Tabia ya kuomba hela halafu ukishatumiwa husemi imefika au kutoa shukrani sio nzuri

Maleven

JF-Expert Member
Sep 8, 2019
624
2,772
Yaani hata kama mtu hutatoa shukrani ila umjulishe tu alietuma kua hela imefika, lakini unakuta unamtumia mtu ikishafika ndio anapotea moja kwa moja hatoi shukrani wala hasemi kama hela imefika.

Hii tabia inakatisha sana tamaa
 
Tatizo mnakera mno ,unakuta mtu namba yako anaifahamu , majina yako unayotumia anayajua yote
Bado akituma hata dk kadhaa hazijapita anauliza umepata? Agrrr mnakera
 
Ni human nature lakini mm huwa siulizagi kama umepata au hujapata kitu muhimu ni jina lake tu lahuko napotuma.
 
Kupenda kushuuriwa sanaaa ni tabia ya umwinyi achana nayo

ukishampa inatosha
 
Hatufundishi watoto kushukuru wanaposaidiwa. Wakiwa watu wazima hivyo hivyo, hawashukuru kwa kitu chochote. Kila kitu wanaona ni haki yao tu. Siyo kwako tu. Inatokea mara nyingi sana. Hata wanaojiita wasomi ni hivyo hivyo. It is sad.
 
Watu wa namna hii ukiwatumia pesa break ya kwanza ni kwenda kwa wakala kutoa hela halafu anasubiri umpigie kumuuliza kama imefika au lah

Hana muda tena wa kukutafuta mana ameshapata hitaji lake
 
Back
Top Bottom