- Thread starter
- #41
Swali,Kwanini makazi yao yanaitwa illegal settlements km ni azimio la UN?Israel taifa haram? Hmm hiyo hoja ngumu.
Zingatia:
1. Israel (ile ya leo, si ile ya Biblia) ni nchi ya pekee iliyoanzishwa kwa azimio la Umoja wa Mataifa.
2. Mfano nchi kama Kenya ilianzishwa kwa hiari ya Mwingereza, Tanganyika ilianzishwa kwa hiari ya Mjerumani halafu Mwingereza, nchi nyingi za Afrika vilevile.
Sioni mantiki kuita nchi yenye msingi katika haki ya kimataifa "Haram"
Utawala wake juu ya Ukingo wa Magharibi wa Yordani (West Bank) ni kitu kingine. Nchi nyingi hautambui.
Majadiliano kuhusu Wapalestina miaka mamia iliyopita ni bure. Palestina kama taifa walianzishwa pamoja na Israeli katika azimio lilelile la Umoja wa Mataifa.
Miaka 100 iliyopita hakuna Palestine, ilikuwa wilaya ya kusini ya jimbo la Syria ya Uturuki (tusema: Milki ya OSmani - Ottoman Empire) tu.