TACAIDS: Wafadhili wanaendelea kununua ARVs

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) imekanusha taarifa iliyochapishwa na gazeti la Mwananchi iliyosema wafadhili wajitoa dawa za UKIMWI.

TACAIDS imesema taarifa hiyo si ya kweli hakuna wafadhili waliojitoa, kwa kuwa hadi sasa mahusiano ya Tanzania na wafadhili yako vizuri.

Wamesema taarifa sahihi ni kuwa kwa muda wa miaka 8 fedha za wafadhili zilipungua kwa baadhi ya mambo ya mapambano ya UKIMWI na hiyo sio kwa Tanzania pekee bali nchi zote zinazotegemea wafadhili.

Kutokana na hilo, serikali iliunda Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI(ATF) ambao umewezesha serikali kununua septrin kwa miaka mitatu mfululizo.
1606417875592.png
 
Hatujawahi kushindwa vita.Iddi Amin tulimshinda t,hiyo 400k ya dawa haiwezi tushinda sisi ni nchi tajiri
 
Mabeberu haya tunachukua misaada yao,kwani dozi ya laki 4 kwa mwezi kila mgonjwa inatushinda kweli jamani kama nchi huru?

Ni USD 75 per person per year ndo gharama za matibabu hio ni kwa regimen mpya ya TLD ambayo ndo hutumika kama first line. Hio ni bei kwa nchi zinazoendelea kama yetu ila kwa nchi zilizoendelea inafika hadi $2000 hadi 10000.

Kwaio $75 X 1.6 million ( Ambayo ndo population with HIV TZ kwa 2018) = $120 million ambayo ni kama TSH 280 billion kwa mwaka. Kwaio tunaweza bana au mnasemaje??

IMG_4232.jpg



NB: Hayo ni makadilio rough tu kwa combination ya dawa moja tu tukumbuke kuna regimen zaidi ya 10 za ARV ambazo zinakua prescribed kwa wagonjwa tofauti tofauti kulingana indication zao na mahitaji. Hapo bado matibabu ya magonjwa nyemelezi, kukinga na kuzuia maambukizi mapya, Uzazi salama, vijana, N.K
 
Back
Top Bottom