mungu ni mmoja kwa maana wote tunao amini katika umbaji twa amini yeye ndio muumba wa vyote. Lakini katika ufuasi/kumfuata Mungu hakika hatumfuati Mungu mmoja. Wako waliopata neema ya kumfuta Mungu wa Kweli na wako ambao hawajaipata hiyo neema, Wamepotea/wamepotezwa lakini hawajui.


Kuhusu Taifa teule la Mungu ni kweli huu ndio utaratibu wa Mungu alio jiwekea ambao unajidhihirisha kwetu hata kwa kutumia logic ya akili za kibinadamu.

Umeeleza Vizuri kuhusu Abraham kuchaguliwa kuwa uzao wake ndio utaunda hilo taifa teule la Mungu . Nimesha sema mara kadhaa humu ni taifa teule kwa maana ya kuwa Mungu ageliwatumia wazawa/baadhi ya watu kutoka vizazi hivyo kwa ajili ya kuwa humbiria/kutoa ujumbe/ unabii uhusuo mambo ya Mungu na jinsi gani ya kumtii na kumtumikia.

Utaona alimchagua Abraham kwanza, katika watoto wa Abraham akachaguliwa Isihaka, katika watoto wa Isihaka akachaguliwa Yakobo nk ,nk, Mwishowe alichaguliwa Mfalme Daudi ambaye hatimaye kwa kupitia uzao wake Mungu mwenyewe alikuja hapa duniani kama Emanuel ambaye ni Bwana Yesu.

Baada ya Bwana Yesu Kuja hapa duniani wafuasi wake, yaani wale walio mpokea yeye kuwa Bwana na Mwokozi wao, nao kwa kupitia YESU wamekua/wamefanywa kuwa taifa teule la Mungu. Na ndio maana Mungu Mwana au nafsi ya Mungu ya uana/ubinadamu ilitia timu yenyewe hapa duniani kufanya kazi hiyo.

Kuhusu dini ya kiyahudi ni kweli kuwa asilimia kubwa ya Wayahudi, Mungu kawanyima hiyo neema ya kumkubali na kumtambua akiwa hapa duniani. Hata hivyo Tora yao imewawekea wazi kabisa kupitia manabii ambao ni ndugu kati yao wanadamu, kuwa atakuja Masihi/Bwana Yesu kuchukua pahala pa Mfalme Daudi. Wao wakaishia kufikiria mambo ya kimwili zaidi na wakasahau ya Kiroho. Wakadhania Masihi angewashindia vita hivi vya adui wa Kimwili,. Kumbe Masihi ni kweli kawashindia ile vita ya kiroho ambayo ni kupambana na dhambi na kushinda adhabu yake ya kifo cha kiroho na kimwili. Ukisha shinda vita vya kiroho ndio umemshinda shetani, wafuasi wake na kazi zao zote.

Utaona kuwa baada ya Bwana Yesu/Mungu kuja hapa duniani na kuwa fanya wafuasi wake walio mpokea kuwa taifa teule, aliwapa wale wafuasi baraka za kwenda kuuhubiri ulimwengu mzima habari njema za Wokovu wa Mungu kwa mwanadamu. Pia akawapa msaidizi Roho Mtakatifu ambayo ni nafsi ya Mungu ya tatu kuwa ongoza.

Yeyote aliye kuja na Imani ya Kiislam alikuwa makini kwa kujinasibisha kwa Mungu pale aliposema tunamkubali Nabii Issa SA (kwa mujibu wao Bwana Yesu/Issa bin Mariam) na mafundisho yake na akaenda mbali kwa kutengeneza mazingira ya kuwa aminisha wanadamu kuwa Mungu/Bwana Yesu ndio Nabiii Issa bin Mariamu ndiye Yesu. Wakati kama wewe ni mkristo uliye pataa neema ya Mungu ya kulijua neno la uzima la Mungu/Biblia kinachotajwa na wenzetu wa Uislam kusuhu Bwana Yesu eti ndiye Nabii Issa SA sio kweli. Na Mkristo kusema Nabii Issa wa Quran Tukufu ndiye Bwana Yesu wa Biblia anatenda dhambi ya uongo na anapaswa kutubu.




 
Mkuu nakuunga mkono but Issa siyo yesu jaribu kuelewa.
 
Mkuu nakuunga mkono but Issa siyo yesu jaribu kuelewa.
Nabii Issa ni Mtume wa Mungu alyezaliwa na Maryam Bint Imran ..Nabii Issa hakuzaliwa hana Baba na huu ndo Muujiza mkubwa juu ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu..Nabii Issa alikuja na ujumbe wa kumuabudu Mungu aliye mmoja , kusali na kutoa zaka pamoja na kufanya yaliyo mema hakuuliwa wala hakusulubiwa kwa mujibu wa imani yangu ya Uislam.


Naomba nieleweshe juu ya Yesu.
 

Mkuu Zitto Junior, naomba nikurekebishe mahali

Ahadi za Mungu kwa wana wa Israeli hazifutiki kamwe mpaka mwisho wa dahari, hilo ni agano la MUNGU na Ibrahimu hili ni agano la milele na milele

YEREMIA - SURA YA 31
1 Wakati huo, asema Bwana, nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Israeli, nao watakuwa watu wangu.
2 Bwana asema hivi, Watu wale walioachwa na upanga walipata neema jangwani; yaani, Israeli, hapo nilipokwenda kumstarehesha.
3 Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.


Kuhusu Waisraeli kuwakataa mitume na Manabii mtume Paulo alishasema sababu na chanzo chao

25 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.
27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao. (isaya 27:9) kuijua hiyo ahadi
28 Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.
soma warumi 11 sura nzima

Kwa maelezo zaidi juu ya hawa watu

soma Isaya na Yeremia
 

Alikufa au hakufa? Na kama alikufa alifufuka au hakufufuka. Kama hakufufuka yuko wapi? Maana wafu wako kaburini wakisubiria ile siku ya mwisho wa dunia yaani siku ya hukumu. Kiranja wa hiyo siku ni Bwana Yesu mwenyewe.

Bwana Yesu aliteswa, alisulubiwa, akafa, akazikwa na siku ya tatu akafufuka. Ameshinda kifo na dhambi, hatimaye akapaa akishudiwa na watu kwenda mbinguni.
 

Yesu ni kwetu wakristo, nyie ndio mnamwita nabii Issa
 
inawezekana waisrael wangemkubali Kristo dunia au watu wa mataifa wasingemjua kwa nafasi aliyo nayo.

28 Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.

Bibilia haijasaza kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…