Tafakuri, utumbuaji majipu na ufukuaji makaburi

MUSIGAJI

JF-Expert Member
Dec 26, 2014
2,187
2,462
Wakuu amani iwe kwenu,

Siku ya leo Mh Rais amezungumza na wahariri juu ya mambo mbalimbali yaliyofanyika katika mwaka mmoja huu wa utawala wake. Mtakumbuka kuwa katika kipindi hiki kuna habari ya utumbuaji majipu ambayo kimsingi imemjenga kisiasa Mh katika huu mwaka mmoja kwa watu wa kawaida.

Tumekuwa tukishuhudia watu wakitumbuliwa katika nafasi zao na wengine kufikishwa mahakamani kama kina Masamaki.Hawa watu wengi walifanya makosa/ubadhilifu kabla ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani lakini serikali hii imewawajibisha ni jambo jema sana.

Leo katika hotuba ya Mh Rais amezungumza jambo moja ambalo kimsingi limeendelea kunifikirisha sana,suala la ufukuaji makaburi.Mh amesema hayupo kufukua makaburi maana akiyafukua mengine atashindwa kuyafukia hivyo yeye ataanzia hapo tu alipoikutia nchi hataangaika na yale mengine yaliyopita.

Ametoa mfano wa fedha za kiwanda kule Lindi zilivyotafunwa na amekiri kuwa waliozitafuna wapo.
Sasa katika hali hii watu wanapokuwa wakizungumza kuwa wanaotumbuliwa na kupelekwa mahakamani ni vidagaa wale manyangumi tutawezaje kumbishia mtu anayesema hivyo.Mtu akisema hii ni doubles standard si atakuwa sahihi?

Kwa nini hawa watendaji wengine wakurugenzi wawajibishwe kwa mambo yaliyofanyika katika awamu ya nne wakati huohuo waliohusika na ufisadi mkubwa namna hii ambao bila shaka walikuwa/ni wanene wasiguswe kwa kuogopa kufukua makaburi?.
 
Hii tanzania wewe zaliwa,ishi, kufa. Ukisema ufatilie mambo ya nchi kwenye siasa unaweza ukazeeka mapema tuu.
Sasa we fikiria mtu anasema hafukui makaburi ya nyuma sasa kilichomfanya awafukuze wakurugenzi wa bandari, tra, tbs, muhimbili n.k ilikuwa ni nini hasa kama hafukui makaburi si angewaacha au angewastaafisha. Kwanini anafukua makaburi kwa kuchagua? Mana mpaka leo sijasikia swala la lugumi, escrow etc ina mana hiyo mahakama ya mafisadi atashtaki wamachinga au?
 
Kiukwel nilikua ndali ya daladala, kwa makini nafuatilia majibi yake,

Aisee pale hamna kitu aisee, off point kichiz yan, hao waulizaji wenyewe nao vila.z"a,

Kiukwel kauli yake hiyo ya kufukua makaburi imenisononesha sana na hapo ndo nimejua jins gam serikal ya ccm ilivyo ya kinafiki na ya kubebana kwenye kutetea maovu,
Cjaelewa hiyo mantiki ya mahakama ya mafisadi iwapo tutaendelea kwa kauli hizo za *sitaweza kuyafukia*

Kweli mwenye sikio asikie, hawez kufukua makaburi ya waliofinance kampeni,
 
Si aliahidi kuwalinda 'wakubwa' wakati na baada ya kuwa mkuu wa kaya, je aliahidi kumlinda 'dagaa'. Anyway, katika uvuvi, dagaa pia hutumika kama chambo.
Yawezekana hao kina nanii wametumbuliwa ili kuwanasa wananchi.
 
Inabidi Mkulu arudi afafanue hiyo kauli kwa taifa upya. x pm aliwahi sema tukabeza kuwa kuna mafisadi ukiyagusa nchi inatikisika. JPM yy kasema serikali ya awamu ya 5 atayakamata mafisadi yote, ambayo naamini ndiyo kayabatiza jina la makaburi leo na kakiri hatafukua makaburi hayo. Hz kauli tata sana.
 
Kuwekwa na kujiweka vitu viwili tofaut watu walimkataa lowassa sababu asinge kubali kuwekwa. Ndo haya sasa.
 
Hii tanzania wewe zaliwa,ishi, kufa. Ukisema ufatilie mambo ya nchi kwenye siasa unaweza ukazeeka mapema tuu.
Sasa we fikiria mtu anasema hafukui makaburi ya nyuma sasa kilichomfanya awafukuze wakurugenzi wa bandari, tra, tbs, muhimbili n.k ilikuwa ni nini hasa kama hafukui makaburi si angewaacha au angewastaafisha. Kwanini anafukua makaburi kwa kuchagua? Mana mpaka leo sijasikia swala la lugumi, escrow etc ina mana hiyo mahakama ya mafisadi atashtaki wamachinga au?
there is no such a thing called patriotic politics
 
Back
Top Bottom