Tahadhari leo kwa wateja wa M-PESA.

Tahadhari leo kwa wateja wa M-PESA.

Leo nilikuwa nahamisha pesa kiasi cha 500,000/= kutoka kwenye akaunti yangu ya M-Pesa kwenda Tigo-Pesa nikapata message hii,

"Samahani, muhamala wako haukukamilika kwasababu za kiufundi. Tafadhari wasiliana na huduma kwa wateja".

Nilipoangalia salio pesa ikawa imekatwa lakini haijafika kwenye akaunti ya Tigo pesa, nilipopiga Huduma kwa wateja wakasema kuna matatizo ya kiufundi NISUBIRI MASAA 72 yaani siku tatu.

Yaani hapa nimechoka na pesa ilikuwa ya kusafirishia msiba.
Mimi nimenunua umeme jana wa 50000 kupitia Airtel nikaona kimya. Baada ya kupiga kuulizia wakasema ni kweli nimenunua lakini tanesco wanarekebisha mtandao nisubiri baada ya masaa 72 nikawaambia hiyo ni kero kubwa kwakuwa nauhitaji umeme huo wakati huo mpaka sasa hawajarudisha pesa wala hawajatuma umeme. Lakini baada ya dakika 10 nikanunua kupitia tigo nikapata. Inakera sana!
 
Hapo tatizo ni tiGo maana hata nami iliwahi kunisumbua kutuma pesa kutoka Airtel Money kwenda Tigo pesa. Muda mchache uliopita nimepokea pesa kupitia Mpesa bila tatizo lolote.
Asee umeandika lugha ya kiswahili lakini!!![emoji119] [emoji119]
 
Mwezi wa tano mwaka huu niliwahi kuhamisha pesa M pesa kwenda Airtel money ninunue umeme, hiyo pesa haijawahi kufika mpaka leo na wala haijawahi kurudi kwenye akaunti yangu ya Mpesa mpaka leo.
Me walinichukulia 200, yangu ya umeme haikurudi pia kama kuna sehemu nina ogopa kuweka pesa ni m.pesa
 
Utakuja poteza pesa zako utajuta usipende kuweka kiasi kikubwa cha pesa kwenye mitandao ya simu weka Bank tu mkuu ndipo salama zaidi.
 
Mm huwa situmi pesa cross network. Bora ungemwambia huyo mtu aende kwa wakala akachukue pesa zake na wewe uzitolee hapo
 
Mpesa ndo mtandao wenye pesa nyingi inayozunguka. Sababu umeenea sana japo wana gharama kubwa ila huduma zao nzuri sana
 
"Samahani, muhamala wako haukukamilika kwasababu za kiufundi. Tafadhari wasiliana na huduma kwa wateja".


Pole sana

Lakini hawa mitandao ya simu huwa wanaomba ushauri kwa wataalamu wa kiswahili kabla hawajatumia maneno kwenye mifumo yao?

Nilipata kuona na kusikia neno muamala na siyo muhamala sasa sijui lipi neno sahihi

Kiswahili kinazidi kupata umaarufu duniani, kama sisi ambao ni kitovu hatutakuwa na kiswahili standard basi tutawapoteza wanaokinyemelea
 
Kama hautawafuata makao makuu, sahau hiyo pesa, hakuna cha tatizo la kiufundi wala takataka gani, fuatilia pesa yako.
 
Hiyo michezo sio migeni kwenye masikio yangu
 
Back
Top Bottom