Ukijifanya una roho nzuri eti watu wataniona mbaya, utaishia kupata hasara mpaka ukome!
Mi mchana wa saa saba lunch time, nimeenda napopaki ( mwendo wa dk 3 na ofisini)
Huwa mda huo naenda kujilaza garini, wale waoshaji ni (wadada wafanya usafi hiyo sehemu) basi wamejaa kwenye boneti, matambara na ndoo zao za kuoshea Magari vyote wamevipandisha juu ya boneti la gari yangu, wanasubiri kula vichwa!
Nimeishia kuwaangalia tuu maana siwezi maneno na wanawake nna hasira mnoo!
Binafsi sipendi mtu asiyeheshimu kitu cha mwenzake!