Tafakari ya Mwanakijiji leo...

Tafakari ya Mwanakijiji leo...

Mkuu unaweza kushawishi kwa kujiamini pale tu kitu unachosimamia ni dhamira safi.Wananchi wana madai ya msingi na serikali inajua ni ya msingi lakini yaliyo nje ya mpango wao wenye maslahi tusiyoyajua.

Huwezi kushawishi u.puuzi zaidi ya kutumia nguvu hasa ukijua hula ya unao waongoza ni Watanzania! Hawa si wakuwaimbia nyimbo za falsafa ni kusema kwa kauli moja inatosha inabidi wasikilize umma kwa nguvu.

By the way mkuu,serikali imeshindwa kutushawishi, sawa.lakini huoni na sisi tumeshindwa kuwashawishi vile vile?

Hapa tukubaliane pande zote tumefeli na kuhatarisha muelekeo wa Taifa! Basi walau tusake muafaka!!!

thats exactly is the point; kiongozi akishindwa kwa hoja ashindwe; akishindwa kushawishi ashindwe asi resort kwenye kutumia njia nyingine ambazo hazileti ushawishi. Fikiria kwa mfano, serikali iamue kujenga hilo bomba la gesi kwa nguvu na kuhamisha wana kijiji na watu wakaandamana na wengine kujeruhiwa wengine watasema "serikali imesema" mimi nitasema "serikali imeshindwa kushawishi".

Kama serikali haiwezi kushawishi haipaswi kuendelea na mradi
 
Sisi unaotuita wajinga wa kufikiri,

Sijawahi kumuita mtu mjinga wa kufikiri usianze kwenda ambako si kwenda. NImesema kitu ambacho kiko dhahiri. Baadhi ya watu mara moja (kwa sababu ya preconceived ideas) waliamini kuwa nazungumzia exclusively kuhusu suala la BAVICHA. Halikuwa lengo langu.

Nataka nikuhakikishie hatusomi thread tukaishia hapo, we take it kidogo to next level of thinking.
1. Kauli/Thread hii imeandikwa na nani?
2. Thread hii imeandikwa wakati gani?
3. Thread hii imeandikwa katika mazingira gani?

Acha kujishusha hivyo; sijamuita mtu mjinga. Kufikiri kwa mwelekeo mmoja tu (BAVICHA) siyo ujinga.
4. Thread hii inamlenga nani? (For this matter OK as you've Just said MTWARA,Uongozi wa Vyama, BAVICHA)
Baada ya hapo sisi 'wajinga' ndio Analysist.

sawa; hili mbona wala si tatizo.

Despite all. I still respect you MMK[/QUOTE]
 
Kwa maandiko unapaswa ''ulikate" lakini wangapi unawaona wanatembea na jicho moja! na una uhakika gani lililobakia halitakosea?
Ok! ikitokea likikosea nitachukua hatua nyingine,ila kama halita nikosesha na bwana wangu it is ok.

Well maandiko sehemu fulani Yesu alisema "yaacheni magugu na ngano yakue pamoja!" Ila hakusema wakati wa mavuno tuchanganye pamoja ngano na magugu,kila kimoja kitakaa sehemu yake
Hufai katika chain ya uongozi out ,hapa hahitaki kushawishi kama ulisha mkuza katika maadili ya uongozi na kuonywa,utaachwa na kuwa wa mataifa kama sii kufunzwa na ulimwengu

Wengine watakuambia alitimiza kilichoandikwa.
ok alitimiza ahadi ,ila katika uongozi huoni wapo wasaliti ambao binafsi ama wametumwa kuhujumu uongozi/taasisi fulani?
Kiongozi hapasi kuwa dikteta,ila kama ni kwa manufaa ya wengi na faida kwa taifa ni vizuri kuwa dikteta,Huwa siku zote mwili na akili huwa zinatofautiana ila kwa manufaa yako na jamii hutumia udikteta kuukandamiza mwili wako mwenyewe
 
Mi nashangaa kwa nini mnaangaika kuchangia hoja nyepesi kiasi hichi, na sikutegemea ianzishwe na mtu kama MMK,

Uongozi ni composition ya hayo yote aliyosema + kufukuza. Ingawa kufukuza ni hatua ya mwisho na inachukuliwa pale inapoonekana kubaki kwa hawa watu kuna madhara zaidi ndani ya taasisi kuliko kuondoka.

MMK umeweka mpaka wa uongozi sehemu ambayo siyo. Jaribu kusoma taasisi mbali mbali zenye nidham uone inajengwaje. Anza na jeshi ( sio lazima iwe Tz)

Uongozi ni kusimamia sheria na taratibu zilizopo. Uongozi ni mambo mengi.

Kazi pia ya kiongozi ni kumpeleka punda kunywa maji. Swala la kunywa ni juu ya punda.

Jifunze kwa Wilson Mandela na mke wake wa kwanza Winnie ujue athari za usaliti.
Mm siamini mia kwa mia hoja wa Mzee Mwanakijiji . uongozi ni pamoja na udiktete ktk uongozi na utendaji bora.
 
Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari
Shukran kwa busara naona siku hizi unatoa mawazo ya ki-utu uzima.au mambo yaelemea kwa uwapendao
 
Kuna watu wana matatizo; watu wanapenda kufikiria vitu kwa upenyo mdogo sana na hii ni hatari. Kuna matukio mengi ambayo yametokea nchini na yote nimeyafikiria katika kauli hiyo hapo juu. Tumeona mwitiko wa serikali dhidi ya wananchi wa Mtwara walioandamana kuhusu suala la gesi. Mwitikio wa serikali umekuwa ni kejeli, mikwara na vitisho siyo ushawishi. Hili tumeliona huko nyumba ambapo serikali pia imetumia nguvu dhidi ya wananchi kwa sababu imeshindwa kuwashawishi.

Haya ya CDM nayo yanaweza kuwemo humo humo kwani nayo yanaonesha tatizo lile lile la kushindwa kushawishiana. Watu wanapotengeneza mitandao ambayo badala ya kufanya sapoti ya mtu yanaanza kumtega mtu, kujaribu kumwangusha au kumchafua ni kwa sababu watu hao wameshindwa hoja (na hapa nazungumzia pande zote zinazogongana - hakuna aliye salama).

Sasa mtu anaweza kujaribu kwa kutumia hoja lakini mtu asiyeweza hivi hutumia kushawishi kwa kutumia nguvu (ziwe za physical, law, procedures au hata jina lake).

Tusifikiri kidogo let think wider than personal politics.


Binafsi sikuwa mbali na wewe nilijua unazungumzia general context katika uongozi lakini kwa kuwa na issue ya CDM umeigusia na kwa sasa ndiyo iko burning sidhani kama ulitegemea watu wasi link bandiko lako hili na hiki kinachoendelea CHADEMA.

Napingana na wewe kwenye eneo la kuviziana na kutegana. Maana ili uvizie na kutega lazima umeshapata taarifa za uovu au uhaini dhidi ya taasisi. Walichokifanya CHADEAMA katika hili si kuvizia na kutega ni wao kuwa na tetesi za uovu/uasi na kuweka mtego. Iwe ni kwa kupandikiza mtu wa kushiriki uasi (participant observing/recording intelligence) ili baadaye aje na taarifa/ushahidi usio na mashaka kwa ajili ya hatua zaidi. Katika hili CHADEMA wamefanikiwa na wametegua bomu baya sana na ambalo nashawishika kuamini akina Mwigulu Nchemba na Wassira ndiko walikuwa wameweka imani yao.

Ndiyo maana katika sakata zima linaloendelea kama kweli kuna mtu alitumwa na Menejimenti ya CHADEMA kufuatilia usaliti/uasi wa baadhi ya wanachama wake sioni tatizo lolote as far as kama chama lazima muwe na intelejensia ambayo itanusa masuala mazito kama haya. Vinginevyo chama hakiwezi kufika kokote.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mwalimu pamoja na ushawishi mkubwa sana aliokuwa nao kwa Watanzania kuna mambo ilikuwa inabidi alazimishe yafanyike:
-Utakumbuka suala la watu kuhamia kwenye vijiji lilivyomhangaisha;
-Unajua pia alivyolazimisha kura tatu kule Tabora;
-Kuna baadhi ya viongozi walifukuzwa TANU na baadae CCM wakati chama cha siasa kilikuwa kimoja tu!
Ukiacha hayo ya zamani sana, sasa hivi sote tumeshindwa kuwashawishi WATANZANIA waone kwamba CCM haitufai. Wala hatutaweza mwaka 2015! Watu wezi kabisa ndio wanaotarajiwa kuwa marais wetu.
 
Mwanakijiji,
Hii Ndio tafsiri pekee unayoijua ya Uongozi? Hii tu,, y. UONGOZI NI USHAWISHI? hiyo tuuu,, kweli?
 
Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari

- Haya maneno yameandikwa na mtu ninayewaambieni all the times anafaa kugombea Urais huko kwenu, huyu Dr. Kitila na Zitto, basi ndio wanafaa, wengine wote hawafai kiongozi ni yule anayeweza kukosoa bila kuogopa nyie mmezoea kuogopana na kutishana tishana tu, sasa hapa mmepewa kubwa yao ona mnavyohangaika hangaika, tulizeni boli tafakari hapa!!

le mutuz
 
what i see ni kwamba MWANAKIJIJI NA ZITTO wana urafiki wa hali ya juu sana,na ni mtu anaempa backup ya kutosha sana katika mazingira tatanishi,wanachofanya ni kujivunjia heshima zao
 
- haya maneno yameandikwa na mtu ninayewaambieni all the times anafaa kugombea urais huko kwenu, huyu dr. Kitila na zitto, basi ndio wanafaa, wengine wote hawafai kiongozi ni yule anayeweza kukosoa bila kuogopa nyie mmezoea kuogopana na kutishana tishana tu, sasa hapa mmepewa kubwa yao ona mnavyohangaika hangaika, tulizeni boli tafakari hapa!!

Le mutuz
sisi waislam tunaamin siku zote mtu ukitaka kufaulu maishani basi subiri kwa rah'mani,ikitimia miadi wa juu hurudi chini,kama kubeba boxi nje ya nchi kumeshinda utawezaje kujenga hoja??kichwa kazi yake ni kufikiri,wewe ukaamua kwa khiyari yako kukimbilia nje ya nchi kwenda kukiharibu kichwa chako kwa kubebea mabox,ona upeo wako ulivokosa maono ya mbali,
huelweki unacheka au unalia,umeyagharim sana maisha yako,unatia huruma sana,,
unatembea hali ya kuwa ushakuwa maiti mda mrefu sana,pole sana ndugu yangu
 
sisi waislam tunaamin siku zote mtu ukitaka kufaulu maishani basi subiri kwa rah'mani,ikitimia miadi wa juu hurudi chini,kama kubeba boxi nje ya nchi kumeshinda utawezaje kujenga hoja??kichwa kazi yake ni kufikiri,wewe ukaamua kwa khiyari yako kukimbilia nje ya nchi kwenda kukiharibu kichwa chako kwa kubebea mabox,ona upeo wako ulivokosa maono ya mbali,
huelweki unacheka au unalia,umeyagharim sana maisha yako,unatia huruma sana,,
unatembea hali ya kuwa ushakuwa maiti mda mrefu sana,pole sana ndugu yangu

[h=2]Tafakari ya Mwanakijiji leo...[/h]
Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari

- Wachana na mimi huu ni mfupa umemshinda fisi wewe huuwezi, jadili hoja wachana na watu soma maneno ya mwanaume hapo juu kudadeki!!

le mutuz
 
Tafakari ya Mwanakijiji leo...



- Wachana na mimi huu ni mfupa umemshinda fisi wewe huuwezi, jadili hoja wachana na watu soma maneno ya mwanaume hapo juu kudadeki!!

le mutuz


Eti eeh,kama ulimshinda fisi,basi sisi tutaufanya namna hii :croc::croc::croc:,kisha tunakulipua like :boom::boom::boom::boom::boom:
 
Kwani nimeandika somo zima la uongozi? of course uongozi ni zaidi ya haya lakini kiini hasa cha uongozi ni ushawishi siyo sheria wala taratibu. Ni uwezo wa kushawishi watu kuona wasichokiona, kukubali ambalo walikuwa hawakikubali au hawataki kukikubali na kutenda yale ambayo vinginevyo wangekuwa wanasita kuyafanya. Huwezi kuwa na kiongozi ambaye anakimbilia 'taratibu na sheria' kwa vile kashindwa kushawishi.

Kitu kimoja ambacho Nyerere alikuwa mbali sana kuliko viongozi wetu wengi wa sasa ni kuwa aliweza kushawishi (kama alishawishi kwa mazuri au la hilo jingine). Kiongozi ni lazima ajifunze kushawishi. Na hili ni kweli zaidi kwenye utawala wa demokrasia.

......

Tungeweza kuongea zaidi kama ungeweka case study unless itakuwa ngumu kukosoa ulipokosea kutoka kwenye message ya kwanza.

Hata huyo Nyerere pamoja na ushawishi kuna baadhi walimhujumu na alipogundua ALIWASHUGHULIKIA IPASAVYO.

Kitu ambacho unapaswa kusema ni kuwa; katika uongozi...ushawishi ni hatua ya kwanza katika kundi husika au kundi fulani. Ila kuna hatua zinafuata na ya mwisho zikishindikana zote ni wewe kiongozi kujiuzulu.
 
mwanakijiji falsafa za aina hii huwa ni ngumu sana kwenye jamii zenye njaa kama tanzania. Kwa mtanzania akiahidiwa hela hata cheo anasahau hata wenzake, jamii au familia yake kwa taaabu zinazowapata
 
Tafakari ya Mwanakijiji leo...



- Wachana na mimi huu ni mfupa umemshinda fisi wewe huuwezi, jadili hoja wachana na watu soma maneno ya mwanaume hapo juu kudadeki!!

le mutuz.......

Wewe ndiye mfupa walioshindwa wengi?????? akili yako naona haiko sawa na kama haiko ikosawa basi unashikiwa na watu wengine. Fikiria watu wengine wala sio wewe kama wewe.

Ulishawahi ishi kijijini kule ambako wana jimulikia kwa kutumia kijinga cha kuni, mlo mmoja au kushindia uji?
 
Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari

Uongozi ni utumishi, ni kuonesha mfano, ni ujenzi wa taifa (kisiasa, kiuchumi, kijamii, kimaadili etc). "Tawi linalozaa baba hulitunza... lisilozaa hulikata..."
 
Mgema akisifiwa....................
Field ni sehemu ya mwisho ya kujifunzia/kufanyia jambo kama ukifeli field ndiyo mwisho ya darasani ni muongozo tuu wa kufika field.Tunakukaribisha ktk uongozi na dhani tutajifunza mengi tukiwa Field.
 
Zitto Kabwe


Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari- MwanaKijiji

Source: Facebook



Like · · Share · 13 minutes ago via mobile ·

CDM haina tabia ya kulindana kama nyinyi. Mnalindana mpaka mnazalisha makundi kibao, ngoja tuone ili linaloanzisha la Wasira kuutaka Urais, hii ni njama ya makusudi kama ile alivyofanyiwa Six na chenge. Akitokea kirusi tunakipulizia dawa mapema.
 
Back
Top Bottom