Tafakari ya Mwanakijiji leo...

Tafakari ya Mwanakijiji leo...

Mwisho wa siku hutulazimishi tuamini kwamba kila mtizamo wako ulivyo basi ndio uko sahihi, ni wewe ndio ulikuwa mpiga debe mkubwa wa CCJ kwenye Media matokeo yake chama kikafa kabla hakijasajiliwa, kuna muda tuache tutumie uwezo wetu wa kufikiri na usidhani unaweza kufikiri kwa niaba yetu, hell no.

www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/347364-akina-mzee-mwanakijiji-ni-wavivu-kufikiri-10.html#post4986677

unaikumbuka hii?
 
Chadema hakuna uongozi ....viongozi wa chadema upeo wa kutatua migogoro ni kufukuzana tu......inatia shaka
 
Kamnukuu mwanakijiji kwa style ya kinafki,ivi jamaa ana jiamini sana na hayo maboksi meusi eh?atambue panya watabaki t
 
Ila ccm ndio kuna viongozi wazuri tu aisee hii ndio tanzania.
 
Kibe
Akil yako ina soma analog bdo hamia digital
 
soma vizuri nilichoandika unalia nini kwa mods?
Zitto kanukuu hiyo kutoka kwa mwanakijiji akaiandika kinafiki kwenye fb page yake, what does it mean?
Mbona hiyo nukuu haipo kwenye facebook ya Zitto? hebu rudi tena kwenye account ya Zitto ujiridhishe, mimi nimeangalia hamna kitu kama hicho yeye anaongelea katiba mpya kwenye post zake za leo.
 
Last edited by a moderator:
Chadema hakuna uongozi ....viongozi wa chadema upeo wa kutatua migogoro ni kufukuzana tu......inatia shaka

Kwa taarifa yako ndugu KIBE , CCM inaunganishwa na Hayo madaraka waliyonayo tu , ukiwatoa madarakani wape Only 2 years , baada ya hapo kwishney ! Cdm wanajitahidi sana kushinda Mitego , ungejua pesa iliyotumika kusambaratisha CDM hadi leo , utashangaa kwa nini Cdm bado ipo ! Kumbuka Ccm ni 'maisha ' lakini Cdm ni ' uhai '
 
Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari

CCM haina ushawishi tena kwa Watanzania, hii iko wazi maana mpaka kule ambako kulikuwa kunaaminika kuwa ndiyo ngome ya CCM wananchi wamekata tamaa wanaandamana kwa mabango yanayoonesha kuwa CCM wanategemea nguvu ya vyombo vya dola Polisi, TISS na Majeshi(refer;Ukituua mtapelekwa The Hegue). CCM wanategeana wenyewe kwa wenye mfano hai ni zile kura za maruhani, Saga la Joka la mdimu vs Edo...
CCM kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa VITISHO na MIKWARA kwa kua raia wasiokuwa na hatia Arusha, USA, Nyamongo, Tandahimba, Songea, Iringa, morogoro na Znz..
CCM walishindwa hoja ya madaktari badala yake waziri mkuu akaamuru utekaji na uteswaji wa Dr Ully(Refer Liwalo na liwe). CCM inatisha wananchi wenye kuhoji ubadhirifu katika kila sekta, ubadhirifu na UFISADI mkubwa wa rasilimali zetu, itoshe kusema kuwa CCM imeshindwa hoja ya kuleta maisha bora kwa Watanzania....TAFAKARI! Amia CDM tuikomboe nchi yetu...
 
- Ndio maana nilisema Zitto, Mwanakijiji na Dr. Kitila ndio wanaofaa kugombea Urais Chadema, hii ya leo inaitwa kumkoma nyani giladi!!

le mutuz

Wakigombea utawapigia kura? Fikiria vizuri tena kwa mapana kabla ya kuweka chochote hapa JF.
 
Mi nashangaa kwa nini mnaangaika kuchangia hoja nyepesi kiasi hichi, na sikutegemea ianzishwe na mtu kama MMK,

Uongozi ni composition ya hayo yote aliyosema + kufukuza. Ingawa kufukuza ni hatua ya mwisho na inachukuliwa pale inapoonekana kubaki kwa hawa watu kuna madhara zaidi ndani ya taasisi kuliko kuondoka.

MMK umeweka mpaka wa uongozi sehemu ambayo siyo. Jaribu kusoma taasisi mbali mbali zenye nidham uone inajengwaje. Anza na jeshi ( sio lazima iwe Tz)

Uongozi ni kusimamia sheria na taratibu zilizopo. Uongozi ni mambo mengi.

Kazi pia ya kiongozi ni kumpeleka punda kunywa maji. Swala la kunywa ni juu ya punda.

Jifunze kwa Wilson Mandela na mke wake wa kwanza Winnie ujue athari za usaliti.
 
MMK umeweka mpaka wa uongozi sehemu ambayo siyo. Jaribu kusoma taasisi mbali mbali zenye nidham uone inajengwaje. Anza na jeshi ( sio lazima iwe Tz)

Uongozi ni kusimamia sheria na taratibu zilizopo. Uongozi ni mambo mengi.

Kazi pia ya kiongozi ni kumpeleka punda kunywa maji. Swala la kunywa ni juu ya punda.

Jifunze kwa Wilson Mandela na mke wake wa kwanza Winnie ujue athari za usaliti.

Kwani nimeandika somo zima la uongozi? of course uongozi ni zaidi ya haya lakini kiini hasa cha uongozi ni ushawishi siyo sheria wala taratibu. Ni uwezo wa kushawishi watu kuona wasichokiona, kukubali ambalo walikuwa hawakikubali au hawataki kukikubali na kutenda yale ambayo vinginevyo wangekuwa wanasita kuyafanya. Huwezi kuwa na kiongozi ambaye anakimbilia 'taratibu na sheria' kwa vile kashindwa kushawishi.

Kitu kimoja ambacho Nyerere alikuwa mbali sana kuliko viongozi wetu wengi wa sasa ni kuwa aliweza kushawishi (kama alishawishi kwa mazuri au la hilo jingine). Kiongozi ni lazima ajifunze kushawishi. Na hili ni kweli zaidi kwenye utawala wa demokrasia.
 
Nakubaliana na MM kwamba uongozi ni ushawishi lakini kwa swala hili la BAVICHA hakuna ushawishi hapo, wasaliti wachache kama hawa ambao wameshanunuliwa hakuna haja ya kuwashawishi. Hivi kweli kiongozi anamdhalilisha Katibu mkuu wa chama hadharani then kuna haja ya kumshawishi, hata Yesu alisalitiwa na Yuda na hakuona kuna haja ya kumshawishi asimsaliti japokuwa alifahamu..
 
Usisome zaidi ya nilivyoandika; unaweza kuapply kwenye lolote vile.

mkuu, unaponena kuwa hizi kanuni zako zinawekutendeka popote huoni kua unapotosha, yamkini kihoja umemaliza na mlengo wa kisiasa.? Je kifamilia yatupasa kufuata vivyo?
Na neno "ushawishi" hapa ulikua una maana gani?
 
Kwani nimeandika somo zima la uongozi? of course uongozi ni zaidi ya haya lakini kiini hasa cha uongozi ni ushawishi siyo sheria wala taratibu. Ni uwezo wa kushawishi watu kuona wasichokiona, kukubali ambalo walikuwa hawakikubali au hawataki kukikubali na kutenda yale ambayo vinginevyo wangekuwa wanasita kuyafanya. Huwezi kuwa na kiongozi ambaye anakimbilia 'taratibu na sheria' kwa vile kashindwa kushawishi.

Kitu kimoja ambacho Nyerere alikuwa mbali sana kuliko viongozi wetu wengi wa sasa ni kuwa aliweza kushawishi (kama alishawishi kwa mazuri au la hilo jingine). Kiongozi ni lazima ajifunze kushawishi. Na hili ni kweli zaidi kwenye utawala wa demokrasia.

vitabu vitakatifu vinatueleza ya kua yatupasa kukwepa vishawishi, hapa we unaliongeleaje baina na kiongozi na waongozwaji?
 
Back
Top Bottom