MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,214
- 22,280
TAFADHALI MCHUNGAJI WA TAIFA, MTUME NA NABII KOMANDOO MASHIMO MUOMBEE MSAMAHA LE COMMANDANT MAKONDA KWA WANANCHI.
Watu wenye busara akiwemo Lemutuz na Binamu Bananga tayari wameshauri RC Mstaafu aombe msamaha kwa aliowakosea hasa viongozi wenzake. Mwenye busara mmoja akashauri awatumie viongozi wa dini kumuombea msamaha. Asiende kichwakichwa... atangulize mjumbe.
Sasa mimi baada ya kufikiria kwa makini sana nimeona ndugu Bashite aongee na mchungaji wa taifa, mtume na nabii komandoo Mashimo kumuombea msamaha kwa aliowakosea hasa viongozi. Hii tafakuri yangu ni ya kimkakati sana na ninawasihi wananchi wote mnaosoma hapa msipuuze.
Kwanini nimeshauri Mchungaji Mashimo? Sababu ni zifuatazo;
1. Kitendo cha kujiita mchungaji wa taifa ni kete muhimu sana ya kidiplomasia kwa mchungaji Mashimo wakati wa mazungumzo ya kuomba msamaha. Pia ukamandoo wake utamsaidia endapo mambo yakimbadilikia... wanasemaga "mjumbe hauwawi" lakini kwa hii ishu ya Bashite huo msemo unaweza ukapuuzwa. Komandoo Mashimo ana-fit.
2. Huyu mchungaji ameonyesha kuendelea kumkubali Bashite hadi siku za hivi karibuni hivyo ni rahisi kuguswa na hitaji lililopo. Baadhi ya viongozi wa dini walijitenga nae mapema tu.
3. Mashimo anapatikana kirahisi mno. Ni kiasi cha kudamka mapema na kumkuta stendi ya mbezi mwendokasi. Ukifika pale fuata tu sauti ya mchungaji anayehubiri.
4. Kwa kuwa Mashimo ni mchungaji mpenda kiki ambaye huwa lazima kwenye kila tukio linalo-trend aweke pua yake hivyo itakuwa rahisi kukimbilia hii tenda. Tena awahiwe haraka sana kabla hajaenda Ukraine kuwafanyia maombi kama alivyosema huko Insta.
5. Ukisoma uandishi wa mchungaji Mashimo na Bashite kwenye post zao utagundua wanafanana kiuandishi. Nadhani IQ zao zinafanana pia... hivyo wakutanishwe waelewane. Ndege wafananao huruka pamoja.
6. Gharama ya kumtumia Mashimo haitakuwa kubwa. Ikitengwa Tsh 30,000/= akapewa advance Tsh 17,000/= tayari tunaanza kuhesabu ushindi.
Watu wenye busara akiwemo Lemutuz na Binamu Bananga tayari wameshauri RC Mstaafu aombe msamaha kwa aliowakosea hasa viongozi wenzake. Mwenye busara mmoja akashauri awatumie viongozi wa dini kumuombea msamaha. Asiende kichwakichwa... atangulize mjumbe.
Sasa mimi baada ya kufikiria kwa makini sana nimeona ndugu Bashite aongee na mchungaji wa taifa, mtume na nabii komandoo Mashimo kumuombea msamaha kwa aliowakosea hasa viongozi. Hii tafakuri yangu ni ya kimkakati sana na ninawasihi wananchi wote mnaosoma hapa msipuuze.
Kwanini nimeshauri Mchungaji Mashimo? Sababu ni zifuatazo;
1. Kitendo cha kujiita mchungaji wa taifa ni kete muhimu sana ya kidiplomasia kwa mchungaji Mashimo wakati wa mazungumzo ya kuomba msamaha. Pia ukamandoo wake utamsaidia endapo mambo yakimbadilikia... wanasemaga "mjumbe hauwawi" lakini kwa hii ishu ya Bashite huo msemo unaweza ukapuuzwa. Komandoo Mashimo ana-fit.
2. Huyu mchungaji ameonyesha kuendelea kumkubali Bashite hadi siku za hivi karibuni hivyo ni rahisi kuguswa na hitaji lililopo. Baadhi ya viongozi wa dini walijitenga nae mapema tu.
3. Mashimo anapatikana kirahisi mno. Ni kiasi cha kudamka mapema na kumkuta stendi ya mbezi mwendokasi. Ukifika pale fuata tu sauti ya mchungaji anayehubiri.
4. Kwa kuwa Mashimo ni mchungaji mpenda kiki ambaye huwa lazima kwenye kila tukio linalo-trend aweke pua yake hivyo itakuwa rahisi kukimbilia hii tenda. Tena awahiwe haraka sana kabla hajaenda Ukraine kuwafanyia maombi kama alivyosema huko Insta.
5. Ukisoma uandishi wa mchungaji Mashimo na Bashite kwenye post zao utagundua wanafanana kiuandishi. Nadhani IQ zao zinafanana pia... hivyo wakutanishwe waelewane. Ndege wafananao huruka pamoja.
6. Gharama ya kumtumia Mashimo haitakuwa kubwa. Ikitengwa Tsh 30,000/= akapewa advance Tsh 17,000/= tayari tunaanza kuhesabu ushindi.