Tabora Imesahaulika !

M-bongo

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
338
71
Ni ukweli usiopingika kuwa Mji wa Tabora umesahaulika sana kiasi cha watu kupaita Tabora Chuo cha Mafunzo yaani ukiweza kuishi Tabora basi hakuna Mkoa utakao kusumbua Hapa Tanzania, ukiwa Tabora na ukapata dharura yoyote ya safari ya nje ya tabora itakulazimu usubiri ratiba ya mabasi ndipo uweze toka maana Tabora ni kisiwa na kuna tetesi kuwa hata vigogo wa Nchi hawapendi sana kwenda Tabora sababu ya ahadi ya Ujenzi wa barabara imekuwa ya miaka na hakuna dalili licha ya ujenzi wa daraja la Malagalasi wana JF tuwasaidieni ndugu zetu wa Tabora kupiga kelele ili angalau wapate barabara nilichogundua sasa bila kelele mambo hayaendi
 
Ni ukweli usiopingika kuwa Mji wa Tabora umesahaulika sana kiasi cha watu kupaita Tabora Chuo cha Mafunzo yaani ukiweza kuishi Tabora basi hakuna Mkoa utakao kusumbua Hapa Tanzania, ukiwa Tabora na ukapata dharura yoyote ya safari ya nje ya tabora itakulazimu usubiri ratiba ya mabasi ndipo uweze toka maana Tabora ni kisiwa na kuna tetesi kuwa hata vigogo wa Nchi hawapendi sana kwenda Tabora sababu ya ahadi ya Ujenzi wa barabara imekuwa ya miaka na hakuna dalili licha ya ujenzi wa daraja la Malagalasi wana JF tuwasaidieni ndugu zetu wa Tabora kupiga kelele ili angalau wapate barabara nilichogundua sasa bila kelele mambo hayaendi

Karibu M-bongo lakini Tabora, anatoka Speaker Mzee Six, Waziri Kapuya, waziri Magreth, mh Seleli na viongozi wengine manatakiwa mjipange jamani msitegee fadhila za serikali
 
Yale yale -sasa watu toka Tbr wamejenga Dar, Mz na wanasema kwao miundombinu mibovu! Sasa wa kumlaumu ni nani?

Hivi Tbra na Kigoma wapi kuna uafadhali?
 
Yale yale -sasa watu toka Tbr wamejenga Dar, Mz na wanasema kwao miundombinu mibovu! Sasa wa kumlaumu ni nani?

Hivi Tbra na Kigoma wapi kuna uafadhali?

Nadhani heri ya Kigoma wako karibu na nchijirani hata upatikaji wa baadhi ya vitu ni nafuu...
 
We Unafikiri Baada Ya Kumtoa Yule Kijana Mchapakazi Na Mzalendo Halisi Ndugu Yetu Mpendwa,[magufuli]kuna Cha Barabara Tena Hapo We Zubaeni Mchekwe. Mkiona Inabana Hamieni Dar Tuje Tubanane.sasa Kumbe Tufanyeje Na Hayo Ndiyo Maendeleo Ya C C M Miaka Mingi Baada Uhuru. Na Mnacholalamika Ni Nini Wakati Mnajua Akili Zenu Ni Kama Za Samaki Maana Samaki Ndiye Kiumbe Mwenye Kumbukumbu Ndogo Kuliko Viumbe Vyote Duniani Maana Kama Hayo Yoote Mnayaona Inakuwaje Eti Ikifika Wakati Wa Uchaguzi Mnasahau Mara Moja Na Kuwachagua Tena Miaka Nenda Rudi Sasa Mtakula Jeuri Yeni
 
Ni ukweli usiopingika kuwa Mji wa Tabora umesahaulika sana kiasi cha watu kupaita Tabora Chuo cha Mafunzo yaani ukiweza kuishi Tabora basi hakuna Mkoa utakao kusumbua Hapa Tanzania, ukiwa Tabora na ukapata dharura yoyote ya safari ya nje ya tabora itakulazimu usubiri ratiba ya mabasi ndipo uweze toka maana Tabora ni kisiwa na kuna tetesi kuwa hata vigogo wa Nchi hawapendi sana kwenda Tabora sababu ya ahadi ya Ujenzi wa barabara imekuwa ya miaka na hakuna dalili licha ya ujenzi wa daraja la Malagalasi wana JF tuwasaidieni ndugu zetu wa Tabora kupiga kelele ili angalau wapate barabara nilichogundua sasa bila kelele mambo hayaendi

Kw ahilo wala hujakosea na kuongezea tu, si Tabora peke yake iliyosahaulika bali hata Tanga, Mtwara, Kilwa, Pwani, Mafia, Kigoma, Kondoa, sijui kwa nini?
 
Serikali Kwa Sasa Ilitakiwa Iwafikirie Wachapakazi Wake Wa Zamani Ambao Wengi Waliondolewa Wakati Wa Serikali Ya Kimajungu Ya Mhe Nkapa Wewe Unafikiri Wizara Kama Ya Ujenzi Leo Hii Angepewa Mtu Kama Nalaila Kiula Halafu Wakashirikiana Na Magufuli Tungekuwa Wapi? Nadhani Hata Hii Aibu Tunayoiona Sasa Hivi Ya Barabara Ya Sam Nujoma Ya Kilometa Moja Ambayo Inajengwa Sasa Mwaka Wa Nne Isingekuwepo. Et We Unazungumza Mambo Ya Tabora Mbali Kote Huko Sisi Watoto Wa Town Wenyewe Ambao Tunahitaji Kutembeza Michuma Yetu Ktk Barabara Za Dar Tumekwama Itakuwa Huko Labda Msubiri Siku Atakaporudi Yesu.hamieni Huku Dar Maana Hii Ni Nchi Yetu Wote Ya Nini Mteseke?huko Achieni Nyani Na Ngedere Waishi Huko Maana Hawahitaji Miundo Mbinu.
 
Serikali Kwa Sasa Ilitakiwa Iwafikirie Wachapakazi Wake Wa Zamani Ambao Wengi Waliondolewa Wakati Wa Serikali Ya Kimajungu Ya Mhe Nkapa Wewe Unafikiri Wizara Kama Ya Ujenzi Leo Hii Angepewa Mtu Kama Nalaila Kiula Halafu Wakashirikiana Na Magufuli Tungekuwa Wapi? Nadhani Hata Hii Aibu Tunayoiona Sasa Hivi Ya Barabara Ya Sam Nujoma Ya Kilometa Moja Ambayo Inajengwa Sasa Mwaka Wa Nne Isingekuwepo. Et We Unazungumza Mambo Ya Tabora Mbali Kote Huko Sisi Watoto Wa Town Wenyewe Ambao Tunahitaji Kutembeza Michuma Yetu Ktk Barabara Za Dar Tumekwama Itakuwa Huko Labda Msubiri Siku Atakaporudi Yesu.hamieni Huku Dar Maana Hii Ni Nchi Yetu Wote Ya Nini Mteseke?huko Achieni Nyani Na Ngedere Waishi Huko Maana Hawahitaji Miundo Mbinu.

Huu kama si upuuzi mtauitaje?
 
Tanga, Mtwara, Kilwa, Pwani, Mafia, Kigoma kondoa HIVI NYIE NI WANYAMA MPAKA MKAKOSA MBINU?KWANI HAWA VIONGOZI WOOTE WANATOKA DAR?SASA IWEJE WAMERUNDIKANA NA MBAYA ZAIDI WAMEWASAHAU? CHA KUFANYA NI NYIE PIA KUHAMIA DAR NA FAMILIA ILI MBANANE NAO MTAKUBALI VIPI MIAKA NENDA RUDI KUKAA BILA MIUNDO MBINU?NA KUWAACHA WAO WAKIISHI KIFALME KULE MASAKI?KARIBUNI SANA DAR HUKO WAACHIENI WANYAMA MAANA WAO HAWAHITAJI MIUNDO MBINU.
 
Tanga, Mtwara, Kilwa, Pwani, Mafia, Kigoma kondoa HIVI NYIE NI WANYAMA MPAKA MKAKOSA MBINU?KWANI HAWA VIONGOZI WOOTE WANATOKA DAR?SASA IWEJE WAMERUNDIKANA NA MBAYA ZAIDI WAMEWASAHAU? CHA KUFANYA NI NYIE PIA KUHAMIA DAR NA FAMILIA ILI MBANANE NAO MTAKUBALI VIPI MIAKA NENDA RUDI KUKAA BILA MIUNDO MBINU?NA KUWAACHA WAO WAKIISHI KIFALME KULE MASAKI?KARIBUNI SANA DAR HUKO WAACHIENI WANYAMA MAANA WAO HAWAHITAJI MIUNDO MBINU.

Anaendeleaza upuuzi kama ule alioufanya Msabaha bungeni ya kutaka kuwashughulikia kina six wakati yeye ndie aliyekuwa akishughulikiwa.
 
Igeni Mfano Wa Wachagga Wa Kule Kibosho Maana Wao Walidanganywa Na Serikali Kuwa Kwa Kuwaondoa Wale Wazungu Ktk Yale Mashamba Makubwa Maisha Yao Yangebadilika Na Kule Kibosho Kungekuwa Kama Nyuu Yok Wakaona Poa Lakini Cha Kushangaza Yale Mashamba Baada Tu Ya Miaka 10 Serikali Yenye Meno Mengi Na Tumbo Lisilojaa Ikatafuna Kila Kitu Na Kuacha Vumbi Tu Pale.wachaga Wala Hawakupiga Kelele Wakajua Tayari Tushatiwa Changa La Macho Kwa Hiyo Woote Wakawa Na Mkakati Wa Kuhamia Dar Na Baada Ya Miaka Kumi Mbeleni Kule Kibosho Walibaki Wazee Tu Na Vikongwe Na Na Sasa Hivi Wote Wako Dar Na Maisha Ni Mazuri Na Wanasaidia Kule Walikotoka Sasa Hivi Miaka Kama Mitano Iliyopita Serikali Hiyo Hiyo Wakaamua Kuwarudisha Wale Wazungu Kule Kibosho Na Mpaka Sasa Wameshaanza Kuzalisha Na Mashamba Yao Yamerudia Kama Enzi Ya Zamani Lakini Hayana Kibarua Hata Mmoja Mkibosho Vibarua Wote Wanatoka Sehemu Nyingine Kama Tanga Upareni Nk Sasa Nyie Huko Kama Hakuna Miundo Mbinu Mnangoja Nini?
 
Kwani Kuna Sheria Inayosema Raia Wa Tanzania Kuhamia Mkoa Mwingine Ni Kosa?sasa Kama Siyo Kosa Kinachokufanya Mtu Na Akili Zako Timamu Kukaa Ukiteseka Porini Au Kukaa Sehemu Isiyo Na Miundo Mbinu Au Sehemu Haina Hospital Au Shule Ni Nini?karibuni Dar Hapa Hakuna Kinachoshindikana Hata Hiyo Njaa Ya Mwaka Jana Niliyosikia Iliwatafuna Hapa Dar Hatujui Kitu Kama Hicho Na Hapa Kila Siku Ni Krismas Karibuni Karibuni Maana Sitaki Kusikia Eti Mtanzania Mwenzangu Anateseka Wakati Dar Sasa Tunashauriwa Na Dactari Tupunguze Kula Maana Tunaweza Kupata Kisukari Sasa Hivi Vyakula Tupeleke Wapi? Karibuni Sana
 
sasa wajameni,ikiwa wote ndugu Major watakwenda dar,watabanana vp?Maana Rukwa,tanga,Pwani,Lindi,Ntwara mikoa yote hiyo imesahaulika.
Wajameni tuwasaidieni kupiga kelele,lakini na wao pia,wasijenge Dar wakajenga TBR mji utakua tu,miundo mbinu itakuja.
 
Hiyo Mindo Mbinu Itashushwa Na Mungu?halikuniki Miaka Mingapi Tangu Uhuru Mpaka Leo Sasa Tuna Lugha Gani Mpya Ya Kuwadandanya Hawa Wana Tabora Wao Waje Tu Dar Tutaenea Tu
 
Yale yale -sasa watu toka Tbr wamejenga Dar, Mz na wanasema kwao miundombinu mibovu! Sasa wa kumlaumu ni nani? Hivi Tbra na Kigoma wapi kuna uafadhali?
Mkoa wa TBR uko nyuma ki maendeleo na umesahaulika, naungana na mkuu kweli tuwasaidie kupiga kelele ili angalau waweze kuwasili siku hiyo hiyo Dar.
Kingine kinachochangia watu wsijenge kwao (TBR) ni mambo ya ndumba na ngai.

Kw ahilo wala hujakosea na kuongezea tu, si Tabora peke yake iliyosahaulika bali hata Tanga, Mtwara, Kilwa, Pwani, Mafia, Kigoma, Kondoa, sijui kwa nini?
Kwa sasa angalau huu ukanda wa pwani una nafuu, baada ya barabara ya kibiti-lindi kuisha kwa 80%, Kilwa kutangazwa sehemu ya 'kuhistoria???' na UNESCO, kupatikana kwa umeme wa gasi kule MTR, na nimesikia kuwa bandari ya Mtwara itaanza kupokea meli kutoka nje soon. HIi ni faraja kwa ukanda huu wa pwani.

Sio Tabora, kulikuwa na viwanda 2, sido na nyuzi ambavyo vyote vipo kwenye koma kama sikosei.

Maisha magumu sana kule, unaweza kuzunguka kutwa nzima unatafuta change ya 10,000.

Poor Tabora,
 
Kasana,

Tupe mawazo interventions to address ngai na ndumba! Manake watu wanalalamikia Wakilimanjaro tu kuwa wanapendeleawa.. sasa Tbr wana Spika, Sita, Sileli, Kapuya- sasa kwa nini hatoi mchango wa kutosha? Au ndo sababu za ndumba?

Nakataa kuwa Tanga kumesahaulika..tutakuwa tunamkosea Mungu!
 
Kasana,

Tupe mawazo interventions to address ngai na ndumba! Manake watu wanalalamikia Wakilimanjaro tu kuwa wanapendeleawa.. sasa Tbr wana Spika, Sita, Sileli, Kapuya- sasa kwa nini hatoi mchango wa kutosha? Au ndo sababu za ndumba?

Nakataa kuwa Tanga kumesahaulika..tutakuwa tunamkosea Mungu!
Mkuu mimi kabila langu ni huko pamoja ya kuwa kwa sasa makazi yako kusini. Mara ya mwisho nilikatiza huko 5yrs ago, na nikatishwa na mambo ya kalumanzira, hivyo kwa mtazamo niliondoka nao huko sina hata dalili ya kujenga huko.

Seleli anajitahidi sana kuutetea huu mkoa, lakini zinatakiwa juhudi za wakazi wa mkoa huo waungane ili wa invest huko, la sivyo maendeleo ya kweli yatakuwa ni ndoto.
 
Wazalendo,

Si Tabora tu; inabidi kila mtu achangamkie maendeleo ya mkoa anaotoka, tufanye ushindani wa kimaendeleo kuendeleza mikoa pale panapowezekana. Nafikiri wengi hapo mikoa hii iliwasomesha shule za msingi, sekondari tena bure tuu! Hii ni mojawapo ya giving back to community" wekeni zile "investment" huko, (zile mnazotaka kuleta Tanzania baada ya kupata dual citizenships). Maana it takes a little kufanya watu waje kwa wingi na kukuza mji. Ukianzia huko Mtwara kwa kina Mkapa, Mrope, na rest of M, M, M's; mmesomeshwa na shule huko, sasa fanyeni shughuli za kuendeleza miji sio kusubiri SERIKALI tuu, Serikali huyu atafanya mangapi???

Na yie akina Katembo, Kifaru, Kasungura, Kifaru, Komba ,Simba na the rest of everyone mwenye jina la Wanyamawanyama, Ndegendege n.k. Huko mna madini ya kutosha tu, zaidi ile Magnesium; sasa angalieni mtaitumiaje kunufaisha Tanzania, na Songea yenu; pia huko kunatoa kahawa nzuri sana kama vile Kilimanjaro, sijui kwanini Kilimanjaro ndio iko kwenye ramani na Tanzania na ndio inapeta zaidi yenu.

Akina Shelukindo, Shekifu, Shemdasi, Shem nini sijui, tafuteni wenzenu wote wenye kuitwa She, She, na angalieni mtafanyaje pia, Lushoto being the one best area conducive for production of fruits, mtafanyaje ku-take advantage ya hiyo hali kuendeleza huko milimani na Tanzania kwa ujumla!

Inanikumbusha Profesa Ngware pale UD used to say, akisihi wanafunzi, "mtakapo maliza shule, tafadhali kama huna cha kufanya mjini rudini kijijini kwenu ukasaidie kuharakisha maendeleo ya kwenu", alisema "msibakie kung'ang'ania Dar es Salaam, maana mpaka sasa wenyewe tumeshatosha na kubanana, sasa mrudi kwenu hatutaki fujo". People used to get offended, lakini alikuwa na point.

Hii pia imenifanya nifikirie, hivi, mikoa tofauti imetoa watu tofauti, kuna need ya mimi mwenyewe kufanya utafiki na kuandika kitabu kufuatilia kile kilichoanzishwa na Dk.Bundara, labda, wachagga ndivyo walivyo, au wasukuma ndivyo walivyo, ama wahaya ndivyo walivyo-Inashangaza kuna mikoa ina rasilimali zote, na maendeleo yanakuwa madogo ama hamna, wakati sehemu nyingine yenye zile rasilimali zile zile, maendeleo yapo ya haraka haraka, KULIKONI??? Il'l update on my findings!

Na mwisho, while niko na sprit yaku-give back, ndugu zangu mlio-graduate from UD, It's about time, tuanze kusaidia Chuo Kikuu, (if you don't already do), nina-organize a society ya Alumni, kazi itakuwa ni kutoa misaada ya hali na mali pale panapowezekana. Someting like, Kisura Foundation, inatoa scholarship, inajenga nyumba za kulala, inanunua vitabu n.k. Especially nyie mliosoma bure pale UD, return, au to put it lightly, please give back, maana madeni mliokopeshwa mmegoma kulipa! Changia hata kitabu basi aah.

Asanteni.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom