Wakuu heshima zenu
Tahadhari kwa hizi namba tajwa hapo juu.
Siku ya Jumatano tarehe 19/10/2016 saa 3 asubuhi alinipigia bwana mmoja anajiita Samweli (0787-332977) akanitaja kwa jina nilosajili kwenye line yangu ya airtel na kuniuliza leo hujaenda kazini? Nikajibu ndiyo nipo home, akasema mimi naitwa Samweli(Mkurungezi wa kampuni nipo Dodoma) naomba uende AICC Hospital utamkuta Dr Shabani(0689-694153) mwambie Samweli ameniomba nisimamie mzigo wake wa dawa boxes 40 akataja jina gumu la dawa silikumbuki vizuri kila box shilingi 400,000 x 40 = 16,000,000.
Kuna mzungu anatokea KIA nakutumia no yake mara moja atakupigia mwambie wewe ni mwakilishi wa Kampuni na atakukabidhi million 24 cash, million 16 utalipa AICC na million 8 ni faida tutagawana mimi, mhasibu wangu na wewe, nikamjibu sawa. Baada ya muda mfupi akanipigia huyo Shabani A.K.A dr akaniuliza wewe ndiyo mwakilishi wa Samweli? Nikamjibu ndiyo. Mwambie wakaguzi wa TRA wanataka 480,000 cash bila mhuri wa TRA mzungu atakataa, nikamjibu kuwa ongea naye mimi nimeambiwa kusimamia kupaki mzigo (alipotaja hiyo hela nikaanza kushituka kuwa hapa kuna jambo). Baada ya muda Samweli akapiga cm akaniambia nimeongea na dr anataka 480,000 cash, akajifanya analalamika vibaya sana nikamwambia million 8 kutoa lakini 480,000 baki 7,520,000 mbona ni faida kubwa sana? Akasema isiwe tabu hapa mfukoni nina 280,000 naomba uniongezee laki 2 nikamwambia isiwe tatizo tuma hiyo 280,000 kwenye airtel money yangu nitaongezea hiyo laki 2 akasema sawa.
Baada ya kama dak 5 Shaban (dr) akapiga akasema Samweli amenitumia 280,000 amesema laki 2 unatoa wewe nikamjibu ni kweli natoa mimi lakini nipe dak 20 tu, baada ya dak 15 nikampigia nikamwambia nipo hapa getini japo sikuwa getini njoo unipokee au nielekeze ofisini kwako nipo na hela. Akasema ukiingia mlinzi atashituka nikamjibu mbona watu wengi wanaingia hashituki kwani anajua nakuja kufanya nini na wakati mimi nakuja kuonana na dr wangu? Wewe tuma kwenye simu nikamwambia poa ngoja niende airtel money town, Arusha airtel money ni za shida nyingi ni m-pesa akaniambia fanya haraka naandaa mzigo nije nao hotelini atapofikia mzungu na mhasibu wenu. Baada ya dak kama 5 mzungu feki(0787-407501) akapiga akaniambia anapata supu karibu na Golden Rose wapo na mhasibu wa kampuni lakini anavyoongea kimombo nikajua huyu ni tapeli, nikamwambia nakuja hapo nikufuate akakataa akasema anatafuta hoteli ya kulala na kupokelea mzigo.
Baada ya muda kidogo akanipigia Samweli (mkurugenzi feki) akaniuliza unafanya kazi gani? Nikamwambia nipo Monduli kambini akakata simu nikapiga hakupokea tena mpaka leo.
Hawajamaa ni matapeli wazoefu ukikurupuka unaenda na maji, maswali nilijiuliza inakuwaje mtu ambaye unamjua umuulize unafanya kazi gani? Kama wewe ni mkurugenzi wa kampuni dr anashindwaje kukuamini 480,000 wakati mnafanya biashara ya mamilioni? Maswali ni mengi sana siwezi kuandika yote.
Hawajamaa wamesajili majina yale ambayo wanayatumia kutapeli lakini ukituma pesa hutakaa uwapate na wanaomba hela kidogo iliusishituke. Tuwe makini jamani nimeona ni wafahamishe msije mkatapeliwa na sijui na wanazitoa wapi no za simu za watu pamoja na kutaja eneo ulipo, kama hawashirikiani na watu wa customer care basi wanashirikiana na watu wa karibu yako.
Tusikimbilie hela za haraka unaweza kutapeliwa kirahisi sana.
Nilichelewa kuirusha/post kutokana kuwa na majukumu mengine nilikuwa sijapata muda wa kuichapa.
Jamani mimi siyo mwandishi wa habari kwa hiyo mapungufu mtanisamehe japo lengo langu ni tahadhari kwa wadau wasijitapeliwa.
Asanteni.
Asante mkuu na pole sana
Mimi binafsi wameshanipigia mara 2, mwaka ,moja nikiwa mkoani morogoro , Mara ya pili nikiwa mkoani kagera
Wa morogoro
Alinipigia akataja jina langu na fani yangu , akaongea kuwa anafanya Kazi ofisi ya waziri mkuu kitengo cha kilimo kwanza na yuko iringa ,
Maelezo yalifanana kama yako ila alitlhitaji msaada wa bailing za tractor na alitaka mimsaidie akaniunganisha na dealer ambaye alikuwa mwanamke ambaye alimtambulisha kama kanali wa jeshi ( mzinga), na mhasibu aliyefikia Mildland hotel , yaani walizunguka mwisho yule kanali akadai mzigo upo tayari na inatakiwa laki 4 , ndio mzigo utoke jeshini maana mhasibu wa jeshi katia ngumu , aisee dau nililokuwa nimetangaziwa lilikuwa kubwa yaani kila bailing moja laki 6 na bailing 10 hvyo mil 6, na nikipewa hizo pesa ni dipost mil 4 kwenye akaunti yake na Mimi nichukue 2 , aisee lilikuwa dili la fasta kidogo nichanganyikiwe
Nilichofanya nikamwambia yule kanali wa uongo tukutane gate la chuo kikuu cha SUA , sababu alinambia yuko mzinga , basi nikasubiri kama dk 5, ikapigwa simu aisee mzigo upo tayari , hivyo nimekwama laki 2 , maana nimeambiwa nitoe laki 4, risit itoke sababu mzigo ni wa magendo , duuh nikashituka
Ikabidi nimpigie , jamaa aliyenipigia mwanzo yule wa ofisi ya waziri mkuu
Akadai yuko porini hana access na Mpesa hvyo nitoe then watarudisha pesa yule mhasibu wa kilimo kwanza akitoa , hapo nikashtuka
Nikamwambia nipe muda , kama dk 30 nikapiga , jibu namba unayopiga haipatikani ,nikajaribu ya kanali haipatikani , hapo nikagundua kweli walikuwa matapeli ,
Jina la tapeli huyo alijitambulisha kama MAPUNDA
Kagera
Kagera ilikuwa mwanzoni mwa mwaka huu ,jamaa akawa ananijua japo simjui akajitambulisha kuwa yuko bunda walihitaji msaada wa madawa flani yako biharamulo na MZEE flani yuko pale , aliongea mengi na kumiunganisha na mzungu anayetokea SA , nilichomjibu ni simple tu , OK Niko tayari ila Mimi Niko bukoba mjini sina nauli ya kwenda biharamulo nitumie nauli nikufanyie Kazi yako na sihitaji commission yoyote
Jamaa akasema tumia pesa yako , nikamjibu hiyo sio plan wala dili langu ni lako ,
Jamaa alikata simu , ila lafudhi ilikuwa ya kichaga