Benny
Naamini kabisa hukuelewa kabisa nilichoandika,! Ni hivi sizungumzii picha yako na mtu fulani au kitu fulani nazungumzia picha za makundi na hicho unachoita coincidence.
Kuna picha sipo nazo hapa lakini picha ya kwanza walipiga watu saba chini ya mtu watatu walikaa kushoto na wane walikaa kulia! Wale wane walikuja kufa kwa kufuatana kwa miezi minne mfululizo.
Picha nyingine jamaa wakiwa sekondari siku ya mahafali walipiga picha ya kumbukumbu wanafunzi kama kumi hivi na mabinti wa shule ya jirani.
Kwenye ile picha kuna kijana mmoja alikuwa kachuchumaa na binti mmoja halafu mwingine alikuwa kasimama pia na binti...baada ya miaka kupita kila mmoja bila kutegemea alimuoa binti aliyekuwa naye karibu na siku wanakutana kwenye kuangalia album mmoja ndio akakumbuka hilo tukio