Kuna mdada mmoja jamani ni mrembo mpaka wanawake wenzake wanampenda, anaishi maeneo ya Mbezi Beach mtaa siutaji watu watamsumbua, ana kila kitu kuanzia biashara kubwa tu, nyumba na magari ya kifahari kila siku anahangaika kuomba ushauri kwa wanasaikolojia ili wamsaidie kutatua msongo wa mawazo alionao.
TATIZO:
Mwanaume wake wa kwanza hakumpa haraka alimzungusha mpaka ikafikia huyo mwanaume akamjengea nyumba ili tu demu akubali kumpa mambo yetu. Demu akalegea akatoa tunda, siku jamaa alipokula tunda tu hakuonekana tena mpaka leo.
Mwanaume wake wa pili, naye hakumpa haraka akichelea maumivu, jamaa alihangaika mpaka akamnunulia demu Harrier, baadaye sana demu akashawishika tena akaliwa tunda. Jamaa aliporudia mara mbili tu akapata safari kwenda majuu aliporudi baada ya mwaka mmoja akamshiti huyo dada mpaka leo.
Kwa mfano huu hai, mtaona ilivyo vigumu kutabiri mapenzi. Unaweza kuchelewa kutoa penzi na ukaachwa, mwenzio aliyetoa penzi chapchap watu wanaweza kuweka kambi hapo hapo milele.
Siwezi nikajua huyu mdada ana siri gani nyuma ya pazia hasa mambo ya chumbani, lakini ukweli unabakia pale pale mambo haya hayana kanuni.