witnessj
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 28,839
- 47,747
Haaaa haaaa haaaaTusio na magari tunakomaje? Nawaomba tuwavumilie wenye magari na vichambo na manyanyaso. Usishangae ukiwekewa tambara chini usichafue kapeti la gari, au kufungiwa mlango (ukifunga wewe utaharibu!!!). Usifungue vioo na Ac hawashi. achilia mbali yale maangalizo unayopewa utasikia... huko nyuma kuna laptop ... Gari hii sasa hivi Yadi ni Shilingi Milioni..... ukiagiza nje ni Shiling.... Mafuta ya kuweka shilingi elfu ishirini ishirini yanaharibu pampu... hata kama hujauliza. ole wako usimsifie utaisoma ya JPM.
Mada ya mwenye gari ni mada kuuu usianzishe mada na hata kuchangia kuwa mwangalifu hasa kama mwenye gari yuko na wife/mchepuko utasikia ile saiti ... viza inasumbua sana... exchange rate leo ilikuwa balaa. hivi zile milion tisa alilipa?
NDO SWAGA ZAO.
Kudadeki nimeanza kuweka akiba ya kununulia namimi gari kila mwezi naweka Sh 65,000/- ni mwezi wa tisa sasa. Hivi gari bei gani?
WENYE MAGARI BIG RESPECT KWENU LAKINI MUNGU ANAWAONA !!!!!!
....mkuu nimebaki nakuonea huruma tuu...Sio kwa kilio hiki
