Leo nilikuwa nahamisha pesa kiasi cha 500,000/= kutoka kwenye akaunti yangu ya M-Pesa kwenda Tigo-Pesa nikapata message hii,
"Samahani, muhamala wako haukukamilika kwasababu za kiufundi. Tafadhari wasiliana na huduma kwa wateja".
Nilipoangalia salio pesa ikawa imekatwa lakini haijafika kwenye akaunti ya Tigo pesa, nilipopiga Huduma kwa wateja wakasema kuna matatizo ya kiufundi NISUBIRI MASAA 72 yaani siku tatu.
Hiyo mitambo inaweza kukata pesa tu isitume? kama ina tatizo kwanini isikatae kukata pesa mwanzoni kabisa? na kwanini wakae na pesa yangu masaa 72 bila riba kama sio wizi ni nini.
Yaani hapa nimechoka na pesa ilikuwa ya kusafirishia msiba.