So sad huwa najiuliza tulipoteza vipaji vingapi paleAsante mishanajr.hili tukio ccm walicheza hiyo miaka na kuchoma shule ilikuwa kipindi ya viama vingi hili kufanya propaganda ccm walichoma hili kusingizia wapinzani lakini Mungu yupo.nimemaliza shule kubwa hapo kipindi hicho.
swissme
Siyo kila kitu ni siasa mkuu. Siamini kama CCM ni waovu kiasi hiki mpaka wachome bweni la wasichana kisa eti wasingiziwe wapinzani. Kuna conspiracy theories zingine huwa nakubaliana nazo lakini hii ya kwako hapana.Asante mishanajr.hili tukio ccm walicheza hiyo miaka na kuchoma shule ilikuwa kipindi ya viama vingi hili kufanya propaganda ccm walichoma hili kusingizia wapinzani lakini Mungu yupo.nimemaliza shule kubwa hapo kipindi hicho.
swissme
The very night has a story to tell and may be one day the truth will be revealedSiyo kila kitu ni siasa mkuu. Siamini kama CCM ni waovu kiasi hiki mpaka wachome bweni la wasichana kisa eti wasingiziwe wapinzani. Kuna conspiracy theories zingine huwa nakubaliana nazo lakini hii ya kwako hapana.
Kuna makala ndefu ilitoka kwenye gazeti ikihusisha tukio hili na mambo ya mauzauza na kwamba eti mabinti wale waliendelea kuonekana wakiwa wanalia. Shule ilibidi ifungwe tena hata baada ya kufunguliwa kutokana na mauzauza hayo.
Ukifunikwa sana na chuki za kisiasa kila kitu kwako kinakuwa ni siasa. Hata ukijamba utasingizia chama kingine kimekutega. Tuache urazini ujipambanue!
Inauma sana hasa issue ya wanafunzi. Imetimia miaka 22 sasa. Hao wanafunzi kwasasa wangekuwa na around miaka 36 - 40 hivi ambapo ingekuwa faida kubwa kwa familia zao na taifa kwa ujumla.
Hao wazazi wawili imeniuma pia nikakumbuka 2007 nilikuwa nasafiri kutoka Dar kwenda dom sasa hiyo safari dada yangu hakuitaka kabisa kwa siku hiyo tulichukua takriban saa 3 tukiongea yeye hataki niende na mimi nataka kwenda mpaka akashindwa nikaondoka. Ile kufika Kibamba tu ikatokea ajali pale darajani ambapo tulinusurika wote hakuna safari iliyoendelea maana gari iluyokuwa mbele yetu ndio ilipata ajali na kuziba njia na sisi kwenda karibu na ile gari ambambo tungekuwa na speed walao 70 ingekuwa balaa zaidi. Narudi kwa sister anakwambia unapoondoka kwa kinyongo hutokea haya.
Sasa navuta hisia kwa hawa mabinti ambao waliondoka kwa kinyongo huku Mungu akiwakataza wasiende lakini bila kujua wazazi wakalazimisha kwa nia nzuri tu. Kiukweli kujinyonga kwao waliona hakuna namna ya kuishi tena bila wanao wawili tena their only.
R.I.P All
Duu mmh...! Kwahiyo hapo ni wazi kabisa kulikuwa na clear channels za tahadhari toka kwa Kitale, na hata kule kukataa wasisafiri siku ile na matukio yote yaliyofuatia ilikuwa ni mwendelezo huo huo wa tahadhari lakini hakuna aliyeweza kuzing'amua kwa hakikamshana jr kuna siku nilikuwa naangalia kipindi cha Mkasi. Mgeni alikuwa mchekeshaji Kitale, rafiki mkubwa wa marehemu Sharo milionea,mchekeshaji mwingine marehemu. Hawa walikuwa marafiki wakubwa wakishirikiana kila kitu. Siku ya kifo cha Sharo alimuomba Kitale waende wote Tanga na kwa kawaida Kitale asingekataa ila siku hio alikataa akimsihi Sharo waende kesho yake. Sharo akaamua kuondoka mwenyewe kuanzia anaondoka Kitale akapoteza amani na raha hadi akajisikia mgonjwa akaenda kulala mapena. Alianza kuota ndoto za ajabu kuhusu rafiki yake, kilichomuamsha ndotoni ni simu ya Kitale mpigaji akiwa mtu mwingine akimuarifu Sharo kapata ajali amefariki.
Ebana Mshana umenena kweli, mie miaka imepita, kipindi fulani niliteseka kwa siku 2,moyo unalipukaa unamiaaa kitu kinanikaba kooni machozi yanatoka nakua na hali mbaya nagala galaa kama haitoshi wasiwasi unaniizidi, naulizwa umepatwa na nn lakini sijui nina nn, nawajibu sijielewi ila siko fresh wengine wakasema basi kuna watu wanakufanyia ubaya kuwa makini, mwingine akasema huenda ni dalili za presha, wengine wakasema basi hao watu wanakusengenya. Lakini siku 3 hali yangu ikawa mbaya zaidi mara simu nikapigiwa na baba ananiambia anaumwa, fastaa nikasafiri kwenda kumuona heee nimefika mtu kazidiwa basi tukamuuguza mwisho akafariki.Ni alfajiri nyingine tena kunapambazuka....
Kwanza kwa huzuni kubwa naomba nitoe pole nyingi kwa ndugu na jamaa wa mama aliyeuliwa kikatili usiku wa kuamkia jana kwenye uwanja wa transforma chalinze! Mpaka juzi saa tano usiku alikuwa hai nyumbani kwake (si mbali sana na eneo alipouliwa) lakini asubuhi ya jana alikutwa uwanjani hapo akiwa kafa kifo cha kikatili na mateso makubwa. .mwili unaonyesha alibakwa na watu zaidi ya wawili kuvunjwa mikono kunyongwa na hatimaye kutobolewa macho RIP [emoji144] [emoji24] [emoji25]
===============================
Tumejifunza katika masomo yaliyotangulia kuhusu mlango wa sita/mlango wa machale, mara nyingi ikija kama sauti ya kutoa tahadhari au moyo kupasua au kukosa pumzi kila ukikumbuka jambo husika! Ukiwa na fikra yakinifu lazima ubadili mawazo
Sasa huu mlango wa sita hutokea ukaunganisha familia kwa namna ya ajabu kabisa kupitia kwa mama watoto na hata baba mwenyewe
Ninapoandika haya muda huu kuna watu wako kwenye vituo mbalimbali vya usafiri wa majini angani na nchi kavu na wengine wanajiandaa kwenda huko
Ni katika ya watu hao kuna ambao kati yao
-usiku mzima alikuwa akiiwaza hii safari moyo unapiga paa/una shikamooo na kukosa amani
-mke au mume anakosa amani na kukushauri uahirishe safari na ukimuuliza kwanini anakwambia hajui
-mtoto/watoto wanaota ndoto za ajabu na kukusihi usisafiri au kama ni wadogo kulia bila sababu kila unapokaribia kutoka (kuna kule kumlilia mzazi lakini siku hiyo inakuwa tofauti )
Haya ni matukio ambayo kwa namna fulani yanakunyima amani moyoni..unajaribu kujiuliza bila jibu kuna kuna nini leo
Kuna kitu kinaitwa willpower, nguvu ya kutenda bila kujifahamu (ipo willpower ya kuamua kutenda pia, njia zote na ishara zote za kukutahadharisha kuwa uendako sio salama, na kama hiyo nguvu imeamua kukuepusha na janga linalokunyemelea yatatokea haya
-utasahau kufungasha kitu muhimu kitakachokulazimu urudi nyumbani kukichukua
-utaachwa na gari au itatokea dharura yoyote ya kukuchelewesha kufika kituo husika
-kwa sababu nyingine zozote zile utakosa kusafiri kwa kuachwa na chombo husika iwe ndege boat/meli au gari
Utakasirika sana na hata kugombana na aliyesababisha hiyo hali kama si mtu wa kutafakari. ..... ni mpaka pale utakapokuja kupata taarifa za kutisha kuhusu ajali ya chombo ulichotaka kusafiri nacho ndio litakupambazukia kuwa kwanini kulikuwa na mikwamo kiasi kile
Usipoisikiliza ile sauti! Usipotafakari ile mikwamo na ukalazimisha kwa kupingana na ile nguvu ya ndani basi unaenda kukutana na mustakabali wako
Haya mambo yapo na shuhuda ni nyingi mno...sikiliza waliokoka kusafiri na Mv Bukoba nk . utapata ushuhuda wa ajabu kabisa
Na hii si lazima iwe safari ya mbali kuna baadhi yetu mwisho wao waliuona kabisa . siku moja kabla unakuwa ni mtu wa mawazo na kukosa furaha bila kujua sababu ninini...ni mpaka litimie la kutimia ndio watu wataanza kusimulia
Ni muhimu sana kusikiliza sauti zinenazo ndani yetu zina ujumbe gani ...sauti ya ndani ni jicho la kiroho linaona mbele ya muda mavune yaliyokuzonga ndio yanazuia tu kukupa clear msg ya kile kinachotaka kukutokea... .. kabla ya kuchukua uamuzi wowote sikiliza sauti yako ya ndani..utaokoka na mengi
Masikiniii hadi nimejitahidi kuzuia chozi. Najaribu kuona vile baba alivyojilaumu na nafsi kumsuta yarabiiii daah.!!!!Ushuhuda wa kuhuzunisha wa Shauritanga girls boarding school
Nakukumbuka ilikuwa ni 1994 (kama sijakosea) ulipotokea moto kwenye shule tajwa hapo juu ambao uliondoka na mabinti 41 (kama sijakosea tena) kati yao kulikuwa na ndugu wawili
Tunafahamu ishu za kutoroka shule hasa weekend na kwenda home hasa kama sio mbali
Weekend hiyo wale mabinti wawili walitoroka na mpango wao ilikuwa wakalale nyumbani na kurudi Shuleni Jumapili
Wakashinda nyumbani vizuri na wazazi wao ilipofika jioni wakatakiwa kurudi shule (wazazi hawakuwa na lengo baya) mabinti walijitetea kwa nguvu zote mpaka kusaidiwa na mama lakini baba alishikilia msimamo wake..ikabidi waondoke kwa roho nzito mno kurudi Shuleni
Usiku ule wale mabinti ni kati ya wanafunzi walioteketea na ule moto
Hawa wazazi walikuwa wameshafunga kizazi hawakutaka kuzaa tena..
Baada ya kupata hizi taarifa na nafikiri kabla ya mazishi waliandika ushuhuda huu nao wakajiua kwa sumu