Hawa jamaa ni hatari.Mimi walinipigia nikabaki nacheka.Eti mtu anakwambia anamjua muuza viatu vya shanga na batiki.Halafu ya hivyo vitu bei yake anajua.Anataka umpigie muuzaji ubargain bei aliyokupangia.Kuna mzungu anatoka ngorongoro atavichukua Kia kwenda navyo ng'ambo.Yaani ni full comedy.Usipokuwa mjanja unaliwa.
Lakini mimi nilishaapa siku moja nitakuja kula hela ya tapeli.
Sababu wana-formula ya kutapelia kwa muda flani. Ikibuma wote kwa pamoja wanahamia formula nyingine!
Hii ya mzungu kuendelea kutapelia, haijakaa vizuri, kwa mjanja yeyote ni rahisi sana kuigundua.
Kuna hizi hela za chambo kwa ajili ya kuopolea mzigo ndohizo huwa nasema maranyingi kwamba ole wao!
Ingawa ni maranyingi sana nimewakosakosa, wakapitia tundu la sindano kusevia.
Siku1 waliingiza kiasi cha sh.4,000,000/= cash kwenye account yangu na wakanipigia cm kuniulizia kama hiyo cash nimeipata.
Nilivyo na kawaida kabla ya mjadala wowote lazima nihamishe salio lote kwenda account nyingine na kuitoa muda huohuo. Kama mtu katuma kimakosa hulazimu kumrejeshea baadae baada ya kujiridhisha.
Ss waliponiuliza nikwaambia subiri kdogo ntakujibu.
Nikaingia kwenye acct kuuliza salio nikaona cash mil.4. Nikaicommand ihamie kwenye acct nyingine ikagoma, ikidai salio halitoshelezi.
Tayari nikajua kwamba nipo kwenye ligi, mchezo wa kutafuta ubingwa!
Nikawapigia nikawaeleza kuwa nimekiona hicho kiasi nani kanitumia? Wakanitajia jamaa nisiye mfahamu na kunielekeza nimpigie kupata maelekezo. Lakini kabla ya kumpigia wakanitahadharisha, nimwamkie kwa lugha ya kinyenyekevu nikianza na shikamoo, maana ni mtu mzito na wa makamo.
Mtu huyo nilipompigia akanieleza fedhahizo zimeingizwa na boss wangu wangu ambae zamani tulikuwanae kazini. Na kwamba hizo pesa nisizichukue hadi Kwamba kanitumia hizo hela ili nimkopeshe kwa kumuongezea milioni2 kwa ajili ya kununulia uwanja maeneo ya mjini. Na kwakuwa mimi ni mwenyeji nimsaidie, kwenda hilo eneo na mil.6.
Nikawauliza kwa kutumia authentication kila swali. Nikagundua hawana lolote wanalolielewa kwangu ama kwa huyo boss wangu.
Nikawaambia kuwa tuonane popote wanapotaka wao ama waje nyumbani "kupopoa" hizo hela ambazo boss wangu kahitaji.
Ni hadithi ndefu. Lakini mara nyingi wanaoliwa huwa wanaaminishwa kupata faida maradufu ya fedha watakazotoa wao. Ni mbinu za kizamani. Ukiingiwa tamaa, lazima uliwe.