Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Salaam wakuu,
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoani Tabora, imewaonya wanasiasa wote wanaofanya Kampeni kabla ya muda wa kisheria waache mara moja kufanya kampeni na kutoa Rushwa kwani ni kinyume cha Sheria.
Hivyo wataanza kukamatwa sababu Wanavunja Sheria.
Habari kwa kina...
TAKUKURU YAMTUHUMU ISMAEL ADEN RAGE KUFANYA KAMPENI KABLA YA WAKATI
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU mkoani Tabora ilimshikilia Mkurugenzi wa Voice of Tabora FM Redio, Ismael Aden Rage, Mei 23 kwa tuhuma za rushwa na kuanza kampeni kabla ya wakati
Rage ametoka kwa dhamana Mei 24, ametuhumiwa kuwakusanya wapiga kura na viongozi wa CCM ngazi ya kata na Matawi kwa lengo la kuwashawishi wampigie kura
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tabora, Mussa Chaulo amesema, kufanya kampeni kabla ya wakati ni kinyume cha sheria namba 11 ya mwaka 2007
Chaulo amewatahadharisha wenye nia ya kugombea kutowahonga watu pesa ili wapigiwe kura, pia wasivunje sheria kwa kujifanya kampeni kabla ya wakati
#JFSiasa #Rushwa #JamiiForums #Kampeni
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoani Tabora, imewaonya wanasiasa wote wanaofanya Kampeni kabla ya muda wa kisheria waache mara moja kufanya kampeni na kutoa Rushwa kwani ni kinyume cha Sheria.
Hivyo wataanza kukamatwa sababu Wanavunja Sheria.
Habari kwa kina...
TAKUKURU YAMTUHUMU ISMAEL ADEN RAGE KUFANYA KAMPENI KABLA YA WAKATI
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU mkoani Tabora ilimshikilia Mkurugenzi wa Voice of Tabora FM Redio, Ismael Aden Rage, Mei 23 kwa tuhuma za rushwa na kuanza kampeni kabla ya wakati
Rage ametoka kwa dhamana Mei 24, ametuhumiwa kuwakusanya wapiga kura na viongozi wa CCM ngazi ya kata na Matawi kwa lengo la kuwashawishi wampigie kura
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tabora, Mussa Chaulo amesema, kufanya kampeni kabla ya wakati ni kinyume cha sheria namba 11 ya mwaka 2007
Chaulo amewatahadharisha wenye nia ya kugombea kutowahonga watu pesa ili wapigiwe kura, pia wasivunje sheria kwa kujifanya kampeni kabla ya wakati
#JFSiasa #Rushwa #JamiiForums #Kampeni