Hossam
JF-Expert Member
- Feb 10, 2011
- 3,538
- 2,155
Ni sawa sisi Wanyanyembe, na kwa hakika hakuna awezaye kuleta mabadiliko Tabora au kuamua kukubali mabadiliko kwa faida ya Wanatabora na Watanzania kwa ujumla ila sisi wenyewe, lakini jee, Tabora haikupewa elimu sahihi ya uraia kwa wakati ama imechelewa kukubaliana na upepo wa mabadiliko?
Maana ni Tabora hii imewaelimisha wengi viongozi wetu, ni Tabora hii imekuwa ikikumbukwa kihistoria kama business center enzi zile za 1890s na hata nusu ya kwanza ya karne ya ishirini.
Tabora ina kila rasilimali zenye kuweza kuipaisha na kuifanya kinara wa maendeleo Tanzania, tupia macho misitu yetu uone mbao safi na asali, ona udongo wenye rutuba uwezao kuotesha mazao yote yote, sasa kwa nini tuko mkiani?
Hivi ni blanket la alfajili ya usingizi mtamu wa uzembe na wa kuzuia kuchangamka ama ni fikra potofu za wakoloni na kuogopa kivuli zimetufikisha mkiani?
Jee ni kweli mzigo mzito wa ujinga mpe mnyamwezi? Sina hakika kama tumecheleweshewa ama kutokukubali mageuzi ya kweli, kama asubuhi imefika basi tuamke wajameni.
G Kassanga.
Maana ni Tabora hii imewaelimisha wengi viongozi wetu, ni Tabora hii imekuwa ikikumbukwa kihistoria kama business center enzi zile za 1890s na hata nusu ya kwanza ya karne ya ishirini.
Tabora ina kila rasilimali zenye kuweza kuipaisha na kuifanya kinara wa maendeleo Tanzania, tupia macho misitu yetu uone mbao safi na asali, ona udongo wenye rutuba uwezao kuotesha mazao yote yote, sasa kwa nini tuko mkiani?
Hivi ni blanket la alfajili ya usingizi mtamu wa uzembe na wa kuzuia kuchangamka ama ni fikra potofu za wakoloni na kuogopa kivuli zimetufikisha mkiani?
Jee ni kweli mzigo mzito wa ujinga mpe mnyamwezi? Sina hakika kama tumecheleweshewa ama kutokukubali mageuzi ya kweli, kama asubuhi imefika basi tuamke wajameni.
G Kassanga.