denoo49
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 6,113
- 6,953
Kwani nimeandika somo zima la uongozi? of course uongozi ni zaidi ya haya lakini kiini hasa cha uongozi ni ushawishi siyo sheria wala taratibu. Ni uwezo wa kushawishi watu kuona wasichokiona, kukubali ambalo walikuwa hawakikubali au hawataki kukikubali na kutenda yale ambayo vinginevyo wangekuwa wanasita kuyafanya. Huwezi kuwa na kiongozi ambaye anakimbilia 'taratibu na sheria' kwa vile kashindwa kushawishi.
Kitu kimoja ambacho Nyerere alikuwa mbali sana kuliko viongozi wetu wengi wa sasa ni kuwa aliweza kushawishi (kama alishawishi kwa mazuri au la hilo jingine). Kiongozi ni lazima ajifunze kushawishi. Na hili ni kweli zaidi kwenye utawala wa demokrasia.
katika kiwango changu kidogo cha usomaji wa mambo ya utawala bora na utawala wa demokrasia ckuwahi pata kukutana na kitu ushawishi kama sehemu au kanuni moja wapo ya utawala bora, kiongozi bora. Je nipate kuyaamini toka kwako kua ushawishi ni ni sehemu ya kiongozi bora?? Na unahisi dunia yote ya sasa itasadiki vivyo?