Taifa stars vs Mozambique.

Taifa stars vs Mozambique.

Mkuu, achana na mpira wa Bongo!....mpira wa Bongo ni presure tu! usipoangalia utapata ugonjwa wa moyo.
Tanzania hatuwezi soccer ya kimataifa na haitakuja kutokea....labda baada ya miaka 500. FULL STOP...Utaki unaacha

mkuu yani sibet tena kwa taifa stars. Labda wabadilike japo ni ndoto.
 
Mkuu, inakera sana hii team, ningeandika kama yalivyokuwa moyoni ningekula ban!!
Mie mwenzio nilishajiapiza kitambo sana haitakujatokea mimi nikapenda soccer la Bongo! hata pale Taifa sijawahi ingia.
Yaani Arsenal initese na soccer la bongo linitese? Jibu ni hapana....mateso ninayopata na Arsenal ya England yananitosha
 
Yani nikwamba tumefungwa hakuna cha kusema wamejitahidi!!
 
Nilijua tu hawa simba hawafiki popote wasubiri kipigo kwa moroco na lvory cost wafumue kikosi tena
 
Tanzania tumetolewa nje ya michuano kwa mikwaju ya penat 7kwa 8 waliopata msumbiji
 
mkuu kama ni kujifunza basi tungekua hata kwenye top50 kwenye rank ya dunia,tutafute kitu kingine cha kufanya tu tunashiriki na sio kushindana

Kama ingekwa ni kushindwa mara moja moja tu, ningekubali na kuwa mzalendo, lakini tangu nipate fahamu miili yetu imejaa makovu. Tusubiri visngizio - matayarisho duni, chakula kibaya, hali ya hewa, wachwezaji hawakupewa posho.....Sasa tusubiri tuje kufungwa petu.

Tuanzishe mmashindano ya Kiduku, mdundiko katika ngazi ya shina, wadi, wilaya, mkoa hadi Taifa, lakini iwe sisi kwa sisi, tukiwaita hata Warundi watatushinda. Kimataifa viongozi wetu wanaweza kushindana kwa rushwa na ubadhir¡fu wa mali ya umma, nina hakika kila mwaka wanabeba kombe .
 
1.kaseja 2.chapombe 3. Maftaa 4.yondan 5.nyoso 6.kazimoto 7. Ngasa 8.boban 9.boko 10. Jonas 11.samata ,. Hii ni timu ya taifa au nimekosea jina? Kwa mwendo huu tz hata malaika aje kutufundisha hatuwezi fika popote
 
Acheni kutoka mapovu, vijana wamejitahidi unafikiri kufika penati masihara, nakumbuka (Msumbiji) Tico tico alitutoa nishai na Maximo wetu Taifa kipindi kile si bora sa hivi tumetolewa kwenye penati.
 
1.kaseja 2.chapombe 3. Maftaa 4.yondan 5.nyoso 6.kazimoto 7. Ngasa 8.boban 9.boko 10. Jonas 11.samata ,. Hii ni timu ya taifa au nimekosea jina? Kwa mwendo huu tz hata malaika aje kutufundisha hatuwezi fika popote
Hao ndo bora kwa wachezaji wa Tanzania tulionao, ebu niambie wewe ungekuwa kocha nani ungemuita timu ya Taifa, halafu unajaribu kutaja wanaotokea Simba makusudi ili ujiridhishe kwamba iliyofungwa ni Simba, kwa taarifa yako iliyofungwa ni timu ya Taifa na kwa nini hujawataja Aggrey Morris, Erasto Nyoni, Frank Domayo, Thomas Ulimwengu waliocheza badala yake unataja Boko, Nyoso, Maftah, Mkude na Boban ambao hata hawakuanza hapo si kutafuta uchokozi.

Ngoja Kagame ianza kocha achukue wengine kutoka Yanga na kelele zote hizi zitaisha maana mapovu yote haya ni kwamba Yanga hawana mchezaji timu ya Taifa wala hakuna kingine.
 
dah! kisicho liziki hakiliki: vijana wamejitahidi; uzembe ulifanyika ktk mechi ya awali.
 
Unachukua wachezaji wote toka litimu lilipigwa 12 unategemea nini,. Tuache fitna tz soccer litasonga mbele,. Kibabu kipo golini
halafu unachukua na mchezaji mmoja toka kwenye litimu kimeo limepigwa 5-0 kwenye ligi na kuwa litimu pekee kulambwa 5 na mnyama msimu huu!!
 
Mkuu ninahasira hapa acha tu, niliamua kuandika hivyo kuhofia ban!! Timu haifanyi maandalizi ya kutosha, hapo hapo inajaza wavuta bangi, ukiangalia msingi wa soka nchini unakosa wapi/vipi tunatengeza vipaji vya kuweza kushindana. Hatuna viongozi wabunifu, tunao viongozi wanaoongoza kwa kuiga, mazoea na kutaka kujitajirisha bila kujali wananchi kupitia viingilio wanatutengenezea maradhi na kutupunguzia siku za kuishi.
Hili la kutolewa kila mashindano imeshakuwa jadi, system nzima ya nchi yetu inahitaji Total overhaul kuanzia magogoni hadi kwa mwenyekiti wa mtaa. Nasema hivyo kwa sababu M'kiti wa mtaa wanajua wananchi wanaokaa nao, hivyo hata viwanja vya kufanyia mazoezi wanapiga bei, hivyo hivyo pale magogoni kama mzee mzima anapenda mchezo wa soka, anashindwa nini kusema nahitaji kuona mwezi mmoja kwa mwaka kwa ajili ya michezo, inawezekana hizo week nne zikagawanywa kila miezi mitatu mashindano yafanyike kwenye shule na kuna watu wameajiriwa, hakuna gharama za kuendesha ni amri tu.

thats right kaka,tatizo ni system,hata tukimleta wenger,fagasoni,morinyo,etc hakuna cha maana sana kitakachofanyika tutaendelea kulaumu makocha kila siku kwa taifa star whatever is exellent
 
Huu ni ujinga kila siku 2nachapwa why hi timu isivunjwe tusiwe na tim.Kod ze2 zinapotea kw kuwekeza kwenye unprofitable sports shit! Ujinga huu
 
Mie mwenzio nilishajiapiza kitambo sana haitakujatokea mimi nikapenda soccer la Bongo! hata pale Taifa sijawahi ingia.
Yaani Arsenal initese na soccer la bongo linitese? Jibu ni hapana....mateso ninayopata na Arsenal ya England yananitosha

kama umechangia kwenye hii thread, sina shaka kuwa nawe ni mfuatiliaji mzuri tu wa soka bongo ndo maana ulijua kuwa stars inacheza leo, ila ndo utanzania tena, timu ikishinda mnaipenda, ikishindwa mnaikana tena kwa kauli tete!!
 
kama umechangia kwenye hii thread, sina shaka kuwa nawe ni mfuatiliaji mzuri tu wa soka bongo ndo maana ulijua kuwa stars inacheza leo, ila ndo utanzania tena, timu ikishinda mnaipenda, ikishindwa mnaikana tena kwa kauli tete!!
Mkuu nashukuru kwa kuliona hilo, hawa washabiki wa Ndala wanafiki sana kama wazee wao kina Yusuf Mzimba na Ibrahim Akilimali, juzi hapa stars imeshinda ikaitwa timu ya Taifa leo imetolewa inaitwa Simba wananiudhi kweli, ndo maana walipigwa mkono.
 
halafu unachukua na mchezaji mmoja toka kwenye litimu kimeo limepigwa 5-0 kwenye ligi na kuwa litimu pekee kulambwa 5 na mnyama msimu huu!!

daa ko kaseja anazidi kua bora kila kukicha toka kupigwa 12 kule sudan hadi 8,. Anajitaidi sana
 
Back
Top Bottom