Tafakari ya Mwanakijiji leo...

Tafakari ya Mwanakijiji leo...

Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari

Natafakari na nazidi kuelewa nini maana ya TANU/AFRO SHIRAZ/CCM kushindwa kwa HOJA kwa kuwatimua Mtemvu, Fundikira, Msangi, Hanga, Maalim Seif, Jumbe, Babu, n.k.

Huko kulikuwa ni kushindwa kwa hoja kwa uongozi wa Mwalimu JKN. Uongozi siyo vitisho wala mikwara.

Vile vile natafakari na kuelewa kukubalika na kutoshindwa kwa hoja kwa Mwenyekiti JMK kwa kutowavua magamba mapacha watatu: Lowassa, Rostam na Chenge na mafisadi kedekede ndani ya CCM, pamoja na wale waliopata nafasi zao kwa rushwa za uchaguzi.

Huu ndiyo uongozi uliokubuhu na usiyo na vitisho wala mikwara. Hakuna mambo kama vile kupeana siku 90 kwa magamba kujivua au wale walioshinda NEC kwa rushwa "kushughulikiwa" ndani ya miezi 6. Uongozi siyo vitisho wala mikwara.

Mwanakajiji, with all due respect, nashindwa kukuelewa na hii tafakuri yako. Is it not the case of what is good for the goose?

Pia kama mwana-CCM nitategemea kuwa chochote CDM, TLP au NCCR inachofanya kujidhoofisha ni baraka kwa CCM kwani kuvuja kwa pakacha.............!!!!

Sijawahi kuona bondia anamuongezea lishe bora mpinzani wake ili pambano liwe zuri.
 
- Ndio maana nilisema Zitto, Mwanakijiji na Dr. Kitila ndio wanaofaa kugombea Urais Chadema, hii ya leo inaitwa kumkoma nyani giladi!!

le mutuz

kwa hiyo akigombea mmoja wao kupitia chadema utampa kura na kumkana wa ccm.?
 
Anachomaanisha mwanakijiji ni kuwa, "KUSIWE NA KANUNI WALA TARATIBU" na kama vipo visisimamiwe. Kama kanuni zikiwepo na zikasimamiwa ni lazima kuwe na uwajibikaji (kama kufukuza). MM hataki hivyo. Hiyo ndo mantiki yake. ARGUMENT YA AJABU KWELI KWELI. Kuna ulimwengu wa namna hiyo? SIO MAWAZO YA KUFIKIRIKA KWELI MM!
 
Usisome zaidi ya nilivyoandika; unaweza kuapply kwenye lolote vile.
Katika watu ambao napenda kufuatilia tread zao na zina mashiko ni mwanakijiji Big up broo.ila nataka kukuuliza maswali matatu tuu.
1. Je ukiona mkono wako au jicho lako linakokoseha na Mungu wako utafanyaje?
2.katika shamba lako langano/zabibu kukiwa na magugu atayaondoa ama utayaacha?
3.Unamfahamu Yuda iskarioti? Na madhara yake ?
 
Zitto Kabwe


Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari- MwanaKijiji

Source: Facebook


·

True to a certain extent, lakini kama wote wanaamini hivyo, kwanini tunakuwa na situation ya CCJ, CHAUMMA? Walishindwa kushawishi na kukimbilia kwenye 'adultery ya kisiasa? Na unapokuwa na side dish i.e CHAUMMA or CCJ ndio kusema umeshinda hoja?
 
Yani wewe hata ubalozi wa Nyumba kumi hufai. Yani wewe ni zero shuleni, zero kichwani na ziro kwenye familia.



- Ndio maana nilisema Zitto, Mwanakijiji na Dr. Kitila ndio wanaofaa kugombea Urais Chadema, hii ya leo inaitwa kumkoma nyani giladi!!

le mutuz
 
True to a certain extent, lakini kama wote wanaamini hivyo, kwanini tunakuwa na situation ya CCJ, CHAUMMA? Walishindwa kushawishi na kukimbilia kwenye 'adultery ya kisiasa? Na unapokuwa na side dish i.e CHAUMMA or CCJ ndio kusema umeshinda hoja?

Baelezee baelezee wanafiki washakunaku hao,baelezee mashankumpe vizabizabina baelezee washambenga wakubwa hao baelezee
 
Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari

Heri yote hayo, maana tumetoka kwenye mstari wa nidhamu, na ni bora kuliko kuatamia ufisadi na kuhalalisha utawala usio jali sheria na uwajibikaji.
 
Kuna watu wana matatizo; watu wanapenda kufikiria vitu kwa upenyo mdogo sana na hii ni hatari. Kuna matukio mengi ambayo yametokea nchini na yote nimeyafikiria katika kauli hiyo hapo juu. Tumeona mwitiko wa serikali dhidi ya wananchi wa Mtwara walioandamana kuhusu suala la gesi. Mwitikio wa serikali umekuwa ni kejeli, mikwara na vitisho siyo ushawishi. Hili tumeliona huko nyumba ambapo serikali pia imetumia nguvu dhidi ya wananchi kwa sababu imeshindwa kuwashawishi.

Haya ya CDM nayo yanaweza kuwemo humo humo kwani nayo yanaonesha tatizo lile lile la kushindwa kushawishiana. Watu wanapotengeneza mitandao ambayo badala ya kufanya sapoti ya mtu yanaanza kumtega mtu, kujaribu kumwangusha au kumchafua ni kwa sababu watu hao wameshindwa hoja (na hapa nazungumzia pande zote zinazogongana - hakuna aliye salama).

Sasa mtu anaweza kujaribu kwa kutumia hoja lakini mtu asiyeweza hivi hutumia kushawishi kwa kutumia nguvu (ziwe za physical, law, procedures au hata jina lake).

Tusifikiri kidogo let think wider than personal politics.
 
True to a certain extent, lakini kama wote wanaamini hivyo, kwanini tunakuwa na situation ya CCJ, CHAUMMA? Walishindwa kushawishi na kukimbilia kwenye 'adultery ya kisiasa? Na unapokuwa na side dish i.e CHAUMMA or CCJ ndio kusema umeshinda hoja?

Well, bado ni kweli. Unapojaribu kuwashawishi watu wa chama chakeo kuelekea upande fulani na unatumia njia za kawaida za ushawishi (kupendekeza sera tofauti, itikadi tofauti au mwelekeo tofauti) na hupati mwitiko unaotarajia unaweza kuamua kabisa kuanzisha chama kinachoendana na malengo na mitazamo yako. Lakini ili uanzishe chama hicho inabidi uwashawishi watu wakubaliane na wewe; siyo uwatishe au kuwashawishi kwa ahadi za vyeo au vitu kama hivyo.
 
Katika watu ambao napenda kufuatilia tread zao na zina mashiko ni mwanakijiji Big up broo.ila nataka kukuuliza maswali matatu tuu.
1. Je ukiona mkono wako au jicho lako linakokoseha na Mungu wako utafanyaje?

Kwa maandiko unapaswa ''ulikate" lakini wangapi unawaona wanatembea na jicho moja! na una uhakika gani lililobakia halitakosea?
2.katika shamba lako langano/zabibu kukiwa na magugu atayaondoa ama utayaacha?

Well maandiko sehemu fulani Yesu alisema "yaacheni magugu na ngano yakue pamoja!"

3.Unamfahamu Yuda iskarioti? Na madhara yake ?

Wengine watakuambia alitimiza kilichoandikwa.
 
Anachomaanisha mwanakijiji ni kuwa, "KUSIWE NA KANUNI WALA TARATIBU" na kama vipo visisimamiwe. Kama kanuni zikiwepo na zikasimamiwa ni lazima kuwe na uwajibikaji (kama kufukuza). MM hataki hivyo. Hiyo ndo mantiki yake. ARGUMENT YA AJABU KWELI KWELI. Kuna ulimwengu wa namna hiyo? SIO MAWAZO YA KUFIKIRIKA KWELI MM!

Shindwa! ningetaka kusema hivyo ningesema hivyo. Ukiwa na kanuni unatumia kanuni kushawishi compliance. Kwa vile wengi mmekaa kwenye suala la CDM badala ya kufiki upana wa hoja yangu fupi niseme hivi. HIvi haya yanayotokea CDM yanakuja yakishangaza watu? Kwamba hakuna mtu aliyejua haya yakitokea? Hizo kanuni zilikuwa wapi hadi watu wanafikia mahali kuitana masalia? Miaka miwili zaidi zakubembelezana, kubebana na kuchekeana? Uongozi gani huu?
 
Kuna watu wana matatizo; watu wanapenda kufikiria vitu kwa upenyo mdogo sana na hii ni hatari. Kuna matukio mengi ambayo yametokea nchini na yote nimeyafikiria katika kauli hiyo hapo juu. Tumeona mwitiko wa serikali dhidi ya wananchi wa Mtwara walioandamana kuhusu suala la gesi. Mwitikio wa serikali umekuwa ni kejeli, mikwara na vitisho siyo ushawishi. Hili tumeliona huko nyumba ambapo serikali pia imetumia nguvu dhidi ya wananchi kwa sababu imeshindwa kuwashawishi.

Haya ya CDM nayo yanaweza kuwemo humo humo kwani nayo yanaonesha tatizo lile lile la kushindwa kushawishiana. Watu wanapotengeneza mitandao ambayo badala ya kufanya sapoti ya mtu yanaanza kumtega mtu, kujaribu kumwangusha au kumchafua ni kwa sababu watu hao wameshindwa hoja (na hapa nazungumzia pande zote zinazogongana - hakuna aliye salama).

Sasa mtu anaweza kujaribu kwa kutumia hoja lakini mtu asiyeweza hivi hutumia kushawishi kwa kutumia nguvu (ziwe za physical, law, procedures au hata jina lake)

Tusifikiri kidogo let think wider than personal politics.
Mwisho wa siku hutulazimishi tuamini kwamba kila mtizamo wako ulivyo basi ndio uko sahihi, ni wewe ndio ulikuwa mpiga debe mkubwa wa CCJ kwenye Media matokeo yake chama kikafa kabla hakijasajiliwa, kuna muda tuache tutumie uwezo wetu wa kufikiri na usidhani unaweza kufikiri kwa niaba yetu, hell no.
 
"So your task will be to win people's mind and count you as credible by your writings.After attaining the superior credibility,you can now directs issues whatever our interests are.I strongly believe that you can manage it mr....."Said one of TISS executive officers to mr....
 
Mwisho wa siku hutulazimishi tuamini kwamba kila mtizamo wako ulivyo basi ndio uko sahihi, ni wewe ndio ulikuwa mpiga debe mkubwa wa CCJ kwenye Media matokeo yake chama kikafa kabla hakijasajiliwa, kuna muda tuache tutumie uwezo wetu wa kufikiri na usidhani unaweza kufikiri kwa niaba yetu, hell no.

Well.. hakuna aliyefanikiwa ambaye hajawahi kushindwa. Kama hujawahi kuonja kushindwa unaweza usijue namna ya kushinda! Kwani CCK haijasajaliwa kama chama cha siasa?
 
Shindwa! ningetaka kusema hivyo ningesema hivyo. Ukiwa na kanuni unatumia kanuni kushawishi compliance. Kwa vile wengi mmekaa kwenye suala la CDM badala ya kufiki upana wa hoja yangu fupi niseme hivi. HIvi haya yanayotokea CDM yanakuja yakishangaza watu? Kwamba hakuna mtu aliyejua haya yakitokea? Hizo kanuni zilikuwa wapi hadi watu wanafikia mahali kuitana masalia? Miaka miwili zaidi zakubembelezana, kubebana na kuchekeana? Uongozi gani huu?

Unatafuta kuitwa msaliti, huwa hatuisemi CDM wenzio.
 
Tukisema tunaonekana tunachonga sana ila ukweli ni lazima usemwe ila mbivu na mbichi vijulikane.

Hii hapa ni nukuu yake Zitto kutoka Fb page yake kwa kutumia nukuu ya mwanakijiji kaandika hivi.
" Uongozi ni ushawishi, uongozi siyo kutengeshana, kunyemelezeana na kufukuzana, na uongozi siyo vitisho au mikwala
Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja
Hii ni kweli kwa vyama vile vile vitisho kushindwa hoja"

my outlook:
Unganisha dot on uhusiano wa Zitto na msalaia, tukio la sasa, utaona nukuu ya zitto ina maana halisi ya vijembe kwa heche na BAVICHA.

Mwenye macho haambiwi tazama.
 
Back
Top Bottom