The Native Son
Member
- Jul 14, 2009
- 86
- 19
Nisaidieni wadau tutafakari pamoja, je hii mahakama ya 'ICC" yenye makao makuu yake huko Hegue ni kwa ajili ya waafrika tu?? Maana ilianza na wanyarwanda na sasa wakenya na nilisikia kwenye chombo kimoja cha habari cha ughaibini kuwa wanajiandaa kuandaa mashitaka dhidi ya wa 'Ivory Coast'. Je ni vipi kuhusu Bush, Blair na washirika wao kwa uvamizi wa Iraq na Obama na washiki wake kwa uvamizi wa sasa wa Libya kwa kivuli cha Nato na UN????